Adbox

Friday, 29 August 2014

MMILIKI WA HOTEL YA SNOCREST ATAKIWA KULIPA ZAIDI YA BILIONI 3

8/29/2014 01:33:00 am

PICHA YA MUONEKANO WA HOTEL YA SNOW CREST

Mahakama kuu nchini kitengo cha biashara kanda ya Arusha imemuamuru mfanyabiashara ambaye pia ni mmiliki wa hoteli ya Snowcrest ya jijini Arusha,Wilfred Tarimo pamoja na familia yake kumlipa jumla ya $ 1.7 sawa na zaidi ya sh,3 bilioni mkurugenzi wa kampuni ya Grand Alliance Ltd,James Ndika kama malipo ya awamu ya kwanza ya kununua hisa ndani ya hoteli hiyo.


Mbali na agizo hilo mahakama hiyo pia imeagiza washtakiwa wanne kati ya watano katika kesi hiyo  walipe  kiasi cha riba cha asilimia 4 ya fedha hizo  tangu kufunguliwa kwa kesi hiyo na kiasi kingine cha asilimia 7 tangu kufungwa kwa shauri hilo hadi siku ya malipo.


Hukumu ya kesi hiyo ilisomwa mwishoni mwa wiki iliyopita na Jaji Robert Makaramba mbele ya mahakama hiyo mara baada ya kueleza kuridhika na ushahidi uliowailishwa na upande wa mlalamikaji kupitia kwa wakili wake Melkizedek Lutema.


Katika kesi hiyo iliyopewa usajili wa nambari 9 ya mwaka 2012 Ndika alieleza kutapeliwa jumla ya $ 1.7 milioni  sawa na sh,3 bilioni baada ya kupatiwa hati mbili za eneo la hoteli hiyo lakini baadaye ilikuja kubainika kwamba eneo la hoteli hiyo lina hati tatu.


Katika hati ya madai mlalamikaji anadai kuwa hati moja kati ya tatu ilikuwa na mkopo wenye riba wa kiasi cha sh,1.5 bilioni kupitia benki mojawapo hapa nchini na baada ya kugundulika hilo ilikwamisha biashara ya mauziano ya hoteli hiyo.


Kwa mujibu wa nakala ya hukumu iliyosainiwa na Jaji Makaramba washtakiwa watano katika kesi hiyo mshtakiwa wa kwanza ,Wilfred Tarimo,Derick Tarimo,Doreen Tarimo ambaye ni mke wa mshtakiwa wa kwanza Irene Tarimo pamoja na kampuni ya Snowcrest And Wildlife Safaris Ltd  wameamriwa kumlipa Ndika fedha hizo pamoja na kiasi cha riba hadi tarehe ya kukazia hukumu.


Mbali na agizo hilo washtakiwa wote katika kesi hiyo pia waliamriwa kulipa gharama za uendeshaji wa kesi hiyo  tangu ilipoanza kuunguruma huku wakipewa nafasi ya kukata rufaa ndani ya siku 30  tangu hukumu hiyo ilipotolewa.


Akihojiwa jijini Arusha wakili wa upande wa mlalamikaji,Lutema alisema kuwa wao wameridhika na hukumu hiyo na kwa sasa wanajiandaa kuwasilisha gharama za uendeshaji wa kesi hiyo tangu ilipoanza kuunguruma mnamo Januari 5 mwaka 2012.

Friday, 25 July 2014

WAZEE WA MILA WAKISHIKILIA MAJANI YA BARAKA

7/25/2014 09:26:00 pm
Meneja wa Shirika la Esirwa Richard Ndoros akiwaonyesha wananchi wake Barua ya usajili wa Shirika hilo kwa ajili ya kuanza kazi ya kuleta maendeleo katika kijiji cha Esirwa Wilayani Ngorongoro
Ni Baadhi ya akina mama jamii ya wamasai katika kijiji cha Esirwa wakitumbuiza nyimbo zao wakati wa sherehe za kumkaribisha kijana wao Richard Ndorosi kuanzisha  Shirika la Esirwa kijijini hapo kwa ajili ya kuleta maendeleo.

