Adbox
Showing posts with label Habari. Show all posts
Showing posts with label Habari. Show all posts

Tuesday, 29 July 2025

WATOTO WATANO WAMEFARIKI DUNIA KWA MOTO TABORA

7/29/2025 07:56:00 pm

 







NA LUCAS RAPHAEL,TABORA 


Watoto watano wamefarikia dunia wengine 17 wamenusurika kifo baada ya kuwaka kwa bweni la wasichana  kwa kushika  moto katika kituo cha kulelea watoto yatima cha Igambilo kilichapo kata ya Misha  manispaa Tabora Mkonia hapa.

Akizungumza na waandishi wa habari mkurungezi wa kituo hicho na mwasisi wake Halima Laswai alisema kwamba kituo tukio lilitokea mida ya saa 5 usiku baada ya kudai kutokea shot ya umeme.  

Alisema kwamba mara baada ya kupata taarifa hiyo alipinga simu kituo cha kizima moto na kutoa ushiriiano kwa ajili ya kuzima moto huo.

Alisema kwamba wakazi wa kijiji hicho cha misha walifanya kazi kubwa kwa ajili ya kuzima moto na kuokoa vitu mbalimbali vilivyokuwepo eneo hilo.

Alisema kwamba Chanzo kilikuwa  umeme unawake na kuzima kisha balubo moja kupasuka na kutoa cheche zilizoangukia kwenye moja ya godoro kwenye kitanda na kuzalisha moto uliosambaa .

Halima alisema kwamba vitu mbalimbali vimeteketea na moto vikiwemo vyakula ambavyo vilikuwa upande wa bweni hilo lillilo shika moto.

Alisema vingine ni vifaa vyote vya shule walivyokuwa wanatumia watoto hao kwa ajili ya maosmo vikimo madfutari na sare ,kwani wengi ya watoto wanasoma shule za msingi.

“Watakwenda kuomba uongozi wa shule ya msingi ili watoto hao waweze kutumia nguo za nyumbani kwa ajili ya kuendelea na masomo yao hasa wale walipo kwenye madarasa ya mitihani ambayo ni Darasa la saba na Nne”alisema Halima

Mkurungezi huyo aliaendelea kubainishwa kwamba kutokana na hali hiyo wawalifanikiwa kuokoa maguni mawili ya unga na Mwili ya maharagwe.

Aidha wanaomba wasamalia wema kujitoa kwa ajili ya kuwasidia watoto wao ili waweza kurudia katika hali zao za kawaida kwa ajili ya kupatia vifaa vya shule na chakula

Afisa ustawi wa kituo hicho. Mwajuma Hassani alisema kwamba mida hile ya usiku akiwa amelala upande mwingine wa bweni kwenye kituo hicho alsiia watoto wanapinga kelele za kuomba masaa na kusema moto moto.

Alisema ndipo walipotoka kwenda kwenye bweni lililoshika na moto na kuvunja mlango wa geti na kufanikiwa kuwatoa watoto ila moshi ulikuwa ni mwingi sana .

Alisema walibofika faya walianza zozezi la kuzima moto ila kipindi hicho wenyeji wa eneo hilo walikuwepo kuwasaidia kuzima moto huo  

Alisema kwamba bweni hilo lilikuwa na watoto waliokuwa wanalala ni 23 kati yao walifariki ni 5 na 17 wamenurika na ajili hiyo ya moto.

kamanda wa jeshi la zimamotona  uokoaji mkoani Tabora Mohamed Jihad aliwataja walifarikia kuwani Pili Nasoro (5) Nusra Adam (11)Amina Ismail(7)Tatu Sharif (4) Norata Bakari (5)

Alibainisha kwamba tuki hilo limeleta simazi kubwa katika mkoa wa Tabora licha ya hali hiyo tahadhari zinatakiwa kuchyukuliwa ili kuoka majanga kama hayo.

Alisema kwamba ushari unaotolewa na jeshi hilo lnafuta kuchukuliwa kwa umakini mkubwa ili kuweza kupunguza ajili zinazoweza kusabishwa namoto.

Hata hivyo waliwataka wananchi na Taasisi mbali  mbali kuchukua hatua za tadhari kwa kuangali vifaa kinga kama vinafanya kazi ipasavyo  na kufanya ukaguzi wa mara kwa mara katika majengo na nyumba za kuishi

kituo hicho ni kiliazishwa mwaka 1997 kikiwa na watoto 7 tu na sasa kituo hicho kinawatoto wapatao 50 ila waliotoka ni wengi ambao wapo sehemu mbalimbali kwa ajili ya elimu ya juu na kati 

WATUMISHI OFISI YA WAZIRI MKUU WATAKIWA KUONGEZA BIDII KATIKA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAO.

7/29/2025 12:30:00 pm

NA.MWANDISHI WETU - DODOMA

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi amewaasa Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu kuendelea kufanya kazi kwa bidii na weledi mkubwa katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku.


Ameyasema hayo Tarehe 29 Julai, 2025 wakati akifungua Mkutano na Watumishi wa Ofisi hiyo ambapo alisema kuwa ni  muhimu kuwa na nidhamu ya kazi, kushirikiana na kuendelea kuwa wabunifu katika majukumu ya kila siku, na kuwakumbusha watumishi kuwa kazi wanazofanya zinagusa maisha ya mamilioni ya wananchi, hivyo ni wajibu wa kila mtumishi kuhakikisha anatoa huduma bora na kwa viwango vya juu. 


