DOREEN BLOG

HABARI, MICHEZO NA BURUDANI

Adbox

Friday, 30 January 2026

WAZIRI MAKONDA AWAPOKEA UMIKIDO KWA MIKONO MIWILI AHAIDI KUWAPA USHIRIKIANO

1/30/2026 01:14:00 pm
Na Mwandishi wetu,Dodoma

Katika kuendelea kuimarisha umoja na kujitambulisha kwa Mamlaka mbalimbali, Mwenyekiti wa Umoja wa Vyombo vya Habari Mitandaoni Mkoa wa Dodoma (UMIKIDO), Benny Majata, amefanya mazungumzo mafupi na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Paul Makonda, katika Viwanja vya Bunge jijini Dodoma leo Januari 29, 2026

Katika mazungumzo hayo, sambamba na kujitambulisha kwa Waziri Makonda, Majata amemweleza kuhusu malengo ya kuanzishwa kwa UMIKIDO, ikiwemo kusimamia maudhui yenye weledi, kuhamasisha maadili ya habari mtandaoni, pamoja na kuimarisha ushirikiano kati ya vyombo vya habari na Serikali.

Kwa upande wake, Waziri Makonda amesema milango ya Wizara ipo wazi kwa UMIKIDO kufika ofisini kwa ajili ya kufanya mazungumzo ya kina juu ya namna Wizara itakavyoweza kusaidia umoja huo kutimiza malengo yake.

WABUNGE MASHABIKI WA SIMBA NA YANGA KUTOANA JASHO JAN.31,2026 DODOMA

1/30/2026 12:49:00 pm
Na Doreen Aloyce,Dodoma


WAZIRI Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Bunge Azania Bonanza linalotarajiwa kuwakutanisha mashabiki wa Simba na Yanga Jumamosi Januari 31, 2026 Jijini Dodoma mbapo Bank ya Azania ndio Mdhamini mkuu katika Bonanza hilo.

Akizungumza na vyombo vya hanari Bungeni Dodoma Mwenyekiti wa Bunge Bonanza Mhe. Festo Sanga,wakati akizungumzia maandalizi ya bonanza hilo  ambapo amesema Bonanza hilo ni maono ya Bunge, menejimenti na Spika kuhakikisha linakuwa kiungo cha kuimarisha mahusiano na wadau mbalimbali.

Amesema Bank ya Azania imekuwa ikionesha ushirikiano mkubwa Kwa Serikali Kwa miaka miaka mitatu mfululizo ambapo pia amepokea vifaa vya michezo huku akiipongeza Bank hiyo Kwa ushirikiano mkubwa wanaoonyesha.

Mhe.Sanga amesema mashabiki wa Simba na Yanga wanatarajiwa kupimana nguvu katika bonanza hilo litakalowakutanisha wabunge, wafanyakazi wa Bunge, wizara pamoja na taasisi mbalimbali.


“Bonanza hili ni maono ya Bunge, menejimenti na Spika kuhakikisha linakuwa kiungo cha kuimarisha mahusiano na wadau mbalimbali, kwa kuwa Bunge ni chombo cha wananchi,” amesema Sanga.

Mhe.Sanga amesema bonanza hilo pia linalenga kudumisha umoja na mshikamano kati ya Bunge na taasisi mbalimbali, sambamba na kuunga mkono sekta ya michezo.

"Kwa niaba ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mussa Azzan Zungu tunaishukuru sana Azania Bank Kwa kuendelea Kutoa ushirikiano wao katika sekta ya Michezo". Amesema.

Amesema washiriki wote, wakiwemo wabunge na watumishi wa Bunge, wataanza matembezi ya pamoja kuanzia saa 12:00 asubuhi jirani na Chuo cha Mipango Dodoma kabla ya kuanza kwa michezo rasmi katika viwanja vya John Melini.

Hata hivyo amesema Bonanza hilo wanatarajiwa kujitolea kuchangia damu salama kwa hiari katika tukio hilo litakalofanyika Jumamosi, Januari 31, 2026, kwenye viwanja vya Shule ya Sekondari John Merlin Miyuji jijini Dodoma.