VIJANA WA KIMASAI WAKIIMBA NA KUCHEZA

7/25/2014 09:05:00 pm
Hawa ni Baadhi ya Vijana wa Kimaasai katika Kijiji cha Eswira Kata ya Gelai kilichpo ndani ya Hifadhi ya Ngorongoro wakiimba na kucheza wakati wa sherehe za kumkaribisha mmoja wa wanakijiji Richard Ndorosi kwa kuweza kuanzisha Shirika la Esirwa kwa ajili ya kunusuru kijiji hicho kutokana na changamoto za Kimaendeleo zinazowakabili kijijini hapo ambapo imepelekea wakazi jamii ya wamasai kuteseka kwa muda mrefu bila kupatiwa msaada.

Tuesday, 15 July 2014

KATIBU MKUU MAPUNDA AFANYA ZIARA MKOA WA ARUSHA

7/15/2014 10:34:00 am
six14Katibu mkuu wa UVCCM Taifa na mjumbe wa baraza la katiba Sixtus Mapunda akiendelea na ujenzi katika uwanja wa michezo wa st.Benjamin uliopo Usa river kwa ufadhili wa edinburgh global partnerships na YES Tanzania katika ziara yake ya kwanza ya kikazi ya siku tatu katika Mkoa wa Arusha
six16Aliyevalia sweta ni mkuu wa Wilaya ya Arumeru Nyirembe Munasa akisalimiana na viongozi wa chama Wilayani hapo ambapo mradi huo umetekelezwa kulia ni Katibu mkuu UVCCM Sixtus Mapunda akifurahia jambo
six17Katibu mkuu wa UVCCM Taifa na mjumbe wa baraza la katiba Sixtus Mapunda akipokelewa na viongozi na wa chama hicho mapema kabla ya kutembelea miradi
 six12Katibu mkuu wa UVCCM Taifa na mjumbe wa baraza la katiba Sixtus Mapunda akimkabidhi cheti mmoja wa wa vijana waliojitolea katika mradi wa ujenzi wa kiwanja cha michezo
six11Hapa viongozi na wadau wakishuhudia jiwe la msingi katika kiwanja hicho cha michezo kilichozinduliwa rasmi na Katibu mkuu wa UVCCM Taifa na mjumbe wa baraza la katiba Sixtus Mapunda
six10Katibu mkuu wa UVCCM Taifa na mjumbe wa baraza la katiba Sixtus Mapunda akimkabidhi cheti mshindi wa mbio za pikipiki greengad maarufu kwa jina la Mjusi.
six9Katibu mkuu wa UVCCM Taifa na mjumbe wa baraza la katiba Sixtus Mapunda akizindua shina la Ngarasero
six8Mwenyekiti UVCCM Mkoa wa Arusha Robson Meitinyiku akiongea katika mkutano wa hadhara katika kata ya Leguruki Mkoani Arusha ambapo aliwahimiza vijana wadumishe upendo,Amani katika Nchi yao huku akiwataka kuepuka uvinjifu wa Amani
six6 six5Katibu mkuu wa UVCCM Taifa na mjumbe wa baraza la katiba Sixtus Mapunda akimkabidhi cheti mmoja wa wadau waliodhamini maradi wa uwanja wa michezo kutoka kamapuni ya YES
sixx18Zaidi ya Wanachama wapya 27 kutoka chama cha demokrasia na maendeleo chadema waliochukua rasmi kadi za CCM wakionyasha kadi zao mara baada ya kukihama chama hicho
six20Umati wa wananchi waliojitokeza kumsikiliza Katibu mkuu wa UVCCM Taifa na mjumbe wa baraza la katiba Sixtus Mapunda
six21
six 19Katibu mkuu wa UVCCM Taifa na mjumbe wa baraza la katiba Sixtus Mapunda akimkabidhikadi mwanachama mpya kutoka chadema
six22six20
six4
six3Katibu mkuu wa UVCCM Taifa na mjumbe wa baraza la katiba Sixtus Mapunda akimkabidhicheti mkurugenzi wa YES Tanzania Samwel Mpenzu
six2
six1Katibu mkuu wa UVCCM Taifa na mjumbe wa baraza la katiba Sixtus Mapunda akiongea baada ya uzinduzi wa uwanja pamoja na mashina katika kata ya Ngarasero Mkoa Arusha katika ziara yake ya kwanza ya kikazi toka ateuliwe (Pamela Mollel jamiiblog)

Monday, 10 February 2014

BANANA INVESTMENT YATOA ZAWADI KWA MAWAKALA WAO.