“Pia, nawasihi kuendelea kujenga mshikamano miongoni mwenu. Tunaposhirikiana, tunajenga nguvu ya pamoja ambayo hakuna changamoto inayoweza kutuzuia. Nawaomba tuendelee kufanya kazi kwa bidii na kwa moyo mmoja. Kumbukeni kuwa, kila mchango wenu una thamani kubwa katika kufanikisha malengo ya Ofisi yetu na Taifa kwa ujumla.” Alifafanua Dkt. Yonazi.


Katibu Mkuu Yonazi aliendelea kusema kuwa, katika kuboresha Ofisi hiyo kwa mwaka wa fedha 2025/2026, Ofisi imeendelea kuboresha mazingira ya kazi kwa kushughulikia changamoto zinazohusu mazingira ya kazi na maslahi ya wafanyakazi ikiwa ni pamoja na  kukuza ubunifu katika utendaji kazi wa kila siku na kuimarisha mifumo bora zaidi ya kufuatilia maendeleo ya kazi na kuhakikisha kila mfanyakazi anawajibika ipasavyo kwa nafasi yake.

Katika Mkutano huo watumishi wataweza kupata Elimu kutoka kwa wataalam wa  Mfuko wa Uwekezaji wa UTT kuhusu umuhimu wa kuwekeza, pamoja na mambo mengine pia watapewa elimu  itakayowakumbusha masuala mbalimbali yanayohusu uzingatiaji wa maadili ya utumishi wa umma, masuala ya Afya hususan homa ya ini na magonjwa yasiyoambukizwa.

Monday, 28 July 2025

CCM INATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE MUDA HUU,MBIVU NA MBICHI KUJULIKANA LEO

7/28/2025 06:09:00 pm
Dodoma

Katibu wa Siasa, mafunzo na uenezi CPA Amos Makala anatarijia kutangaza majina ya wagombea Ubunge, udiwani pamoja na nafasi za uwakilishi wa viti maalum kupitia tiketi ya chama cha mapinduzi kuelekea uchaguzi mkuu wa mwezi Oktoba 2025.

Tembelea DOREEN BLOG NA DOREEN TV mara kwa mara upate habari motomoto na uhakika.



DKT. TULIA AITAKA DUNIA KUKABILIANA NA VIKWAZO VINAVYOWAKWAMISHA WANAWAKE

7/28/2025 05:54:00 pm


Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Mhe. Dkt. Tulia Ackson, ameongoza majadiliano muhimu yaliyoandaliwa na UN Women kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, yaliyolenga kutafuta suluhisho la kudumu kwa changamoto zinazowakabili wanawake na wasichana duniani.



Majadiliano haya yamefanyika  katika Ukumbi wa Mikutano wa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, New York, Marekani. Mjadala umejikita katika kuainisha mikakati bora ya kutekeleza ahadi zilizowekwa katika Ajenda ya 2030, Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs), Ajenda ya Wanawake, Amani na Usalama, pamoja na Azimio la Beijing.

Aidha, washiriki wamebainisha kuwa changamoto kama ukosefu wa elimu na mifumo dhaifu ya afya zinaweza kutatuliwa iwapo jamii zitajitahidi kulinda mafanikio yaliyopatikana, kwa kuimarisha mifumo ya kisheria, kisiasa na kifedha kwa ajili ya kuendeleza usawa wa kijinsia.



Katika mchango wake, Mhe. Dkt. Tulia Ackson amesisitiza umuhimu wa kuweka usawa wa kijinsia na utekelezaji wa Ajenda ya 2030 kuwa vipaumbele vya kimataifa, huku akitoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kuungana katika kukabiliana na vikwazo vinavyokwamisha juhudi za Umoja wa Mataifa katika kuwawezesha wanawake na wasichana. 

Amesisitiza kuwa “wakati wa kuchukua hatua ni sasa”, hasa wakati ambapo dunia inakabiliwa na changamoto nyingi zinazotishia maendeleo ya kijinsia.

Thursday, 24 July 2025

JAB Yakabidhi Press Card kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Michuzi Media Group

7/24/2025 05:57:00 pm
IMG-20250723-WA0078
IMG-20250723-WA0081
●Waandishi Wengine Watakiwa Kuhakiki Viambatisho Katika Mfumo


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam


Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amemkabidhi rasmi Kitambulisho cha Uandishi wa Habari (Press Card) Mkurugenzi Mtendaji wa Michuzi Media Group, Muhidin Issa Michuzi, kwa niaba ya waandishi wengine wanaoendelea kukamilisha taratibu za kupata vitambulisho hivyo.


Hafla ya makabidhiano hayo imefanyika jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa jukumu la Bodi hiyo katika kuhakikisha kuwa waandishi wote nchini wanakuwa na vitambulisho halali kwa mujibu wa Sheria ya Huduma za Habari Na. 12 ya mwaka 2016.


IMG-20250723-WA0072
IMG-20250723-WA0079
Akizungumza baada ya kukabidhi kitambulisho hicho, Wakili Kipangula amempongeza Michuzi pamoja na waandishi wengine waliokwishapatiwa vitambulisho vyao kwa kufuata taratibu na kukidhi vigezo vinavyotakiwa kisheria.