Thursday, 29 January 2026

POLISI NJOMBE WAKANUSHA TAARIFA ZA ASKARI KUCHOMWA MOTO NA KUPORWA SILAHA

1/29/2026 09:29:00 am

Jeshi la Polisi Mkoa wa Njombe katika taarifa yake kwa Vyombo vya habari limekanusha taarifa zilizokuwa zimesambazwa katika Mitandao ya Kijamii nchini zikiambatana na picha mjongeo (Video), zikieleza uwepo wa Askari Polisi wa Mkoa huo aliyechomwa moto na kisha kuporwa silaha Mkoani humo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Mahamoud Banga, Januari 28, 2026 amesema kuwa katika Mkoa wa Njombe hakuna tukio kama hilo, akionya dhidi ya wanaoandaa na kusambaza taarifa za uongo na upotoshaji.

"Jeshi la Polisi linatoa wito kwa baadhi ya wananchi wenye tabia za kuandaa na kusambaza taarifa za uongo na upotoshaji kwa njia mbalimbali kuacha kwani ni kinyume cha sheria za nchi na maadili ya Mtanzania na hakuna faida yoyote kwa wanaofanya hivyo pamoja na familia zao na kwa jamii kwa ujumla." Amesema Kamanda Banga.

Polisi pia imesema inaendelea kumfuatilia mtu ama watu waliochukua na kutumia picha mjongeo ya tukio la zamani ambalo askari walikwenda kutoa msaada kwa wananchi na kutengenezea taarifa hiyo ya uongo na kisha kuisambaza katika mitandao ya kijami

Aidha Kamanda Banga amesema Polisi wanaendelea kutekeleza majukumu yao kwa kushirikiana na wananchi kupitia programu za Polisi Jamii ili kubaini na kuzuia uhalifu sambamba na kufanya doria, misako na operesheni katika maeneo mbalimbali ili kuhakikisha maisha na mali za wananchi zinakuwa salama wakati wote.

MWANACHAMA WA CHADEMA ARUSHA MATATANI KWA KUIBA 'FEDHA ZA LISSU'

1/29/2026 08:49:00 am

Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha limetangaza kumkamata Bw. Fredrick Mbwambo, Mwanachama wa Chadema na Mkazi wa Arusha kwa tuhuma za wizi wa fedha ambazo alikuwa amezikusanya kutoka kwa wananchi waliokuwa wamechanga kwaajili ya Mwenyekiti wa Chama hicho Bw. Tundu Lissu kupitia Kampeni yao ya "Funga mwaka na Tundu Lissu".

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, SACP Justine Masejo leo Jumatano Januari 28, 2026 Jijini Arusha mbele ya wanahabari, amesema ukamataji wa mtuhumiwa huyo umefanyika baada ya Polisi kupokea malalamiko kutoka kwa Bw. Alute Mughwai, aliyeeleza kubaini wizi wa fedha zilizokuwa zimechangwa.

"Ufuatiliaji wa awali umeonesha kuwa ukusanyaji huo wa fedha ulikuwa ukifanywa kupitia namba mbili za simu za makampuni tofauti ya simu na inadaiwa zilihamishwa kwenye namba mbili za simu, moja ikiwa ni ya kampuni ya Tanzania na ya pili ikiwa ni ya kampuni ya simu ya nchi jirani." Amesema Kamanda Masejo.

Aidha Polisi ya Arusha imesema kutokana na malalamiko hayo jalada lilifunguliwa kwa mujibu wa taratibu na uchunguzi kuanza sambamba na ukamataji huo na jitihada za kuwatafuta watuhumiwa wengine waliotuhumiwa kuhusika katika wizi huo pamoja na vielelezo unaendelea ili hatua nyingine za kisheria ziweze kufuata.

