Adbox

Friday, 7 November 2025

WANANCHI WALIA NA UGUMU WA MAISHA ULIOSABABISHWA NA GHASIA ZA OKTOBA 29



Kutatizika kwa shughuli za kiuchumi kwa takribani siku tano mara baada ya uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 kumeelezwa kusababisha adha kubwa ya kiuchumi na kijamii kwa wananchi wa Mkoa wa Dar Es salaam hasa kwa wale ambao wamekuwa tegemeo kwa familia na wazazi wao.

Kauli hiyo imeelezwa na wananchi wa Mkoa huo wakati wakizungumza na waandishi wa habari, siku chache mara baada ya Tangazo la Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan la kutaka shughuli za Kijamii na kiuchumi kuendelea kama kawaida mara baada ya ghasia na vurugu za Jumatano ya Oktoba 29, 2025.

"Kutokana na vurugu na ghasia za Oktoba 29, sisi wananchi tunaotegemewa na familia na wazazi tumeathirika sana, siku tano kwenye maisha yetu ni nyingi sana na bahati mbaya hali hii ambayo mimi ni mara ya kwanza kuishuhudia haijaangalia kipato cha mtu kwasababu kukosekana kwa amani kulikotokea kumesababisha hata wenye kipato kukosa huduma na bidhaa muhimu." Amesema Bw. Habibu Sadick, Dereva wa Bajaji Jijini Dar Es Salaam.

Kwa upande wake Iddi Mzese, Mkazi wa Changarawe Jijini Dar Es Salaam kando ya kusisitiza namna ambavyo ghasia na vurugu hizo zilivyosababisha ugumu wa maisha, amewataka Vijana kujiepusha na mikumbo yenye kupelekea kujiingiza kwenye ghasia na uvunjifu wa amani, akihimiza ulinzi wa amani na mshikamano uliopo nchini.

No comments:

Adbox