Adbox

Tuesday, 14 October 2014

TOKOMEZA UJANGILI ,OKOA UTALII WETU WAFANYIKA JIJINI ARUSHA

10/14/2014 05:57:00 pm
 Mhe. Allan Kijazi akipokea mfano wa Tembo katika maadhimisho ya TOKOMEZA UJANGILI WA TEMBO ,OKOA UTALII WETU Uliofanyika kwa matembezi na kuhitimishwa katika viwanja vya Sheikh Amri Abeid , Jijini Arusha Leo.




 Waziri Nyalandu akijadili jambo na muandaaji katika maadhimisho ya TOKOMEZA UJANGILI WA TEMBO ,OKOA UTALII WETU Uliofanyika kwa matembezi na kuhitimishwa katika viwanja vya Sheikh Amri Abeid , Jijini Arusha Leo.
 Nakaaya Sumari katika maadhimisho ya TOKOMEZA UJANGILI WA TEMBO ,OKOA UTALII WETU Uliofanyika kwa matembezi na kuhitimishwa katika viwanja vya Sheikh Amri Abeid , Jijini Arusha Leo.
 Mrisho Mpoto Akijinyoosha .....
 Mrisho Mpoto katikati ya wadau wa TOKOMEZA UJANGILI , OKOA UTALII
 Peter Msechu
 Peter Msechu akitoa Burudani katika maadhimisho ya TOKOMEZA UJANGILI WA TEMBO ,OKOA UTALII WETU Uliofanyika kwa matembezi na kuhitimishwa katika viwanja vya Sheikh Amri Abeid , Jijini Arusha Leo.

 Mrisho Mpoto katika maadhimisho ya TOKOMEZA UJANGILI WA TEMBO ,OKOA UTALII WETU Uliofanyika kwa matembezi na kuhitimishwa katika viwanja vya Sheikh Amri Abeid , Jijini Arusha Leo.
 Peter Msechu katika maadhimisho ya TOKOMEZA UJANGILI WA TEMBO ,OKOA UTALII WETU Uliofanyika kwa matembezi na kuhitimishwa katika viwanja vya Sheikh Amri Abeid , Jijini Arusha Leo.
 Wadau wa Utalii wakipata picha na Peter Msechu katika maadhimisho ya TOKOMEZA UJANGILI WA TEMBO ,OKOA UTALII WETU Uliofanyika kwa matembezi na kuhitimishwa katika viwanja vya Sheikh Amri Abeid , Jijini Arusha Leo.
 Mdau wa utalii akipata picha na Mrisho Mpoto katika maadhimisho ya TOKOMEZA UJANGILI WA TEMBO ,OKOA UTALII WETU Uliofanyika kwa matembezi na kuhitimishwa katika viwanja vya Sheikh Amri Abeid , Jijini Arusha Leo.

 Walter Emmanuel wa Nothern Shots katika maadhimisho ya TOKOMEZA UJANGILI WA TEMBO ,OKOA UTALII WETU Uliofanyika kwa matembezi na kuhitimishwa katika viwanja vya Sheikh Amri Abeid , Jijini Arusha Leo.
Sirili Akko akiongea jambo katika maadhimisho ya TOKOMEZA UJANGILI WA TEMBO ,OKOA UTALII WETU Uliofanyika kwa matembezi na kuhitimishwa katika viwanja vya Sheikh Amri Abeid , Jijini Arusha Leo. Picha Zote Na Gadiola Emanuel na Walter Emanuel wa Northern Shots 