2/10/2014 01:20:00 pm

Mshindi wa kwanza kitaifa ni Bw. Peter Assenga kutoka Morogoro aliyejishindia zawadi ya Gari,hapa akionyesha ufunguo wake katika sherehe zilizoandaliwa na kampuni ya Banana Investment iliopo jijini Arusha.  Mshindi wa pili ni Dorothea kutoka Rombo, Tarakea , na Mshindi wa tatu alipata friji ambae ni Bw. Ibrahim Kikweche kutoka Dar es Salaam. washindi wengine kutoka Arusha ni Bw. Zefania Kira kutoka Namanga aliyeshishindia Tv, Bw. Victor Massawe kutoka Mbuguni aliyejishindia Flat Screen Tv, Bw. Gabriel Shibu Kutoka Ulonga Shangarai

Mmoja wa wakala akipokea zawadi ya Flat Screen TV' 21'' katika sherehe zilizoandaliwa na kampuni ya Banana Investment iliopo Moshono, jijini Arusha.
Wakala akipokea zawadi yake katika sherehe za kuwakabidhi zawadi zilizoandaliwa na kampuni ya Banana Investment iliopo jijini Arusha. Kwa picha Zaidi Bofya hapa >>>

Wednesday, 29 January 2014

Monday, 13 January 2014

MCHUNGAJI AWAAMURU WAUMINI WAKE WALE MAJANI KAMA NG'OMBE AFRIKA KUSINI

1/13/2014 01:42:00 pm

God forgive for saying this, but how stupid can some people be? And how do you follow and obey another human being so blindly? A pastor in South Africa, Pastor Lesego Daniel is making his members eat grass. Yes, grass!

Pastor Daniel, who is the founder and Head Pastor at Rabboni Centre Ministries, situated at Zone 2 Ga-Rankuwa, north of Pretoria, said he was basically trying to prove that humans can be controlled by the spirit and they can eat anything to feed their bodies. I don't know how he managed to convince his members to go outside the church and start eating grass, but he! Unbelievable!


Huyu dada anakula majani kama mbuzi....
Kila mmoja anakula majani kwa style yake....ee Mungu Tusaidie..
Binadamu anatafuna majani...
  Mchungaji mwenyewe ndo huyo hapo juu anajiita 'Pastor Daniel Lesego'

  Hapa anawaombea akiwakanyaga kama magunia...Source: www.wazalendo25.blogspot.com

Sunday, 10 November 2013

WANANCHI WA KIJIJI CHA SAMARIA WAKISALIMIANA NA MBUNGE WAO NAKUTOA SHUKRANI

11/10/2013 04:30:00 pm
Wananchi wakijiji cha Samaria walayani Arumeru Mashariki wakisalimiana na Mh,mbunge wao Joshua nasari mara baada ya kumaliza kuchangisha Harambee kwa Ajili ya uchimbaji wa visima vya maiji.

Wananchi hao walisema wanamshuru sana Mbuge huyo kwa ujio wake pamoja na kuchangia ujenzi wa visima vya maji kwamba ni dhiki kubwa wamekumbana nayo katika kukosa maji.

Walisema kuwa na zaii ya miaka 100 hawajawahi kupata maji katika kijiji chao hivyo hutumia umbali wa masaa nane kwenda na kurudi jambo ambalo limekuwa ni kero kubwa sana katika maisha yao.

Mmoja wa wananchi wa kijiji hicho bi Ndeshukurwa Andrea Mbise akielezea kwa masikitiko makubwa sana alisema kuwa tatizo hilo la ukosefu wa maji limepelekea wengi wao kuishi bila kuoga ama kuoga mara moja kwa wiki kwani maji yamekuwa ni ya shida hivyo kutengewa kwa ajili ya mapishi tu ya nyumbani.

Pia alisema kwamba tatizo hilo limepelekea kufeli mitihani kwa watoto wao mashuleni kwani ile mida ya asubuhi hulazimika kwenda kuchota maji badala ya kwenda shuleni,na ule muda wanaotoka wanakuwa wamechokakitendo cha kuwafanya washindwe kusoma,ambapo huku wazazi wao wakiwa mashambani na sokoni kwa ajili ya kuwatafutia kitoweo.

Alimalizia kwa kusema kwamba wanamshuru sana Mh,Mbunge Nasari kwa kuja kijijini kwao kwa ajili ya Harambee ya kuchangia uchimbaji wa visima na kwamba kupitia hatua hiyo wataondokana na Hadha hiyo ambayo ni kero kubwa kwao.