Amesisitiza kuwa mchakato wa utoaji wa vitambulisho bado unaendelea na ametoa wito kwa waandishi ambao maombi yao hayajakamilika kuingia katika mfumo rasmi wa Bodi ili kuhakiki viambatisho walivyowasilisha.
IMG-20250723-WA0077
IMG-20250723-WA0073


“Kuna baadhi ya waombaji ambao viambatisho vyao havifunguki, havisomeki, vimerudiwa au havikidhi matakwa ya kisheria kama vile vyeti visivyotambulika au kukosekana kwa barua za utambulisho kutoka kwa waajiri,” amesema Wakili Kipangula.


Ametoa rai kwa waandishi kuhakikisha wanafuata maelekezo yanayotolewa kupitia mfumo kabla ya kuwasiliana moja kwa moja na Bodi kuhusu hali ya maombi yao.
IMG-20250723-WA0074
IMG-20250723-WA0075
JAB imekuwa ikitekeleza jukumu la kuthibitisha na kusimamia maadili ya taaluma ya uandishi wa habari nchini, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha wanahabari wanatambulika rasmi na kuwa na vitambulisho halali vinavyotolewa kwa mujibu wa sheria.


Michuzi ameishukuru Bodi kwa mchakato huo na kuwataka waandishi wengine kuhakikisha wanazingatia taratibu ili kuimarisha tasnia ya habari kwa weledi na uwajibikaji.

RAIS SAMIA KUWA MGENI RASMI MAADHIMISHO SIKU YA MASHUJAA KESHO JULAI 25 MWAKA HUU

7/24/2025 04:14:00 pm

Na Doreen Aloyce, Dodoma

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mashujaa yatakayofanyika 25 Julai, 2025 katika Viwanja vya Mnara wa Mashujaa vilivyopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma.

Akizungumza leo Julai 24 ,2025 Jijini Dodoma na waandishi wa habari jijini Dodoma kwa niaba ya Kamati ya Maandalizi ya Maadhimisho hayo, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko (Mb), amesema maadhimisho hayo ni alama muhimu ya kuenzi mchango wa Watanzania waliojitolea kwa ajili ya uhuru, amani na maendeleo ya Taifa.



 “Siku ya Mashujaa ni siku ya kitaifa inayotukumbusha uzalendo wa mashujaa wetu  waliolinda mipaka ya Taifa, waliopambana kwa ajili ya uhuru na waliotoa sadaka kubwa kwa ajili ya amani tunayoifurahia leo,” amesema Dkt. Biteko.

Ameeleza Maandalizi ya maadhimisho hayo yamekamilika, huku akisisitiza kuwa Julai 24, 2025 saa 6:00 usiku, Mwenge wa Kumbukumbu ya Mashujaa utawashwa rasmi na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mheshimiwa Rosemary Senyamule kwa niaba ya Rais, kuashiria kuanza kwa siku ya maombolezo ya mashujaa wa Taifa.



Amesema Maadhimisho ya Julai 25 yataanza saa 3:00 asubuhi kwa gwaride rasmi la heshima linaloongozwa na Vikosi vya Ulinzi na Usalama. Usiku wa siku hiyo, saa 6:00, Mwenge wa Kumbukumbu utazimwa rasmi kuashiria hitimisho la shughuli za maadhimisho kwa mwaka huu.

Mbali na hayo Dkt. Biteko ametoa wito kwa wananchi kushiriki kwa wingi katika tukio hilo muhimu kwa historia ya Taifa, akieleza kuwa kila Mtanzania anao wajibu wa kutambua na kuenzi mchango wa mashujaa kwa vitendo vya uzalendo, mshikamano na kuchapa kazi kwa maendeleo ya nchi.



“Tunapoadhimisha siku hii, tunapaswa kujiuliza: Je, sisi kama kizazi cha sasa tunaendeleza misingi waliyoiacha mashujaa wetu? Ushujaa hauishii vitani pekee, bali uko katika kila tendo jema kwa Taifa letu,” amesisitiza.

Amevitaka vyombo vya habari, wanahabari na watumiaji wa mitandao ya kijamii kushirikiana na Serikali katika kuelimisha umma kuhusu maana, historia na umuhimu wa Siku ya Mashujaa.

“Hii ni siku ya kumkumbuka Mtanzania mwenzetu aliyesimama kwa ajili ya wengine,tuwaambie watoto wetu maana ya ushujaa, thamani ya kujitolea, na umuhimu wa kupenda Taifa lao,” amesema Dkt. Biteko.

Maadhimisho ya Siku ya Mashujaa hufanyika kila mwaka nchini kote kama njia ya kuenzi maisha, mchango na maono ya waliolinda uhuru wa Taifa, na mwaka huu 2025, Serikali imepanga kuyafanya kwa heshima, uzito na mshikamano wa hali ya juu.

=MWISHO=

Tuesday, 22 July 2025

NBC Yakutana na Wateja Wake Wakubwa wa Jijini Arusha, Yajadili Fursa, Ufanisi wa Huduma Zake Kwa wateja.

7/22/2025 01:10:00 am


Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) imekutana na wateja wake wakubwa kutoka kampuni, wateja binafsi na taasisi mbali mbali (Corporates) wa jijini Arusha ili kujadili fursa za biashara, kutambulisha huduma mpya za benki hiyo sambamba na kuwaejengea uelewa zaidi wateja hao kuhusu faida na manufaa ya huduma hizo. Benki hiyo pia ilitumia fursa hiyo kujadili na wateja hao namna inavyoweza kuboresha huduma zake kulingana na mahitaji yao.

