AFANDE SELE AWATAKA VIJANA KUACHA MIHEMKO NA KUTISHIA KUSUSIA UCHAGUZI MKUU OKTOBA MWAKA HUU
DOREEN BLOG
10/15/2025 08:22:00 pm
Mwanamuziki na mfalme wa mashairi Tanzania, Selemani Msindi maarufu kama Afande Sele,amewataka Watanzania hususan vijana kuacha kuwa na mihemko ya kususia kushiriki Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025.
Aidha Afande Sele amesisitiza kuwa kutoshiriki ni kujinyima haki ya kikatiba jambo ambalo sio sahihi katika kulijenga Taifa la baadae.
Akizungumza akiwa mkoani Morogoro, Afande Sele amesema vijana wanapaswa kutumia nguvu yao kwa kushiriki katika kupiga kura badala ya kujiingiza kwenye maandamano yanayoandaliwa na watu wasiolitakia mema taifa.