Katika harambee hiyo ela iliyopatikana ni kiasi cha shilingi zaidi ya milion kumi na mbili 12.

Thursday, 24 October 2013

MENEJA WA KIMAHAMA AKIELEZEA UMUHIM WA KUSOMA VITABU.

10/24/2013 08:36:00 am
Bw,Emmanuel Absolum ambaye ni meneja wa duka la vitabu la Kimahama akieleza umuhimu wa wananchi kujisomea vitabu.

Amesema kuwa kupitia vitabu unapata elimu juu ya mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuongeza ujuzi kwa mambo ambayo mwananchi hayajui.

Akielezea lengo la kufungua duka hilo amesema kuwa ni kuwasaidia wakazi wa jiji la Arusha kupata elimu kupitia vitabu sambamba na kujijengea mazoea ya kusoma ujuzi na ufanisi katika kutambua mambo mbalimbali.

MENEJA WA KIMAHAMA AKIWA KWENYE DUKA LA VITABU

10/24/2013 08:21:00 am
Meneja wa kimahama Emmanuel Absalom akiwa amesimama kwenye duka la vitabu lililo zinduliwa upya na Mkuu wa chuo Habari maalum bw,Jackson Kaluzi, baada ya kuboreshwa na kuwekwa vitabu mbalimbali vya kuvutia ambapo vitabu hivyo ni kama Biblia,vitabu vya wanafunzi wa shule za msingi na sekondari na vingine vingi vya kuelimisha jamii.

Tuesday, 8 October 2013

AINA YA SAMAKI WA BAHARINI

10/08/2013 10:00:00 pm
Hawa ni samaki wekundu kwa jina maarufu(changu mwekundu) smaki hawa wanavutia sana kwa muonekano wao,samaki hawa  wanaopatikana katika bahari ya hindi,ambapo samaki hawa hawawezi kupatikana sehemu nyingine kama kwenye maziwa fofauti na kupatikana kwenye maji ya chumvi ya baharini.

Kama wanavyoonekana hapo juu hawa samaki hawjakaushwa wala kukaangwa hapa ni wametolewa baharini kuvuliwa katika sehemu ya uvuvi  bahari ya Hindi  Mkoani Tanga katika eneo lililopo mkabala kabisa na Radio ya Huruma fm iliyopo ufukweni mwa Bahari.

J

VIONGOZI WA TYCC WAKISOMA RISALA

10/08/2013 09:35:00 pm
Mwanafunzi ambaye ni Mmoja wa viongozi wa Tyccc kanda ya Tanga kwa jina la Douglos Gasper aliyevalia miwani(wa kwanza kutoka kushoto)ambaye pia ni mhazini wa kikundi hicho,akisoma risala mbele ya mgeni Rasmi kwenye mahafali yao ya dini ya kidato cha nne yaliyofanyika katika ukumbi wa Magreth Hall uliopo jijini Tanga.

Kiongozi huyo akisoma risala mbele ya mgeni rasmi pamoja na kadamnasi iliyokuwepo kwenye mahafali hayo ambapo alielezea changamoto wanazokumbana nazo katika kuendesha kikundi chao wakiwa shuleni.

Gasper alisema kuwa mara nyingi wamekuwa wakizuiliwa na uongozi wa shule katika suala zima la kuendesha vipindi vyao dini ikiwemo kuimba kwaya wawapo mashuleni  huku walimu hao wakitumia vipindi hivyo kufundisha masomo mengine jambo ambalo limepelekea wanafunzi wengi kutokuwa na hofu ya Mungu hata kutofahamu kabisa neno la Mungu.

Pia alisema kuwa changamoto nyingine inayowakabili katika utendaji kazi wao ni ufinyu wa kipato kwani hawana biashara yoyote hivyo kulazimika kutoa ela zao mifukoni pale kunapokuwa kumehitajika utatuzi wa jambo fulani na kwamba hali hiyo imepelekea shughuli zao kutokwenda kwa ufanisi.

Waliiomba serikali na uongozi wa dini ya kikristo kuwapa msaada pale watakapokuwa wanahitji msaada ikiwa ni pamoja na kuwawekea walimu wa dini kwenye shule zao ili kuweza kuepukana na tatizo lililokihtiri la kufeli masomo ya dini ya kikristo tofauti na dini nyingine.

Monday, 7 October 2013

Adbox