Katika kufanikisha hilo, jana benki hiyo kupitia timu yake ya Biashara na Uwekezaji (CIB) iliandaa hafla maalum ya chakula cha jioni iliyofanyika jijini humo ikiongozwa na Mkurugenzi wa Wateja Wakubwa wa benki hiyo Bw, Elvis Ndunguru sambamba na maofisa wengine waandamizi wa benki hiyo kutoka makao makuu na matawi yake ya jijini Arusha.

Akizungumza kwenye hafla hiyo Bw Ndunguru alisema tukio hilo ni muendelezo wa jitihada za benki hiyo kuendelea kuwa karibu zaidi na wateja wake kwa nia ya kutambulisha huduma zake mpya ikiwemo huduma ya NBC Connect mahususi kwa kundi hilo la wateja, kupata mrejesho wa huduma hizo kutoka kwa wateja hao sambamba na kutoa fursa kwa wateja kubadilishana fursa za biashara.

“Tukiwa kama muhimili muhimu wa utoaji wa huduma za kifedha nchini, NBC tunatambua umuhimu wa utoaji wa huduma bora kwa wateja na kukuza ushirikiano kati yetu na wateja wetu. Hii inasababishwa na mabadiliko yanayotokana na ubunifu na maendeleo ya kiteknolojia tunayoyafanya kila siku’’

“Hivyo hatua hii ya kukutana na wateja wetu wakubwa inatoa fursa kwetu kuelezea maboresho makubwa tuliyofanya kwenye huduma zetu hivi karibuni sambamba na kutambulisha huduma mpya zilizorahisishwa zaidi kidigitali na zinazoendana na mahitaji ya wateja wetu.’’ Alisema

Aidha, kupitia mpango huo benki hiyo imekuwa ikielezea mikakati yake mipana inayolenga kuwahudumia kwa ufanisi zaidi wateja hao, kuwajengea mitandao ya kibiashara miongoni mwao sambamba na kuwasogezea huduma za kibenki karibu zaidi huku huduma ya NBC Connect ikitajwa kama suluhisho muhimu katika kuwasogezea huduma za kibenki wateja hao wakubwa yakiwemo mashirika na kampuni binafsi, pamoja na taasisi za serikali.

“Tunaamini kuwa msingi wa huduma za kipekee ni kuelewa mahitaji na matakwa ya wateja wetu, matukio kama haya yanatupatia mitazamo au maono yanayotusaidia kuwa wabunifu zaidi na kuboresha uzoefu wa kibenki kwa ujumla.” Aliongeza Bw Ndunguru.

Aidha, Bw Ndunguru alitaja baadhi ya mambo muhimu ambayo benki hiyo imekuwa ikiyazingatia katika kukuza ushirikiano na taasisi za kibiashara hapa nchini kuwa ni pamoja na utoaji wa suluhisho zenye ubunifu katika huduma za kifedha, Ubunifu wa kiteknolojia, Ubia wa kimkakati, Kukuza Ukuaji wa Uchumi pamoja na Uwajibikaji kwa jamii huku kipaumbeke kikiwekwa zaidi kwenye masula ya Elimu, Afya na uhifadhi wa mazingira.

“Hivyo basi NBC tunazialika jumuiya za wafanyabiashara kuangalia fursa na faida za kushirikiana na taasisi hii ya fedha ambayo ina dhamira ya dhati na mafanikio yao, kwa kukuza ushirikiano na kutoa zana zinazohitajika katika ukuaji. NBC inalenga kuwa mshirika mwaminifu anaayetegemewa katika biashara hapa nchini,’’ alibainisha.

Wakizungumzia hatua hiyo baadhi ya wateja wa benki hiyo mkoani Arusha walisema imekuja wakati muafaka hasa katika kipindi hiki ambacho mkoa huo upo kwenye mapinduzi makubwa ya kiuchumi kutokana ustawi mkubwa wa sekta ya utalii ikiwa ni matunda ya jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan kupitia mkakati wake wa Royal Tour.

“Kwa sasa mkoa wa Arusha tupo kwenye kasi kubwa ya mabadiliko ya kiuchumi yanayochagizwa na ukuaji wa sekta ya utalii, biashara, kilimo na viwanda. Ni habari njema kwetu kuona kwamba benki ya NBC ambayo inatuhudumia wadau wengi kwenye sekta hizi inatuunga mkono kupitia huduma zao za kisasa ikiwemo zile za kidigitali ambazo kiukweli zimekuwa msaada mkubwa hususani kwenye huduma za miamala ya kifedha na makusanyo ya serikali,’’ alisema Bw Abdallah Kiwango kutoka Shirika la hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA).


Mkurugenzi wa Wateja Wakubwa wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) Bw, Elvis Ndunguru (kushoto) akizungumza na wageni waalikwa ambao ni wateja wa benki hiyo jijini Arusha wakati wa hafla ya chakula cha jioni iliyoandaliwa na benki hiyo kwa ajili ya wateja wake wakubwa kutoka makampuni, wateja binafsi na taasisi mbali mbali (Corporates) ili kujadili fursa za biashara, kutambulisha huduma mpya sambamba na kuwaejengea uelewa zaidi wateja hao kuhusu faida na manufaa ya huduma hizo. Hafla hiyo iliyoandaliwa kupitia timu ya Biashara na Uwekezaji (CIB) ya benki hiyo ilifanyika jana jioni jijini Arusha.


