Dr Alfred Kikoti ambaye ni Mkurugenzi wa kituo cha kimataifa cha utafiti wa Tembo(world Elephant Centre)akiwaelezea wananchi wa jiji la Arusha kuwa pale watakapowabaini majangiri wanao waua Tembo wawekwe kwenye website,mitandao ikiwa njia mojawapo ya kuwafichua majangiri hao.
Dk Alfred aliyasema hayo kwenye uwanja wa Aicc mara baada ya kumaliza matembezi ya Tembo ambapo kauli mbiu yao ilikuwa ni ''kila baada ya dk kumi na tano tembo anauwawa ''na kwamba kama hali itaendelea hivo baada ya miaka kumi na mbili Tanzania hatutakuwa na Tembo.
Alisema Tembo ni sawa na binadamu,meno ya tembo,pembe za ndovu wasivitumie kama biashara ni kwa ajili ya tembo,hivyo kujitahidi kukataa biashara haramu ya pembe za ndovu na kila Mtanzania kusema ''hapana''
MKUDE ASEMA USALAMA UMETIMIZWA: WANANCHI WATAKIWA KUPIGA KURA KWA AMANI
OKTOBA 29
-
Na Woinde Shizza, Arusha
Mamlaka za usalama katika Jiji la Arusha zimehakikisha maandalizi yote
muhimu yamekamilika kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktob...
6 days ago

No comments:
Post a Comment