Mkurugenzi wa Uchaguzi kutoka Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Ramadhan Kailima, amewatahadharisha wananchi na wadau wa siasa nchini kuwa kuhamasisha watu kutoshiriki kupiga kura ni kosa la kwa mujibu wa Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya mwaka 2024.
Akizungumza katika mahojiano maalum na kituo cha televisheni cha UTV, Kailima amesema kifungu cha 129 cha sheria hiyo kinaeleza wazi kuwa mtu yeyote anayetumia nguvu, vitisho, au udanganyifu kumshawishi mpiga kura kuacha kupiga kura anatenda kosa la ushawishi mbaya, na anaweza kuchukuliwa hatua za kisheria.
Amefafanua kuwa kifungu hicho kinakataza mtu yeyote kutumia au kutishia kutumia nguvu, vurugu, au hila ya aina yoyote kwa lengo la kumshawishi mpiga kura kupiga au kuacha kupiga kura, akisisitiza kuwa hatua za kisheria zitachukuliwa kwa watakaobainika kuvunja masharti hayo.


No comments:
Post a Comment