Adbox
Showing posts with label Biashara. Show all posts
Showing posts with label Biashara. Show all posts

Tuesday, 22 July 2025

NBC Yakutana na Wateja Wake Wakubwa wa Jijini Arusha, Yajadili Fursa, Ufanisi wa Huduma Zake Kwa wateja.

7/22/2025 01:10:00 am


Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) imekutana na wateja wake wakubwa kutoka kampuni, wateja binafsi na taasisi mbali mbali (Corporates) wa jijini Arusha ili kujadili fursa za biashara, kutambulisha huduma mpya za benki hiyo sambamba na kuwaejengea uelewa zaidi wateja hao kuhusu faida na manufaa ya huduma hizo. Benki hiyo pia ilitumia fursa hiyo kujadili na wateja hao namna inavyoweza kuboresha huduma zake kulingana na mahitaji yao.

Katika kufanikisha hilo, jana benki hiyo kupitia timu yake ya Biashara na Uwekezaji (CIB) iliandaa hafla maalum ya chakula cha jioni iliyofanyika jijini humo ikiongozwa na Mkurugenzi wa Wateja Wakubwa wa benki hiyo Bw, Elvis Ndunguru sambamba na maofisa wengine waandamizi wa benki hiyo kutoka makao makuu na matawi yake ya jijini Arusha.

Akizungumza kwenye hafla hiyo Bw Ndunguru alisema tukio hilo ni muendelezo wa jitihada za benki hiyo kuendelea kuwa karibu zaidi na wateja wake kwa nia ya kutambulisha huduma zake mpya ikiwemo huduma ya NBC Connect mahususi kwa kundi hilo la wateja, kupata mrejesho wa huduma hizo kutoka kwa wateja hao sambamba na kutoa fursa kwa wateja kubadilishana fursa za biashara.

“Tukiwa kama muhimili muhimu wa utoaji wa huduma za kifedha nchini, NBC tunatambua umuhimu wa utoaji wa huduma bora kwa wateja na kukuza ushirikiano kati yetu na wateja wetu. Hii inasababishwa na mabadiliko yanayotokana na ubunifu na maendeleo ya kiteknolojia tunayoyafanya kila siku’’

“Hivyo hatua hii ya kukutana na wateja wetu wakubwa inatoa fursa kwetu kuelezea maboresho makubwa tuliyofanya kwenye huduma zetu hivi karibuni sambamba na kutambulisha huduma mpya zilizorahisishwa zaidi kidigitali na zinazoendana na mahitaji ya wateja wetu.’’ Alisema

Aidha, kupitia mpango huo benki hiyo imekuwa ikielezea mikakati yake mipana inayolenga kuwahudumia kwa ufanisi zaidi wateja hao, kuwajengea mitandao ya kibiashara miongoni mwao sambamba na kuwasogezea huduma za kibenki karibu zaidi huku huduma ya NBC Connect ikitajwa kama suluhisho muhimu katika kuwasogezea huduma za kibenki wateja hao wakubwa yakiwemo mashirika na kampuni binafsi, pamoja na taasisi za serikali.

“Tunaamini kuwa msingi wa huduma za kipekee ni kuelewa mahitaji na matakwa ya wateja wetu, matukio kama haya yanatupatia mitazamo au maono yanayotusaidia kuwa wabunifu zaidi na kuboresha uzoefu wa kibenki kwa ujumla.” Aliongeza Bw Ndunguru.

Aidha, Bw Ndunguru alitaja baadhi ya mambo muhimu ambayo benki hiyo imekuwa ikiyazingatia katika kukuza ushirikiano na taasisi za kibiashara hapa nchini kuwa ni pamoja na utoaji wa suluhisho zenye ubunifu katika huduma za kifedha, Ubunifu wa kiteknolojia, Ubia wa kimkakati, Kukuza Ukuaji wa Uchumi pamoja na Uwajibikaji kwa jamii huku kipaumbeke kikiwekwa zaidi kwenye masula ya Elimu, Afya na uhifadhi wa mazingira.

“Hivyo basi NBC tunazialika jumuiya za wafanyabiashara kuangalia fursa na faida za kushirikiana na taasisi hii ya fedha ambayo ina dhamira ya dhati na mafanikio yao, kwa kukuza ushirikiano na kutoa zana zinazohitajika katika ukuaji. NBC inalenga kuwa mshirika mwaminifu anaayetegemewa katika biashara hapa nchini,’’ alibainisha.

Wakizungumzia hatua hiyo baadhi ya wateja wa benki hiyo mkoani Arusha walisema imekuja wakati muafaka hasa katika kipindi hiki ambacho mkoa huo upo kwenye mapinduzi makubwa ya kiuchumi kutokana ustawi mkubwa wa sekta ya utalii ikiwa ni matunda ya jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan kupitia mkakati wake wa Royal Tour.