Wednesday, 28 January 2026

UMIKIDO WAZIDI KUPAA ,WAJITAMBULISHA KWA WAZIRI KATAMBI

1/28/2026 07:43:00 pm

Mwenyekiti wa Umoja wa Vyombo vya Habari vya Mitandao ya Kijamii Mkoa wa Dodoma (UMIKIDO), Benny Majata, amefanya mazungumzo mafupi na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Patrobas Katambi, katika viwanja vya Bunge jijini Dodoma.

Katika mazungumzo hayo, leo Januari 28, 2026 Majata alimweleza Waziri Katambi juu ya malengo ya UMIKIDO katika kusimamia maudhui yenye weledi, kuhamasisha maadili ya habari mtandaoni na kuimarisha ushirikiano kati ya vyombo vya habari na serikali.

Waziri Katambi amepongeza hatua ya umoja huo kujitambulisha, na ameuhimiza UMIKIDO kufika ofisini kwake ili kufanya mazungumzo ya kina kuhusu masuala ya kimaadili, matumizi salama ya mitandao, pamoja na namna vyombo vya habari mtandaoni vinavyoweza kushirikiana na serikali katika kulinda usalama na maslahi ya Taifa.

RAIS SAMIA ANAAHIDI NA KUTEKELEZA "NI MFANO SAHIHI KWETU WASICHANA"

1/28/2026 07:10:00 pm

Rais Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametajwa na Wanawake na Mabinti wa Kitanzania kama Kiongozi wa mfano na mwanamke mwenye athari chanya kiasi cha kutoweza kupimika kwa wanawake na mabinti wa Tanzania, Wakimsifu na kumpongeza kwa ujasiri na umahiri wake mkubwa katika kuwaletea maendeleo Watanzania.

Kauli hiyo imebainishwa na Bi. Asina Sancho, Kijana na Mjasiriamali wa Kitanzania, akisema Rais Samia amewapa sababu mabinti wengi ya kuamini kuwa wanaweza kufikia malengo yao na kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika kupambania ndoto zao.

"Mama Samia ametutia nguvu sisi mabinti kuamini kuwa tunaweza kusimama na kutimiza ndoto zetu, hata katika nyakati za majaribio, Mama Samia ametupa nguvu ya kuamini hakuna linaloshindikana. Katika imani pia Mhe. Rais amesemwa katika namna nyingi mbaya na bado amekuwa na imani na kuwasamehe waliomkosea licha ya wao waliomkosea kutotaka msamaha." Amesema Bi. Sancho.

Aidha katika maelezo yake wakati akizungumza na waandishi wa habari hii leo Januari 28, 2026, Sancho amemsifu Rais Samia kwa utekelezaji wake wa miradi mbalimbali ya maendeleo nchini pamoja na maboresho makubwa katika sekta za huduma za kijamii nchini, mambo ambayo ameyatekeleza katika kipindi kifupi cha uongozi wake.

Akizungumzia siku 100 za awali za kipindi cha pili cha Rais Samia, Sancho ameeleza kuhusu utekelezaji wa ahadi yake ya kuanza mchakato wa Bima ya afya kwa wote pamoja na utoaji wa ajira zaidi ya 12, 000 kwenye sekta ya afya na elimu kama alivyokuwa ameahidi wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa 2025.

Tuesday, 27 January 2026

DKT. MWIGULU ASHIRIKI ZOEZI LA UPANDAJI MITI, DODOMA

1/27/2026 11:48:00 am

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Januari 27, 2026 ameshiriki zoezi la upandaji miti, mbele ya ofisi ya Waziri Mkuu Mlimwa Jijini Dodoma.

Zoezi hilo ni sehemu ya hatua ya kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uamuzi wake wa kizalendo wa kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa kwa vitendo vya kulinda mazingira. 

Akizungumza baada ya zoezi hilo, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu akiwa ameambatana na mwenza wake Mama Neema Mwigulu, amempongeza Rais Dkt. Samia kwa uongozi wake kwa kuendelea kudhihirisha namna alivyo kiongozi mwenye maono, mbunifu na anayejali maslahi mapana ya Taifa.