Mkurugenzi wa Wateja Wakubwa wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) Bw, Elvis Ndunguru (kulia) akibadilishana Mawazo na baadhi ya wateja wa benki hiyo jijini Arusha wakati wa hafla ya chakula cha jioni iliyoandaliwa na benki hiyo kwa ajili ya wateja wake wakubwa kutoka makampuni, wateja binafsi na taasisi mbali mbali (Corporates) ili kujadili fursa za biashara, kutambulisha huduma mpya sambamba na kuwaejengea uelewa zaidi wateja hao kuhusu faida na manufaa ya huduma hizo. Hafla hiyo iliyoandaliwa kupitia timu ya Biashara na Uwekezaji (CIB) ya benki hiyo ilifanyika jana jioni jijini Arusha.





Mkurugenzi wa Wateja Wakubwa wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) Bw, Elvis Ndunguru (katikati aliesimama) akisalimiana na baadhi ya wateja wa benki hiyo jijini Arusha wakati wa hafla ya chakula cha jioni iliyoandaliwa na benki hiyo kwa ajili ya wateja wake wakubwa kutoka makampuni, wateja binafsi na taasisi mbali mbali (Corporates) ili kujadili fursa za biashara, kutambulisha huduma mpya sambamba na kuwaejengea uelewa zaidi wateja hao kuhusu faida na manufaa ya huduma hizo. Hafla hiyo iliyoandaliwa kupitia timu ya Biashara na Uwekezaji (CIB) ya benki hiyo ilifanyika jana jioni jijini Arusha.






Baadhi ya wateja wa benki ya NBC jijini Arusha wakifuatilia hafla hiyo







Mkurugenzi wa Wateja Wakubwa wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) Bw, Elvis Ndunguru (kulia) sambamba na maofisa wengie wa benki hiyo wakizungumza na wageni waalikwa ambao ni wateja wa benki hiyo jijini Arusha wakati wa hafla ya chakula cha jioni iliyoandaliwa na benki hiyo kwa ajili ya wateja wake wakubwa kutoka makampuni, wateja binafsi na taasisi mbali mbali (Corporates) ili kujadili fursa za biashara, kutambulisha huduma mpya sambamba na kuwaejengea uelewa zaidi wateja hao kuhusu faida na manufaa ya huduma hizo. Hafla hiyo iliyoandaliwa kupitia timu ya Biashara na Uwekezaji (CIB) ya benki hiyo ilifanyika jana jioni jijini Arusha.

Sunday, 20 July 2025

CPA AMOS MAKALA AWATAKA WATIA NIA KUWA WAPOLE TAREHE YASOGEZWA MBELE.

7/20/2025 10:41:00 am



Doreen Aloyce, Dodoma

WALIOTANGAZA nia ya kugombea nafasi ya ubunge na udiwani wametakiwa kuwa wapole kwani mchakato rasmi wa kuwateua wagombea watakao ingia kwenye kura za maoni  tarehe 28 mwezi wa saba tofauti na ilivyokuwa tarehe 19 mwezi huu.

Hayo yameelezwa na Katibu wa Chama cha Mapinduzi bh Makala alipokuwa akizungumza na waandishih wa habari juu ya kuhairiahwa tarehe iliyokuwa imepangwa.

Makala amesema kuwa kuhahiriahwa kwa ratiba ya awali inatokana na wagombea wa ubunge na udiwani kuwa wengi hivyo chama kinatakiwa kuhakikiaha kinafanya uchambuzi makini ili kuwapata wagombea makini kwa kutuenda haki kwa kila mtu.

Ameeleza kuwa kabla ya  wa wagombea ubunge na udiwani tarehe 28 mwezi wa saba kitafanyika kikao cha kamati kuu tarehe 26 mwezi wa saba na kufuatiwa na kikao cha halmashauri kuu ya taifa ya CCM ambacho nacho kitafanyika tarehe 26 mwezi wa saba mwaka huu.

Saturday, 12 July 2025

RC WA MANYARA SENDIGA AZINDUA ZOEZI LA USAMBAZAJI WA NISHATI SAFI YA KUPIKIA KWA BEI YA RUZUKU

7/12/2025 06:37:00 pm

Manyara

Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mheshimiwa Queen Sendiga, amezindua zoezi la ugawaji wa mitungi ya gesi kwa bei ya ruzuku, ikiwa ni sehemu ya kampeni ya kitaifa ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia na kupunguza utegemezi wa kuni na mkaa.


Uzinduzi huo umefanyika katika viwanja vya stendi ya zamani mjini Katesh, wilaya ya Hanang, ambapo jumla ya mitungi 3,000 iliyokamilika na vifaa vyake imetolewa kwa wananchi kwa bei nafuu ya ruzuku ya shilingi 17,500 (elfu kumi na saba na mia tano) kwa kila mtungi. Aidha, imeelezwa  kwa mkoa mzima wa Manyara jumla mitungi 16,275 itasambazwa na kuuzwa kwa bei ya ruzuku.


Akizungumza wakati wa uzinduzi, Mheshimiwa Sendiga amesema mpango huo umelenga kuhakikisha wananchi wote, hususani wa kipato cha chini, wanapata fursa ya kutumia nishati safi na salama ya kupikia kwa gharama nafuu.