Wednesday, 10 September 2014

KIVUKO CHA MV. KIGAMBONI KUANZA KAZI KESHO KUTWA

9/10/2014 04:04:00 pm


Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Watendaji mbalimbali hawapo pichani kutoka, Wizara ya Ujenzi, TEMESA na Kikosi cha Maji cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) ambao wamefanya kazi kubwa ya ukarabati wa Kivuko cha MV Kigamboni.
Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akipanda ngazi kwenda kukagua Kivuko cha MV Kigamboni ambacho matengenezo yake makubwa yanakamilika leo.
Luteni Kanali Gwanafi kulia akimuongoza Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwenda kukagua Kivuko cha MV Kigamboni sehemu ya chini mara baada ya kukamilika kwa ukarabati wake.
Luteni Kanali Gwanafi wapili kutoka kulia akitoa maelezo kuhusu ukarabati mkubwa wa Kivuko cha MV Kigamboni kama inavyoonekana.
Taswira-Kivuko cha MV Kigamboni kinavyoonekana mara baada ya Ukarabati wake.
Luteni Kanali Gwanafi kulia akimuonesha Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli sehemu ya juu ya Kivuko cha MV Kigamboni.
Luteni Kanali Gwanafi kushoto akimuonyesha Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Mhandisi Mussa Iyombe kuhusu sehemu ya chini ilivyokarabatiwa.
Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa ndani ya kivuko cha MV Kigamboni huku akipatiwa maelezo kuhusu ukarabati wake.
Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimsikiliza kwa makini Luteni Kanali Gwanafi kuhusu mambo mbalimbali wanayofanya ndani ya kivuko cha MV Kigamboni.
Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akitoka ndani ya Kivuko cha MV Kigamboni mara baada ya ukaguzi wake. Picha zote kwa Hisani ya Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Wizara ya Ujenzi.


Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli amesema kuwa Kivuko cha MV Kigamboni kinatarajiwa kuanza safari zake za usafirishaji rasmi kesho kutwa mara baada ya ukarabati wake kukamilika.

Waziri wa Magufuli alitoa kauli hio leo wakati akikagua kivuko hicho ambacho kilikuwa kikikarabatiwa na Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) kupitia kikosi cha Wanamaji.

Mheshimiwa Magufuli aliongeza kuwa hicho ambacho kinategemewa na wananchi wengi waishio Kigamboni na maeneo jirani kinategemewa kuteremshwa majini kesho jioni mara baada ya maji kujaa na kesho kutwa kuanza rasmi shughuli zake za usafirishaji.

“Nimekagua na kujionea kazi inavyoendelea na nimeridhishwa na mlipofikia mpaka sasa, naamini kazi imefanyika ipasavyo, hivyo basi palipobaki ni matengenezo madogo, kutokana na utendaji wenu wa kazi naamini kesho Kivuko hicho kitateremshwa majini na kesho kutwa kuanza safari”, Alisema Waziri Magufuli.

Aidha, Mheshimiwa Magufuli alikipongeza kikosi hicho cha Navy kwa kufanya kazi usiku na mchana kuhakikisha kuwa wanamaliza ukarabati huo kwa wakati licha ya changamoto nyingi walizokumbana nazo.

Sambamba na hilo, Waziri Magufuli amesema kuwa ndani ya Wiki tatu au nne Boti ya Kutoka Dar hadi Bagamoyo itawasili kwani imeshateremshwa majini huko inapotengenezwa na kilichobaki ni kuifikisha Dar es Salaam

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Mhandisi Mussa Iyombe, amepongeza Jeshi la Wananchi Tanzania kupitia Kikosi cha majini kwa uzalendo wao waliouonesha kwa kukamilisha ujenzi huo kwa gharama nafuu na kwa wakati ili kurejesha huduma za usafirishaji.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA), Mhandisi Marceline Magessa amesema kuwa ukarabati wa MV Kigamboni ulikuwa katika hatua za marekebisho mbalimbali ikiwemo utoaji kutu, kupaka rangi, usafi na uzibaji wa matundu pembezoni mwa kivuko hicho.

Naye kamanda wa kikosi cha majini Brigedia Jenerali Rogastian Laswai amezitaja changamoto zilizowakabili wakati wa utengenezaji wa kivuko hicho kuwa ni pamoja na kushindwa kupaka rangi kutokana na uwepo wa mvua pamoja na kupwa na kujaa kwa maji

Ukarabati wa Kivuko cha MV Agosti 14 mwaka huu mpaka kukamilika kwake hivi leo.