“Shughuli hii imekuwa na utofauti kwa kusababisha miti ipandwe kila kona ya nchi, kwenye vitabu vyetu vitukufu, kupanda mti ni moja ya ibada kwasababu wanufaika wa miti ni wengi”

Kadhalika, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu ametoa wito kwa Watanzania kuadhimisha siku zao za kuzaliwa kwa kupanda miti. “Tunapokuwa na jambo la kukumbuka la aina hii, tufanye kitu ambacho kinaweka alama na manufaa kwa watu wengine”.

Mheshimiwa Waziri Mkuu amepanda mtu aina ya MDODOMA/MTIMAJI (Trichilia Emetica).

Sunday, 25 January 2026

KANISA LA ACK WAIRIMA LASHAMBULIWA KWA MABOMU, GACHAGUA ANUSURIKA

1/25/2026 09:54:00 pm


Makabiliano makubwa yameshuhudiwa katika Kanisa la ACK Wairima, Kaunti ya Nyeri alikokuwa anahudhuria ibada ya leo Jumapili Januari 25, 2026 aliyekuwa Makamu wa Rais wa Kenya Mhe. Rigathi Gachagua.

Kulingana na mashuhuda wa tukio hilo, Polisi waliokuwa wamefunika nyuso zao wametupa mabomu ya kutoa machozi na kurusha risasi za moto katika kanisa hilo, watu kadhaa wakijeruhiwa huku Gagachua na ujumbe wake wakofanikiwa kutoroka.

Hii si mara ya kwanza kwa Naibu huyo wa Rais wa zamani kushambuliwa kanisani ambapo Wiki mbili zilizopita shambulio kama hilo lilitokea nje ya kanisa la Independent Pentecostal Church of Africa (AIPCA) huko Kiamworia, Gatundu Kusini ambapo mafuriko yalitokea baada ya makundi hasimu ya vijana waliokuwa na virungu kuhusika katika vurugu nje ya Kanisa hilo.

Kwenye chapisho lake kwenye Mtandao wa X Gachagua amedai kuwa yeye na washirika wake walinaswa ndani ya Kanisa hilo baada ya shambulio hilo kutokana na kile alichokiita Jaribio la mauaji, akitoa wito wa wananchi kudumisha maombi dhidi ya amani ya nchi hiyo, akidai pia kuchomwa moto kwa magari yake.

Friday, 23 January 2026

WATENDAJI KITUO CHA UOKOZI MWANZA WATAKIWA KUTOA HUDUMA ZA DHARURA KWA SAA 24

1/23/2026 11:46:00 am

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba, ametoa maagizo kwa watendaji wa Kituo cha Kuratibu Utafutaji na Uokozi cha Kikanda – Mwanza, chenye thamani ya takribani shilingi bilioni 19.8, kuhakikisha kituo hicho kinaendeshwa kwa saa 24 na kwa ufanisi wa hali ya juu.

Amesema hayo leo Januari 23, 2026 baada ya kutembelea kituo cha Kuratibu Utafutaji na Uokozi, jijini Mwanza 

Amesisitiza kuwa huduma za uokozi ni kazi ya kuokoa maisha, hivyo hakuna uvumilivu kwa uzembe, kuchelewesha utoaji wa huduma za msaada pindi inapohitajika.

“Hii ni kazi ya kuokoa maisha. Uzembe, kusinzia au kuchelewesha kutoa msaada ni kuhatarisha maisha ya Watanzania. Kituo hiki lazima kifanye kazi saa 24.”

Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amesema ujenzi wa kituo hicho ni uthubitisho wa dhamira ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwatumikia watanzania na kujali changamoto mbalimbali nchini. 

“Kituo hiki kilikuwa kijengwe mwaka 2018 kwenda Mwaka 2020, kilisimama baada ya wenzetu kujitoa, lakini Rais Dkt. Samia akasema tutakijenga kituo hiki kwa fedha zetu ili wavuvi waweze kupata huduma ya usalama katika kazi zao”

MWENYEKITI WA CHADEMA MBEYA VIJIJINI MATATANI KWA UCHOCHEZI

1/23/2026 11:33:00 am

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limetangaza kumkamata na kumshikilia Bi. Getruda Japhet Lengesela, Mkazi wa Nsalala- Mbalizi na ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, Wilaya ya Mbeya Vijijini.

