Viongozi wa dini Mkoa wa Katavi wamefanya Kikao maalumu kujadili kuhusu amani na Mshikamano wa Watanzania, wakihamasisha wananchi kuendelea kutunza na kudumisha amani hasa katika kipindi hiki cha kuelekea kwenye uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025.
Viongozi hao Kwa pamoja wamesema kila Mtanzania anayo nafasi ya kuilinda tunu ya amani tukiyoachiwa na baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere na uchaguzi usiwe sehemu ya kuleta mgawanyiko na kuvuruga amani kwani kukosekana kwa amani kwenye Jamii kunachangia Kwa kiasi kikubwa kurudisha nyuma maendeleo ya Tanzania.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano na kamati ya amani ambaye pia ni Shekhe wa Mkoa waka Katavi Sheikh Mashaka Nassor Kakulukulu amesema katika kipindi hiki watanzania wanatakiwa kuungana na kuzika tofauti za udini ukabila na nyinginezo ili kuvuka salama katika kipindi cha uchaguzi na amani ndio nguzo ya maendeleo kwani hakuna maendeleo pasipo amani.


No comments:
Post a Comment