Friday, 29 August 2014

MMILIKI WA HOTEL YA SNOCREST ATAKIWA KULIPA ZAIDI YA BILIONI 3

8/29/2014 01:33:00 am

PICHA YA MUONEKANO WA HOTEL YA SNOW CREST

Mahakama kuu nchini kitengo cha biashara kanda ya Arusha imemuamuru mfanyabiashara ambaye pia ni mmiliki wa hoteli ya Snowcrest ya jijini Arusha,Wilfred Tarimo pamoja na familia yake kumlipa jumla ya $ 1.7 sawa na zaidi ya sh,3 bilioni mkurugenzi wa kampuni ya Grand Alliance Ltd,James Ndika kama malipo ya awamu ya kwanza ya kununua hisa ndani ya hoteli hiyo.


Mbali na agizo hilo mahakama hiyo pia imeagiza washtakiwa wanne kati ya watano katika kesi hiyo  walipe  kiasi cha riba cha asilimia 4 ya fedha hizo  tangu kufunguliwa kwa kesi hiyo na kiasi kingine cha asilimia 7 tangu kufungwa kwa shauri hilo hadi siku ya malipo.


Hukumu ya kesi hiyo ilisomwa mwishoni mwa wiki iliyopita na Jaji Robert Makaramba mbele ya mahakama hiyo mara baada ya kueleza kuridhika na ushahidi uliowailishwa na upande wa mlalamikaji kupitia kwa wakili wake Melkizedek Lutema.


Katika kesi hiyo iliyopewa usajili wa nambari 9 ya mwaka 2012 Ndika alieleza kutapeliwa jumla ya $ 1.7 milioni  sawa na sh,3 bilioni baada ya kupatiwa hati mbili za eneo la hoteli hiyo lakini baadaye ilikuja kubainika kwamba eneo la hoteli hiyo lina hati tatu.


Katika hati ya madai mlalamikaji anadai kuwa hati moja kati ya tatu ilikuwa na mkopo wenye riba wa kiasi cha sh,1.5 bilioni kupitia benki mojawapo hapa nchini na baada ya kugundulika hilo ilikwamisha biashara ya mauziano ya hoteli hiyo.


Kwa mujibu wa nakala ya hukumu iliyosainiwa na Jaji Makaramba washtakiwa watano katika kesi hiyo mshtakiwa wa kwanza ,Wilfred Tarimo,Derick Tarimo,Doreen Tarimo ambaye ni mke wa mshtakiwa wa kwanza Irene Tarimo pamoja na kampuni ya Snowcrest And Wildlife Safaris Ltd  wameamriwa kumlipa Ndika fedha hizo pamoja na kiasi cha riba hadi tarehe ya kukazia hukumu.


Mbali na agizo hilo washtakiwa wote katika kesi hiyo pia waliamriwa kulipa gharama za uendeshaji wa kesi hiyo  tangu ilipoanza kuunguruma huku wakipewa nafasi ya kukata rufaa ndani ya siku 30  tangu hukumu hiyo ilipotolewa.


Akihojiwa jijini Arusha wakili wa upande wa mlalamikaji,Lutema alisema kuwa wao wameridhika na hukumu hiyo na kwa sasa wanajiandaa kuwasilisha gharama za uendeshaji wa kesi hiyo tangu ilipoanza kuunguruma mnamo Januari 5 mwaka 2012.

Friday, 25 July 2014

WAZEE WA MILA WAKISHIKILIA MAJANI YA BARAKA

7/25/2014 09:26:00 pm
Meneja wa Shirika la Esirwa Richard Ndoros akiwaonyesha wananchi wake Barua ya usajili wa Shirika hilo kwa ajili ya kuanza kazi ya kuleta maendeleo katika kijiji cha Esirwa Wilayani Ngorongoro
Ni Baadhi ya akina mama jamii ya wamasai katika kijiji cha Esirwa wakitumbuiza nyimbo zao wakati wa sherehe za kumkaribisha kijana wao Richard Ndorosi kuanzisha  Shirika la Esirwa kijijini hapo kwa ajili ya kuleta maendeleo.