Taarifa kwa Vyombo vya habari iliyotolewa leo Ijumaa Januari 23, 2026 na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi SACP Benjamin Kuzaga imesema Mtuhumiwa huyo alikamatwa jana Januari 22, 2026 saa tatu usiku eneo la Nsalala, Mji mdogo wa Mbalizi kwa tuhuma mbalimbali za kijinai ikiwa ni pamoja na uchochezi.

Kulingana na Polisi, upelelezi unakamilishwa na hatua zaidi za kisheria zitachukuliwa dhidi yake mara baada ya upelelezi kukamilika.

Thursday, 22 January 2026

TUTACHUKUA HATUA KALI KWA WATAKAOTUMIA TAARIFA BINAFSI ZA WATU KINYEMELA- PDPC

1/22/2026 09:59:00 pm

Tume ya taarifa ya ulinzi wa Taarifa binafsi Tanzania PDPC imetangaza kuanza mara moja kwa ukaguzi wa uzingatiaji wa sheria kwa Taasisi za umma na za binafsi, zinazokusanya na kuchakata taarifa binafsi.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Alhamisi Januari 22, 2026, Mkurugenzi Mkuu wa Tume hiyo Dkt. Emmanuel Mkilia amesema zoezi hilo linafanyika mara baada ya muda wa hiari kuisha kulingana na tangazo la Tume hiyo lililoweka ukomo wa Aprili 8, 2026 kwa Taasisi husika kukamilisha usajili wao.

"Ukaguzi huu utahusisha kubaini Taasisi za umma na za binafsi zinazokusanya, kuhifadhi kuchakata na kusafirisha taarifa binafsi nje ya nchi bila kuzingatia matakwa ya sheria ya ulinzi wa taarifa binafsi sura ya 44 na kanuni zake na PDPC tutachukua hatua kali za kisheria dhidi ya yeyote, taasisi ama kampuni itakayokiuka sheria hii ikiwa ni pamoja na faini, kifungo, fidia kwa waathirika ama vyote kwa pamoja." Amesema Dkt. Mkilia.

Aidha PDPC imesema mtu ama Taasisi itakayobainika kutumia taarifa ya mtu binafsi bila ridhaa yake au kinyume na taratibu zilizowekwa kisheria, Taasisi hiyo itawajibishwa Ipasavyo bila ya kujali hadhi ama ukubwa wa Taasisi itakayokiuka misingi ya sheria katika ulinzi wa taarifa binafsi.

Pamoja na mafanikio yanayotokana na ukuaji wa TEHAMA duniani, kumekuwepo na changamoto mbalimbali ikiwemo ulinzi wa taarifa binafsi ambazo zimekuwa zikikusanywa, zikichakatwa na wakati mwingine kusafirishwa kutoka nchi moja kwenda nyingine bila kuzingatia utaratibu na misingi ya ulinzi wa taarifa binafsi iliyokubalika kisheria.

WANANCHI WA UKONGA WAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUDUMISHA AMANI NA USALAMA

1/22/2026 09:32:00 am

Wananchi wa Ukonga Mkoani Dar Es Salaam wametoa pongezi na Shukrani kwa Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuimarisha amani, utulivu na usalama katika Jimbo lao la Ukonga, suala ambalo limewezesha shughuli za kiuchumi na kijamii kuendelea.

Kwaniaba ya wananchi wengine wa Jimbo hilo wakati akizungumza na Chombo chetu cha habari, Bw. Salum Issa Salum, Mkazi wa Kata ya Buyuni ameeleza kuwa licha ya kupitia baadhi ya changamoto mwishoni mwa mwaka jana, hali kwasasa ni shwari na hatua za maendeleo zimeendelea kushuhudiwa katika Kata hiyo na maeneo mengine kote Tanzania.

"Nisemee zaidi katika miundombinu, Mama amesikia kilio chetu na sasa barabara nyingi zimejengwa kwa kiwango cha lami kupitia miradi mbalimbali ikiwemo mradi wa DMDP kutoka hapa kwetu kwenda Kivule." Amesema Bw. Salum.

