Wakati Tanzania ikielekea kwenye Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwanamke na Nguvu ya Kijani, Dkt. Judith Mhina Spendi, ametoa wito kwa Watanzania wote kusimama pamoja kulinda amani ya taifa. Akizungumza jijini Dar es Salaam, Dkt. Judith alitangaza kongamano la amani litakalofanyika kuanzia Oktoba 25 hadi 27 katika Viwanja vya Posta Kijitonyama, likiwakutanisha viongozi wa dini, vijana, wafanyabiashara na taasisi mbalimbali.
Dkt. Judith alisisitiza kuwa amani ndiyo msingi wa maendeleo, ikieleza kuwa Tanzania imepiga hatua kubwa kiuchumi kutokana na utulivu uliopo. “Hakuna maendeleo bila amani, hakuna uchaguzi huru bila utulivu, na hakuna taifa imara bila mshikamano,” alisema. Akihitimisha hotuba yake, alitoa wito kwa Watanzania wote kuwa sauti ya amani, umoja na ukweli.
“Mimi naahidi amani, wewe je?” — Dkt. Judith Mhina Spendi


No comments:
Post a Comment