VIJANA WA KIMASAI WAKIIMBA NA KUCHEZA

7/25/2014 09:05:00 pm
Hawa ni Baadhi ya Vijana wa Kimaasai katika Kijiji cha Eswira Kata ya Gelai kilichpo ndani ya Hifadhi ya Ngorongoro wakiimba na kucheza wakati wa sherehe za kumkaribisha mmoja wa wanakijiji Richard Ndorosi kwa kuweza kuanzisha Shirika la Esirwa kwa ajili ya kunusuru kijiji hicho kutokana na changamoto za Kimaendeleo zinazowakabili kijijini hapo ambapo imepelekea wakazi jamii ya wamasai kuteseka kwa muda mrefu bila kupatiwa msaada.

Tuesday, 15 July 2014

KATIBU MKUU MAPUNDA AFANYA ZIARA MKOA WA ARUSHA

7/15/2014 10:34:00 am
six14Katibu mkuu wa UVCCM Taifa na mjumbe wa baraza la katiba Sixtus Mapunda akiendelea na ujenzi katika uwanja wa michezo wa st.Benjamin uliopo Usa river kwa ufadhili wa edinburgh global partnerships na YES Tanzania katika ziara yake ya kwanza ya kikazi ya siku tatu katika Mkoa wa Arusha
six16Aliyevalia sweta ni mkuu wa Wilaya ya Arumeru Nyirembe Munasa akisalimiana na viongozi wa chama Wilayani hapo ambapo mradi huo umetekelezwa kulia ni Katibu mkuu UVCCM Sixtus Mapunda akifurahia jambo
six17Katibu mkuu wa UVCCM Taifa na mjumbe wa baraza la katiba Sixtus Mapunda akipokelewa na viongozi na wa chama hicho mapema kabla ya kutembelea miradi
 six12Katibu mkuu wa UVCCM Taifa na mjumbe wa baraza la katiba Sixtus Mapunda akimkabidhi cheti mmoja wa wa vijana waliojitolea katika mradi wa ujenzi wa kiwanja cha michezo
six11Hapa viongozi na wadau wakishuhudia jiwe la msingi katika kiwanja hicho cha michezo kilichozinduliwa rasmi na Katibu mkuu wa UVCCM Taifa na mjumbe wa baraza la katiba Sixtus Mapunda
six10Katibu mkuu wa UVCCM Taifa na mjumbe wa baraza la katiba Sixtus Mapunda akimkabidhi cheti mshindi wa mbio za pikipiki greengad maarufu kwa jina la Mjusi.
six9Katibu mkuu wa UVCCM Taifa na mjumbe wa baraza la katiba Sixtus Mapunda akizindua shina la Ngarasero
six8Mwenyekiti UVCCM Mkoa wa Arusha Robson Meitinyiku akiongea katika mkutano wa hadhara katika kata ya Leguruki Mkoani Arusha ambapo aliwahimiza vijana wadumishe upendo,Amani katika Nchi yao huku akiwataka kuepuka uvinjifu wa Amani
six6 six5Katibu mkuu wa UVCCM Taifa na mjumbe wa baraza la katiba Sixtus Mapunda akimkabidhi cheti mmoja wa wadau waliodhamini maradi wa uwanja wa michezo kutoka kamapuni ya YES
sixx18Zaidi ya Wanachama wapya 27 kutoka chama cha demokrasia na maendeleo chadema waliochukua rasmi kadi za CCM wakionyasha kadi zao mara baada ya kukihama chama hicho
six20Umati wa wananchi waliojitokeza kumsikiliza Katibu mkuu wa UVCCM Taifa na mjumbe wa baraza la katiba Sixtus Mapunda
six21
six 19Katibu mkuu wa UVCCM Taifa na mjumbe wa baraza la katiba Sixtus Mapunda akimkabidhikadi mwanachama mpya kutoka chadema
six22six20
six4
six3Katibu mkuu wa UVCCM Taifa na mjumbe wa baraza la katiba Sixtus Mapunda akimkabidhicheti mkurugenzi wa YES Tanzania Samwel Mpenzu
six2
six1Katibu mkuu wa UVCCM Taifa na mjumbe wa baraza la katiba Sixtus Mapunda akiongea baada ya uzinduzi wa uwanja pamoja na mashina katika kata ya Ngarasero Mkoa Arusha katika ziara yake ya kwanza ya kikazi toka ateuliwe (Pamela Mollel jamiiblog)
Adbox