Katika maelezo yake, Mwananchi huyo amemuombea uhai zaidi na afya njema Rais Samia, akisisitiza pia umuhimu wa kila mwananchi kushiriki kikamilifu katika kuilinda amani ya Tanzania ili kutoa fursa ya Taifa na kila mwananchi kupiga hatua za kimaendeleo.

VIONGOZI WA CHADEMA MBEYA WASHIKILIWA WAKIHAMASISHA MIKUSANYIKO BATILI

1/22/2026 09:14:00 am

Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya linamshikilia Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Mkoa wa Mbeya Bw. Masaga Pius Kaloli na Mwenyekiti wa BAVICHA Mkoa wa Mbeya Elisha Chonya kwa tuhuma za kuhamasisha watu kufanya mikusanyiko isiyokuwa halali.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya Benjamin Kuzaga amesema watuhumiwa hao walikamatwa Januari 21, 2026 saa tisa alasiri katika Kijiji na Kata ya Inyala baada ya Polisi kupata taarifa za uwepo wa Viongozi hao katika eneo hilo wakifanya maandalizi na wakiwahamasisha watu kukusanyika ili kufanya Mkutano bila bila kufuata taratibu za kisheria zilizopo.

"Pamoja na kukiuka kwa makusudi taratibu hizo za kisheria, ikimbukwe kuwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kimezuiliwa na Mahakama kufanya shughuli zozote za kisiasa." Amesema Kamanda Kuzaga.

Taarifa hiyo ya Polisi Mkoa wa Mbeya imeendelea kueleza kuwa upelelezi unakamilishwa ili hatua zaidi za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi ya watuhumiwa hao.

Friday, 9 January 2026

TABORA WAUPOKEA MWAKA MPYA KWA AMANI NA UTULIVU MKUBWA

1/09/2026 11:19:00 am
TABORA WAUPOKEA MWAKA MPYA KWA AMANI NA UTULIVU MKUBWA

Wananchi wa maeneo mbalimbali Mkoani Tabora wameshiriki kwa namna mbalimbali kusherehekea sikukuu ya Mwaka mpya 2026 na kuuaga mwaka 2025, Burudani za muziki katika sehemu mbalimbali za starehe zikionekana kujaa zaidi, amani na utulivu ukitawala pia katika maeneo hayo.


Wengine pia kama ilivyo utamaduni wa wananchi wa Tabora, wameonekana jana usiku Januari Mosi, 2026 wakiwa kwenye mitaa mbalimbali wakiimba na kusherehekea kuumaliza mwaka 2025 na kuuanza mwaka mpya 2026.

Polisi pia wameonekana katika maeneo yote yenye mikusanyiko mikubwa ya watu ili kuhakikisha hali ya ulinzi na usalama inakuwepo ili kutoa fursa ya kila mmoja kufurahi na wengine kuendelea na biashara zao bila ya vitisho vyovyote vya uvunjifu wa amani kwenye jamii.

Jana Disemba 31, 2025 wakati wa hotuba yake ya kuukaribisha mwaka Mpya, Rais Samia Suluhu Hassan wa Tanzania, aliwatakia kheri na mafanikio tele watanzania wote, akiahidi kwamba serikali yake itaendelea kuwatumikia watanzania wote kikamilifu ikiwa ni pamoja na kujenga umoja wa Kitaifa nchini, akitoa rai ya kutokubali kugawanyika kiitikadi na kimtazamo wanapoendelea na ujenzi wa Taifa lao.

AMANI YATAWALA, WATANZANIA WAKISHEREHEKEA MWAKA MPY

1/09/2026 11:19:00 am

Tanzania kama ilivyo kwenye Mataifa mengine kote duniani inasherehekea mwaka mpya wa 2026, Mamilioni wakishuhudia fataki, sherehe za kitamaduni na kidini na mikusanyiko ya kifamilia na kindugu, kuashirikia mwanzo wa mwaka mpya wa 2026 wakiwa na wingi wa matumaini ya ustawi na maendeleo yao binafsi.