Aidha, amewaagiza Wakuu wa Wilaya wote mkoani Manyara kusimamia kwa makini zoezi hili, ili kuhakikisha mitungi hiyo inauzwa kwa bei iliyokubaliwa na kuepuka udanganyifu wa baadhi ya Mawakala/wafanyabiashara wasio waaminifu.


“Natoa rai kwa wakuu wa wilaya wote kuhakikisha utaratibu unazingatiwa, na mitungi hii inawafikia walengwa kwa bei ya shilingi 17,500 kama ilivyopangwa. Hatutavumilia wafanyabiashara watakaojaribu kulangua na kuuza kwa bei ya juu ili kujipatia faida isiyo halali,” amesema Sendiga kwa msisitizo.


Mheshimiwa Sendiga ameeleza kuwa kampeni hii ni sehemu ya juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita inahoongozwa na Mhe.Dkt Samia Suluhu Hassan za kupunguza uharibifu wa mazingira unaosababishwa na ukataji miti kwa ajili ya kuni na mkaa, na pia kulinda afya ya wananchi dhidi ya moshi unaosababisha magonjwa ya njia ya hewa.


Mpango huu wa ruzuku unatarajiwa kupunguza mzigo wa gharama ya awali kwa wananchi ya kununua majiko ya gesi na hivyo kuwa chachu ya mabadiliko kuelekea upishi salama na rafiki kwa mazingira.

Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mheshimiwa Queen Sendiga, leo Julai 11. 2025 amezindua zoezi la ugawaji wa mitungi ya gesi kwa bei ya ruzuku, ikiwa ni sehemu ya kampeni ya kitaifa ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia na kupunguza utegemezi wa kuni na mkaa.


Uzinduzi huo umefanyika katika viwanja vya stendi ya zamani mjini Katesh, wilaya ya Hanang, ambapo jumla ya mitungi 3,000 iliyokamilika na vifaa vyake imetolewa kwa wananchi kwa bei nafuu ya ruzuku ya shilingi 17,500 (elfu kumi na saba na mia tano) kwa kila mtungi. Aidha, imeelezwa  kwa mkoa mzima wa Manyara jumla mitungi 16,275 itasambazwa na kuuzwa kwa bei ya ruzuku.





Akizungumza wakati wa uzinduzi, Mheshimiwa Sendiga amesema mpango huo umelenga kuhakikisha wananchi wote, hususani wa kipato cha chini, wanapata fursa ya kutumia nishati safi na salama ya kupikia kwa gharama nafuu.


Aidha, amewaagiza Wakuu wa Wilaya wote mkoani Manyara kusimamia kwa makini zoezi hili, ili kuhakikisha mitungi hiyo inauzwa kwa bei iliyokubaliwa na kuepuka udanganyifu wa baadhi ya Mawakala/wafanyabiashara wasio waaminifu.


“Natoa rai kwa wakuu wa wilaya wote kuhakikisha utaratibu unazingatiwa, na mitungi hii inawafikia walengwa kwa bei ya shilingi 17,500 kama ilivyopangwa. Hatutavumilia wafanyabiashara watakaojaribu kulangua na kuuza kwa bei ya juu ili kujipatia faida isiyo halali,” amesema Sendiga kwa msisitizo.


Mheshimiwa Sendiga ameeleza kuwa kampeni hii ni sehemu ya juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita inahoongozwa na Mhe.Dkt Samia Suluhu Hassan za kupunguza uharibifu wa mazingira unaosababishwa na ukataji miti kwa ajili ya kuni na mkaa, na pia kulinda afya ya wananchi dhidi ya moshi unaosababisha magonjwa ya njia ya hewa.


Mpango huu wa ruzuku unatarajiwa kupunguza mzigo wa gharama ya awali kwa wananchi ya kununua majiko ya gesi na hivyo kuwa chachu ya mabadiliko kuelekea upishi salama na rafiki kwa mazingira.

MAKAMU WA RAIS DKT. MPANGO AWATAKA WAGANGA WAKUU NCHINI KUONGEZA JUHUDI KANUNI ZA AFYA

7/12/2025 06:18:00 pm

DODOMA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango ametoa wito kwa Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri kuongeza juhudi katika kutoa hamasa kwa wananchi ili kuzingatia kanuni za afya bora na kuchukua hatua madhubuti za kujikinga na magonjwa ya kuambukiza na yale yasiyo ya kuambukiza.






Makamu wa Rais amesema hayo wakati akifungua Mkutano wa Mwaka wa Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri unaofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete mkoani Dodoma. Amesema ni vema elimu itakayotolewa izingatie ujenzi na matumizi ya vyoo bora, unawaji mikono kwa maji tiririka na sabuni nyakati zote muhimu ili kukabiliana na magonjwa ya kuambukiza, uondoshaji salama wa majitaka katika ngazi ya kaya na maeneo ya umma pamoja na kutibu maji ya kunywa kwa njia ya kuchemsha au kwa kuzingatia maelekezo ya wataalam.


 

Vilevile Makamu wa Rais ametoa rai kwa Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri kuvitunza vifaa tiba ikiwemo mashine za kisasa za uchunguzi na matibabu pamoja na magari ya kubeba wagonjwa yaliyonunuliwa na Serikali ili viweze kutumika kwa muda mrefu na kutoa huduma kwa watu wengi zaidi.