“Kwa sasa mkoa wa Arusha tupo kwenye kasi kubwa ya mabadiliko ya kiuchumi yanayochagizwa na ukuaji wa sekta ya utalii, biashara, kilimo na viwanda. Ni habari njema kwetu kuona kwamba benki ya NBC ambayo inatuhudumia wadau wengi kwenye sekta hizi inatuunga mkono kupitia huduma zao za kisasa ikiwemo zile za kidigitali ambazo kiukweli zimekuwa msaada mkubwa hususani kwenye huduma za miamala ya kifedha na makusanyo ya serikali,’’ alisema Bw Abdallah Kiwango kutoka Shirika la hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA).


Mkurugenzi wa Wateja Wakubwa wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) Bw, Elvis Ndunguru (kushoto) akizungumza na wageni waalikwa ambao ni wateja wa benki hiyo jijini Arusha wakati wa hafla ya chakula cha jioni iliyoandaliwa na benki hiyo kwa ajili ya wateja wake wakubwa kutoka makampuni, wateja binafsi na taasisi mbali mbali (Corporates) ili kujadili fursa za biashara, kutambulisha huduma mpya sambamba na kuwaejengea uelewa zaidi wateja hao kuhusu faida na manufaa ya huduma hizo. Hafla hiyo iliyoandaliwa kupitia timu ya Biashara na Uwekezaji (CIB) ya benki hiyo ilifanyika jana jioni jijini Arusha.


Mkurugenzi wa Wateja Wakubwa wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) Bw, Elvis Ndunguru (kulia) akibadilishana Mawazo na baadhi ya wateja wa benki hiyo jijini Arusha wakati wa hafla ya chakula cha jioni iliyoandaliwa na benki hiyo kwa ajili ya wateja wake wakubwa kutoka makampuni, wateja binafsi na taasisi mbali mbali (Corporates) ili kujadili fursa za biashara, kutambulisha huduma mpya sambamba na kuwaejengea uelewa zaidi wateja hao kuhusu faida na manufaa ya huduma hizo. Hafla hiyo iliyoandaliwa kupitia timu ya Biashara na Uwekezaji (CIB) ya benki hiyo ilifanyika jana jioni jijini Arusha.





Mkurugenzi wa Wateja Wakubwa wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) Bw, Elvis Ndunguru (katikati aliesimama) akisalimiana na baadhi ya wateja wa benki hiyo jijini Arusha wakati wa hafla ya chakula cha jioni iliyoandaliwa na benki hiyo kwa ajili ya wateja wake wakubwa kutoka makampuni, wateja binafsi na taasisi mbali mbali (Corporates) ili kujadili fursa za biashara, kutambulisha huduma mpya sambamba na kuwaejengea uelewa zaidi wateja hao kuhusu faida na manufaa ya huduma hizo. Hafla hiyo iliyoandaliwa kupitia timu ya Biashara na Uwekezaji (CIB) ya benki hiyo ilifanyika jana jioni jijini Arusha.






Baadhi ya wateja wa benki ya NBC jijini Arusha wakifuatilia hafla hiyo







Mkurugenzi wa Wateja Wakubwa wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) Bw, Elvis Ndunguru (kulia) sambamba na maofisa wengie wa benki hiyo wakizungumza na wageni waalikwa ambao ni wateja wa benki hiyo jijini Arusha wakati wa hafla ya chakula cha jioni iliyoandaliwa na benki hiyo kwa ajili ya wateja wake wakubwa kutoka makampuni, wateja binafsi na taasisi mbali mbali (Corporates) ili kujadili fursa za biashara, kutambulisha huduma mpya sambamba na kuwaejengea uelewa zaidi wateja hao kuhusu faida na manufaa ya huduma hizo. Hafla hiyo iliyoandaliwa kupitia timu ya Biashara na Uwekezaji (CIB) ya benki hiyo ilifanyika jana jioni jijini Arusha.

Wednesday, 10 September 2014

KIVUKO CHA MV. KIGAMBONI KUANZA KAZI KESHO KUTWA

9/10/2014 04:04:00 pm


Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Watendaji mbalimbali hawapo pichani kutoka, Wizara ya Ujenzi, TEMESA na Kikosi cha Maji cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) ambao wamefanya kazi kubwa ya ukarabati wa Kivuko cha MV Kigamboni.
Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akipanda ngazi kwenda kukagua Kivuko cha MV Kigamboni ambacho matengenezo yake makubwa yanakamilika leo.
Luteni Kanali Gwanafi kulia akimuongoza Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwenda kukagua Kivuko cha MV Kigamboni sehemu ya chini mara baada ya kukamilika kwa ukarabati wake.
Luteni Kanali Gwanafi wapili kutoka kulia akitoa maelezo kuhusu ukarabati mkubwa wa Kivuko cha MV Kigamboni kama inavyoonekana.
Taswira-Kivuko cha MV Kigamboni kinavyoonekana mara baada ya Ukarabati wake.
Luteni Kanali Gwanafi kulia akimuonesha Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli sehemu ya juu ya Kivuko cha MV Kigamboni.
Luteni Kanali Gwanafi kushoto akimuonyesha Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Mhandisi Mussa Iyombe kuhusu sehemu ya chini ilivyokarabatiwa.
Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa ndani ya kivuko cha MV Kigamboni huku akipatiwa maelezo kuhusu ukarabati wake.
Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimsikiliza kwa makini Luteni Kanali Gwanafi kuhusu mambo mbalimbali wanayofanya ndani ya kivuko cha MV Kigamboni.
Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akitoka ndani ya Kivuko cha MV Kigamboni mara baada ya ukaguzi wake. Picha zote kwa Hisani ya Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Wizara ya Ujenzi.


Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli amesema kuwa Kivuko cha MV Kigamboni kinatarajiwa kuanza safari zake za usafirishaji rasmi kesho kutwa mara baada ya ukarabati wake kukamilika.

Waziri wa Magufuli alitoa kauli hio leo wakati akikagua kivuko hicho ambacho kilikuwa kikikarabatiwa na Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) kupitia kikosi cha Wanamaji.

Mheshimiwa Magufuli aliongeza kuwa hicho ambacho kinategemewa na wananchi wengi waishio Kigamboni na maeneo jirani kinategemewa kuteremshwa majini kesho jioni mara baada ya maji kujaa na kesho kutwa kuanza rasmi shughuli zake za usafirishaji.

“Nimekagua na kujionea kazi inavyoendelea na nimeridhishwa na mlipofikia mpaka sasa, naamini kazi imefanyika ipasavyo, hivyo basi palipobaki ni matengenezo madogo, kutokana na utendaji wenu wa kazi naamini kesho Kivuko hicho kitateremshwa majini na kesho kutwa kuanza safari”, Alisema Waziri Magufuli.

Aidha, Mheshimiwa Magufuli alikipongeza kikosi hicho cha Navy kwa kufanya kazi usiku na mchana kuhakikisha kuwa wanamaliza ukarabati huo kwa wakati licha ya changamoto nyingi walizokumbana nazo.

Sambamba na hilo, Waziri Magufuli amesema kuwa ndani ya Wiki tatu au nne Boti ya Kutoka Dar hadi Bagamoyo itawasili kwani imeshateremshwa majini huko inapotengenezwa na kilichobaki ni kuifikisha Dar es Salaam

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Mhandisi Mussa Iyombe, amepongeza Jeshi la Wananchi Tanzania kupitia Kikosi cha majini kwa uzalendo wao waliouonesha kwa kukamilisha ujenzi huo kwa gharama nafuu na kwa wakati ili kurejesha huduma za usafirishaji.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA), Mhandisi Marceline Magessa amesema kuwa ukarabati wa MV Kigamboni ulikuwa katika hatua za marekebisho mbalimbali ikiwemo utoaji kutu, kupaka rangi, usafi na uzibaji wa matundu pembezoni mwa kivuko hicho.

Naye kamanda wa kikosi cha majini Brigedia Jenerali Rogastian Laswai amezitaja changamoto zilizowakabili wakati wa utengenezaji wa kivuko hicho kuwa ni pamoja na kushindwa kupaka rangi kutokana na uwepo wa mvua pamoja na kupwa na kujaa kwa maji

Ukarabati wa Kivuko cha MV Agosti 14 mwaka huu mpaka kukamilika kwake hivi leo.

Monday, 10 February 2014

BANANA INVESTMENT YATOA ZAWADI KWA MAWAKALA WAO.

2/10/2014 01:20:00 pm

Mshindi wa kwanza kitaifa ni Bw. Peter Assenga kutoka Morogoro aliyejishindia zawadi ya Gari,hapa akionyesha ufunguo wake katika sherehe zilizoandaliwa na kampuni ya Banana Investment iliopo jijini Arusha.  Mshindi wa pili ni Dorothea kutoka Rombo, Tarakea , na Mshindi wa tatu alipata friji ambae ni Bw. Ibrahim Kikweche kutoka Dar es Salaam. washindi wengine kutoka Arusha ni Bw. Zefania Kira kutoka Namanga aliyeshishindia Tv, Bw. Victor Massawe kutoka Mbuguni aliyejishindia Flat Screen Tv, Bw. Gabriel Shibu Kutoka Ulonga Shangarai

Mmoja wa wakala akipokea zawadi ya Flat Screen TV' 21'' katika sherehe zilizoandaliwa na kampuni ya Banana Investment iliopo Moshono, jijini Arusha.
Wakala akipokea zawadi yake katika sherehe za kuwakabidhi zawadi zilizoandaliwa na kampuni ya Banana Investment iliopo jijini Arusha. Kwa picha Zaidi Bofya hapa >>>

Wednesday, 11 September 2013

Wednesday, 4 September 2013

Adbox