Adbox

Wednesday, 27 August 2025

BALOZI DKT, ASHA ROSE MIGIRO APOKELEWA RASMI MAKAO MAKUU CCM,AAHIDI USHINDI KUTEKELEZA ILANI YA CHAMA


Na Sebastian Mavyeo, Dodoma

 ‎Katibu mkuu wa chama cha mapinduzi CCM Dkt.Asha Rose Migiro ameishukuru kamati kuu ya CCM Taifa kwa kumteua kuwa mrithi wa Dkt.Emanuel Nchimbi katika nafasi hiyo huku akiahidi  kutekeleza ilani ya chama hicho.

Dkt.Migiro ameyasema hayo leo Agosti 26,2025 wakati alipopokelewa katika ofisi za makao makuu ya chama hicho jijini hapa Dodoma na aliyekuwa katibu mkuu CCM Taifa Dkt.Emanuel Nchimbi ambaye kwa sasa atakuwa mgombea mwenza wa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29.2025.‎‎

Amesema kuteuliwa kwake kumetokana na ushirikiano mkubwa aliyopewa na wanachama wa CCM kipindi alipokuwa  kiongozi wa chama hicho katika   nyadhifa mbalimbali.


‎‎"Nishukuru kamati ya Halmashauri kuu ya CCM kwa kukubali mimi niwe mrithi wa Dkt.Nchimbi,Dkt.Nchimbi ana uzoefu mkubwa ndani ya CCM ameingia akiwa mdogo hadi sasa, hivyo naamini uwezo wake ni mkubwa ndani ya chama.‎‎

"Wanachama wa CCM ndio mtaji na raslimali zetu,kwa upande wangu kuwa katibu mkuu wa CCM ni kutokana na nyie kunipa ushirikiano katika kazi mbalimbali nilizozifanya ndani ya chama hiki hivyo tutahakikisha wagombea wetu wote wanapata ushindi mnono katika uchaguzi mkuu,"amesema Dkt.Migiro.

‎‎Awali aliyekuwa katibu mkuu wa CCM Taifa Dkt.Emanuel Nchimbi amemshukuru mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kumteua kuwa katibu mkuu wa chama hicho kwa kipindi chote alichoongoza . 

huku akiwashukuru wanachama wa CCM kwa ushirikiano waliyompatia kipindi cha uongozi wake.‎‎"kwanza wana CCM  wa Dodoma ni wakarimu sana na watakuonesha ushirikiano,tunaipongeza halmashauri kuu ya CCM kwa kukuteua wewe ,tunavishukuru vikao vya CCM kwa kuona uzito wa nafasi hii na kumteua mtu anayesitahili pia nimshukuru mwenyekiti wa CCM  kwa nafasi aliyonipa kipindi chote pamoja na wana ccm kwa ushirikiano mlionionesha,"amesema Dkt.Nchimbi.‎

Mwish

No comments:

Adbox