 

Pia amewasihi kuimarisha eneo la utunzaji wa kumbukumbu za matumizi ya dawa na vifaa tiba ili kuleta ufanisi katika utunzaji wa dawa na vifaa tiba na kuepuka upotevu. Amesema kutokuwepo na kumbukumbu sahihi za matumizi ya dawa na vifaa tiba hutatiza katika usambazaji wa dawa kutoka Bohari Kuu ya Dawa, na kutoa mwanya wa wizi na matumizi yasiyo sahihi.

 

Halikadhalika Makamu wa Rais amewaagiza Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri kulipa kipaumbele suala la utoaji wa elimu ya matumizi sahihi ya dawa ili kuisaidia jamii kutambua na kuepuka madhara ya matumizi holela ya dawa hususani dawa za maumivu na antibiotics ambazo zikitumiwa kiholela madhara yake ni makubwa. Pia amewataka kusimamia kwa ukaribu utekelezaji wa kiapo cha maadili katika kuwahakikishia wananchi huduma bora.

 

Aidha ameziagiza Mamlaka za Serikali za Mitaa kuhakikisha zinasimamia vema ukusanyaji wa mapato na kuhakikisha yanatumika kiadilifu ili kuboresha zaidi utoaji wa huduma wakati Serikali inapoelekea kutekeleza mpango wa Bima ya Afya kwa Wote.

 

Amesema katika kuhakikisha utoaji wa huduma bora za afya, Serikali imeweka kipaumbele suala la rasilimali watu yenye weledi, ambapo imeajiri jumla ya watumishi wapya 25,936 wa kada mbalimbali za afya katika ngazi ya msingi. Hatua hiyo imesaidia kukabili upungufu wa watumishi na kuongeza uwiano kati ya watoa huduma na wagonjwa. Ameongeza kwamba Serikali itaendelea kutoa kipaumbele katika eneo hilo hususani kwenye kada za kimkakati, ili kuhakikisha upatikanaji wa huduma bora na endelevu kwa wananchi.

 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema katika Mamlaka za Serikali za Mitaa, Serikali imefanikisha ujenzi wa jumla ya vituo kutolea huduma za afya 7414 ikiwemo vituo vilivyokuwepo na vilivyojengwa Awamu ya Sita. Amesema kwa miaka minne ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan jumla ya hospitali kongwe 48 zimekarabatiwa, ujenzi wa majengo ya huduma za dharura 87, majengo ya huduma za wagonjwa mahututi 30 pamoja na mifumo ya hewa tiba 21.

 

Ameongeza kwamba katika kipindi cha miaka minne jumla ya wakinamama zaidi ya laki tisa waliokuwa wakikabiliwa na changamoto za uzazi pingamizi waliweza kufanyiwa upasuaji salama katika vituo vya afya vilivyoboreshwa na vilivyojengwa upya.

 

Kwa upande wake Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama amesema Serikali imeendelea kutoa kipaumbele katika sekta ya Afya ikiwemo kuongeza bajeti kufikia trilioni 2.6 kwa mwaka wa fedha 2025/2026. Amesema kwa miaka minne ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan Bajeti ya Wizara ya Afya imefikia trilioni 7.15 hivyo kufanya mageuzi makubwa ya utoaji huduma za afya nchini. Amesema Wizara inatarajia kuanzisha chaneli maalumu ya Afya (Afya Tv) ili iweze kutangaza taarifa zinazohusu afya kwa wananchi.

 

Amesema juhudi mbalimbali katika kuboresha sekta ya afya zimesaidia kupambana na magonjwa ya mlipuko ikiwemo kumaliza ugonjwa wa Marbug ndani ya muda mfupi wa siku 54, kuimarisha diplomasia ya kimataifa katika sekta ya afya, kupungua kwa vifo vya mama na mtoto, kupungua kwa vifo vinavyotokana na dharura, kuongezeka kwa tiba utalii.

 

Ameongeza kwamba kwa sasa Tanzania inatarajia kuwa kuwa kituo cha umahiri wa matibabu ya upandikizaji ini, kituo cha umahiri matibabu ya mfumo wa mkojo, matibabu ya uzazi kwa wanaume, akili mnemba katika upasuaji, matibabu ya damu na upandikizaji uloto, matibabu ya figo, matumizi ya nyuklia katika matibabu ya saratani.

 

Awali akisoma risala, Mwenyekiti wa Waganga Wakuu wa Mikoa Dkt. Best Magoma ameipongeza serikali kwa maboresho makubwa yaliyofanyika katika sekta ya afya kuanzia ngazi ya afya ya msingi. Pia ameiomba Serikali kuhakikisha inapunguza uhaba wa nyumba za watumishi katika vituo vya kutolea huduma za afya ili kukabiliana na dharura zinazowapata wananchi hususani nyakati za usiku.

 

Mkutano huo wa siku tatu una kauli mbiu isemayo “Wajibu wa Waganga Wakuu wa Miko ana Halmashauri katika kuimarisha Ubora wa Huduma za Afya kuelekea Bima ya Afya kwa Wote”


Thursday, 10 July 2025

RAIS SAMIA KINARA , NISHATI SAFI YA KUPIKIA DUNIANI.

