Adbox

Friday, 14 November 2025

JUMUIYA YA KIKRISTO NCHINI YAUNGA MKONO AHADI YA RAIS SAMIA YA MARIDHIANO YA KITAIFA


Jumuiya ya Kikristo nchini Tanzania CCT, imesisitiza haja ya kufanyika kwa mazungumzo ya Kitaifa na yatakayojumuisha wadau mbalimbali ili kufanya tathimini ya matukio yaliyotokea wakati wa uchaguzi Mkuu wa Tanzania wa Oktoba 29,2025 na kuweka kwa pamoja mikakati ya umoja, amani, haki na maridhiano nchini.

Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo ya CCT Askofu Dkt. Stanley Hotay alipozungumza na waandishi wa habari Mjini Dar Es Salaam, akiungana na  msisitizo wa Rais Samia Suluhu Hassan ya kuanzisha mchakato wa maridhiano mara baada ya uchaguzi Mkuu.

"CCT inashauri kufanyika kwa mazungumzo ya Kitaifa yatakayojumuisha wadau mbalimbali kwa lengo la kufanyika kwa tathmini ya matukio yaliyotokea na kuweka mikakati ya kuimarisha amani, umoja na maridhiano kama alivyosema Mhe. Rais." Amesema Dkt. Hotay.

Kiongozi huyo wa dini amesema serikali pia inapaswa kutoa msaada ea kibinadamu kwa familia zilizoathirika ikiwa ni pamoja na kuwasaidia majeruhi na kuchukua hatua za kurejesha hali ya utulivu nchini, akisema kanisa hilo linaamini kuwa amani ya kweli hupatikana kwa haki.

No comments:

Adbox