TABORA WAUPOKEA MWAKA MPYA KWA AMANI NA UTULIVU MKUBWA
Wananchi wa maeneo mbalimbali Mkoani Tabora wameshiriki kwa namna mbalimbali kusherehekea sikukuu ya Mwaka mpya 2026 na kuuaga mwaka 2025, Burudani za muziki katika sehemu mbalimbali za starehe zikionekana kujaa zaidi, amani na utulivu ukitawala pia katika maeneo hayo.
Wengine pia kama ilivyo utamaduni wa wananchi wa Tabora, wameonekana jana usiku Januari Mosi, 2026 wakiwa kwenye mitaa mbalimbali wakiimba na kusherehekea kuumaliza mwaka 2025 na kuuanza mwaka mpya 2026.
Polisi pia wameonekana katika maeneo yote yenye mikusanyiko mikubwa ya watu ili kuhakikisha hali ya ulinzi na usalama inakuwepo ili kutoa fursa ya kila mmoja kufurahi na wengine kuendelea na biashara zao bila ya vitisho vyovyote vya uvunjifu wa amani kwenye jamii.
Jana Disemba 31, 2025 wakati wa hotuba yake ya kuukaribisha mwaka Mpya, Rais Samia Suluhu Hassan wa Tanzania, aliwatakia kheri na mafanikio tele watanzania wote, akiahidi kwamba serikali yake itaendelea kuwatumikia watanzania wote kikamilifu ikiwa ni pamoja na kujenga umoja wa Kitaifa nchini, akitoa rai ya kutokubali kugawanyika kiitikadi na kimtazamo wanapoendelea na ujenzi wa Taifa lao.
Tanzania kama ilivyo kwenye Mataifa mengine kote duniani inasherehekea mwaka mpya wa 2026, Mamilioni wakishuhudia fataki, sherehe za kitamaduni na kidini na mikusanyiko ya kifamilia na kindugu, kuashirikia mwanzo wa mwaka mpya wa 2026 wakiwa na wingi wa matumaini ya ustawi na maendeleo yao binafsi.
Mkoani Dar Es Salaam, leo mchana katika maeneo mbalimbali kumeendelea kushuhudiwa mikusanyiko ya watu, ikiwemo eneo maarufu la Coco Beach, Wilayani Kinondoni ambapo watu wazima kwa watoto wameshuhudiwa wakibarizi katika fukwe hizo usalama ukiimarishwa na Polisi waliokuwa doria, kuhakikisha kila mmoja anaifurahia siku hii.
"Tunafurahi kuingia mwaka mpya, mwaka jana umekuwa na mchanganyiko wa mambo lakini tunamshukuru Mungu kwa hatua za maendeleo tulizopiga na zaidi kwa kuendelea kuitunza amani yetu. Niwaombe watanzania tusirudi tena kule kwenye vurugu, tuione thamani ya amani, tuilinde na tuwakatae wote wanaotaka kuipoteza." Amesema Bi. Amina Seleman, mmoja wa wananchi waliozungumza nasi Coco Beach.
Tofauti na wachache kwenye Mitandao ya kijamii walivyokuwa wakihamasisha kufanyika kwa maandamano hii leo, amani imeendelea kushuhudiwa, Watanzania wakipuuza miito hiyo ya maandamano na kuendelea na sherehe za mwaka mpya 2026.
-
[image: SPORT AND THE SUSTAINABLE DEVELOPMENT]
*The United Nations* have long recognized, advocated for and supported the
important contributions of spor...
Munere veritus fierent cu sed, congue altera mea te, ex clita eripuit evertitur duo. Legendos tractatos honestatis ad mel. Legendos tractatos honestatis ad mel.
, click here →