7/10/2025 08:08:00 pm

 Aungwa mkono- Eng. Sangweni

Apongeza kasi ya Dkt. Biteko na Uongozi Menejimenti ya Nishati katika kufanikisha Kampeni ya Nishati Safi ya Kupikia.


Asifu juhudi za TANESCO  na REA katika kutekeleza  Kampeni ya Nishati Safi ya Kupikia.


Atoa Rai kwa Watanzania kuhamia kwenye Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) Mha. Charles Sangweni ametoa Rai kwa Wananchi wote kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mhe. Dkt. Samia Suhuhu Hassan katika Kampeni ya Kitaifa  ya kuhamia kwenye Nishati Safi ya Kupikia.

Rai hiyo imetolewa leo tarehe 09 Julai, 2025  na Mha. Charles Sangweni alipotembelea Banda la TANESCO  katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar-es-Salaam yanayoendelea jijini Dar-es-Salaam.

Amesema Tanzania tuna bahati kuwa, Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jemedari Mkuu wa Majeshi ya nchi yetu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa ndiye Kinara wa Kampeni ya Nishati Safi ya Kupikia Duniani.



Amesema, Wizara ya Nishati na Watanzania wote kiujumla, ni muhimu tuunge mkono juhudi zinazofanywa na Rais wetu katika kuhakikisha Watanzania wanahamia katika Nishati Safi ya Kupikia kwanza kwa  kuhakikisha tunapokea na tunaendana na Kauli Mbiu ya Nishati Safi ya Kupikia na kuunga mkono jitihada alizozianzisha.

Amesema, "kama Watendaji, tumefurahi kuona, wenzetu wa TANESCO wameunga Mkono juhudi za Mheshimiwa Rais kwa kuja na kampeni ya kuhamasisha  matumizi ya vyombo mbadala vya umeme vinavyotumia umeme kidogo na ambavyo vinahakikisha Nishati inayotumika kwa ngazi ya kawaida kabisa majumbani inakuwa ni  Nishati Safi." Ameeleza kwa hisia za kuvutiwa na hatua hiyo Mha. Sangweni.

Mha. Sangweni ameeleza zaidi kuwa, katika kutembelea Banda la TANESCO, ameona vitu vingi, ikianzia kwa REA  Usambazaji wa Umeme unavyofanyika kwa kasi na hii inaonyesha kuunga mkono Juhudi za Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na Viongozi wengine wa Wizara akiwemo  Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Mashaka Biteko

Pia, Mha. Sangweni amesema vilevile katika Banda la TANESCO amekuta Wadau wanauza majiko ya umeme yanayotumia Nishati ya umeme kidogo sana ikilinganishwa na majiko mengine ya kawaida.


Mkurugenzi Mkuu huyo wa PURA ameeleza  kufurahishwa kwake zaidi na  majiko hayo yanayotumia mfumo wa sumaku kupitisha moto  kuwa na mfumo wa ku-sence  pale ambapo sufuria haiko jikoni na namna yanavyopunguza kabisa upotevu wa umeme ambao hautumiki.

"Tumeona kwamba, usipoweka sufuria basi hakuna moto ambao un


atoka na wakati mwingine ukiwa umejisahau, kunakuwa na timer ambayo inaweza ikazima jiko kulingana na jinsi ulivyo- set." Amesema Mha. Sangweni.

Amefafanua kuwa, hiyo yote ni katika kuhakikisha kwamba bili iliyokuwa inakuja kwa kiasi kikubwa ambayo ilikuwa inakuja kutokana na majiko ambayo hayana control kama hizo, inaenda kupungua kwa kiasi kikubwa sana.


"Hatua hiyo itatufanya sisi ambao vipato vyetu sio vikubwa kuona kuwa kutumia umeme sio anasa tena bali ni Matumizi Bora Kabisa ya Nishati ambayo iko safi na inayofaa kwa matumizi na ulinzi wa mazingira kama ambavyo Viongozi wetu wa nchi wamekuwa wakituhimiza na kusisitiza ili kama nchi tuingie kwenye Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia." Amesema Mha. Sangweni.



Sunday, 24 July 2016

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI ALIPOTEMBELEA CHUO CHA USAFIRISHAJI

7/24/2016 01:19:00 am


 Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) Prof. Zacharia Mganilwa akifafanua jambo kwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani alipotembelea Chuo hicho kukagua miundombinu yake.
 Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani akitoa maelekezo kwa  Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) Prof. Zacharia Mganilwa kuhusu namna nzuri ya kukiwezesha Chuo hicho kujiendesha kwa faida na kuboresha miundombinu yake.
 Mkuu wa Kitengo cha Uhandisi wa anga katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji NIT Eng. Azizi Mdimi akimuonesha Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani injini ya ndege inayotumia kwa mafunzo wakati alipokagua Hanga katika chuo hicho.
 Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani akikagua ndege inayotumiwa kufundishia wanafunzi wanaosomea utengenezaji wa ndege na urubani alipotembelea Chuo cha Usafirishaji NIT.
 Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) Prof. Zacharia Mganilwa akimuonesha  Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani moja ya kitabu kinachotumiwa kufundishia marubani na wahandisi wa ndege alipotembelea maktaba ya chuo hicho.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani akikagua mtambo unaopima magari ili kujua ubora wake kabla ya kuanza kutumika hapa nchini alipotembelea Chuo cha Taifa cha Usafirishaji NIT. (Picha na Benjamin Sawe-Maelezo)
Adbox