Na Doreen Aloyce, Dodoma
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Samia Suluhu Hassan ameshiriki maadhimisho ya siku ya kumbukumbu ya mashujaa waliopigania Uhuru wa Tanzania yaliyofanyika Mji wa Serikali Wilayani Chamwino Mkoani Dodoma.
Dk.Samia ameongoza maadhimisho hayo kwakuweka Mkuki na ngao huku Jenerali Jacob Mkunda akiweka Sime na shada la maua ambapo kiongozi wa Mabalozi ameweka Shada la maua kama ishara yakuwakumbuka mashujaa hao.
Akizungumza kwaniaba ya mashujaa hao,Mwakilishi wa mashujaa waliopigana vita vya kagera Balozi Brigedia Jenerali Francis Benard Mndolwa amesema anajivunia kuwa mmoja wa wapigania uhuru na kuwa mzalendo Kwa nchi yake na amewasihi wafanyakazi wote kuwa wazalendo.
Nao baadhi ya wananchi wameelezea kuhusiana na siku hiyo ya mashujaa.
Ikumbukwe kuwa siku ya Mashujaa huadhimishwa kila Mwaka mnamo Julai 25 kwa kuwakumbuka Mashujaa wote ambao walitoa maisha yao kwaajili ya kupigania uhuru kwa kulinda amani na heshima ya nchi.
MWISHO






No comments:
Post a Comment