Mkoani Dar Es Salaam, leo mchana katika maeneo mbalimbali kumeendelea kushuhudiwa mikusanyiko ya watu, ikiwemo eneo maarufu la Coco Beach, Wilayani Kinondoni ambapo watu wazima kwa watoto wameshuhudiwa wakibarizi katika fukwe hizo usalama ukiimarishwa na Polisi waliokuwa doria, kuhakikisha kila mmoja anaifurahia siku hii.

"Tunafurahi kuingia mwaka mpya, mwaka jana umekuwa na mchanganyiko wa mambo lakini tunamshukuru Mungu kwa hatua za maendeleo tulizopiga na zaidi kwa kuendelea kuitunza amani yetu. Niwaombe watanzania tusirudi tena kule kwenye vurugu, tuione thamani ya amani, tuilinde na tuwakatae wote wanaotaka kuipoteza." Amesema Bi. Amina Seleman, mmoja wa wananchi waliozungumza nasi Coco Beach.

Tofauti na wachache kwenye Mitandao ya kijamii walivyokuwa wakihamasisha kufanyika kwa maandamano hii leo, amani imeendelea kushuhudiwa, Watanzania wakipuuza miito hiyo ya maandamano na kuendelea na sherehe za mwaka mpya 2026.

Wednesday, 31 December 2025

Yapiga Marufuku uchomaji wa matairi na upigaji fatati usiokuwa na vibali_

12/31/2025 05:20:00 pm


 *_Yapiga Marufuku uchomaji wa matairi na upigaji fatati usiokuwa na vibali_*


Jeshi la Polisi nchini Tanzania limetoa wito kwa wananchi kusherehekea sikukuu ya mwisho wa mwaka na kuukaribisha mwaka mpya kwa kuzingatia sheria na kuzingatia kanuni za kiusalama, likisisitiza kuwa imara katika kuimarisha usalama kwa misingi ya sheria.

Aidha Polisi imetoa rai kwa kila mzazi kuzingatia ulinzi kwa watoto kama sheria, kanuni na taratibu zinavyoelekeza ili kuwaepusha na madhara mbalimbali ikiwemo  kupotea kama ilivyoshuhudiwa katika sikukuu nyingine zilizopita.

Taarifa ya Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini Tanzania David Misime kwa Vyombo vya habari  imesisitiza pia kwa watumiaji wa Vyombo vya moto na watumiaji wa barabara kuzingatia na kutii sheria za usalama barabarani na kuongozwa na kaulimbiu ya wiki ya nenda kwa usalama barabarani isemayo "Familia yako inakusubiri zingatia usalama."

"Kulingana na desturi zetu kama Watanzania huwa tunakuwa na shughuli mbalimbali katika kuhitimisha mwaka na kuukaribisha mwaka mpya ikiwemo kushiriki kwenye mikusanyiko ya kumwomba na kumshukuru Mungu kwenye nyumba za ibada na wengi huka na familia, ndugu, na marafiki na kusherehekea aidha majumbani au sehemu wanazoona zinafaa kufanya hivyo."

Ili hayo matumainu ya kila mmoja wetu na shughuli hizo ziweze kufanyika bila hofu, au wasiwasi, amani, utulivu na uaalama lazima uwepo. Kwa mantiki hiyo Jeshi la Polisi linatoa wito ili kila mmoja aweze kusherehekea sikukuu hizi kwa namna anavyoona inafaa ili mradi havunji sheria ni wajibu wa kila mmoja kuzingatia kanuni za kiusalama kwani usalama huanza na wewe kwanza." Amesema David Misime.

Polisi pia kupitia kwa Msemaji wake David Misime imebainisha kuwa kwa wale waliomba vibali vya kupiga fataki na wakaruhusiwa, wametakiwa kuzingatia maelekezo na muda waliopewa ili kuepuka usumbufu kwao na kwa wengine hasa wagonjwa,Polisi pia ikipiga marufuku uchomaji wa matairi.

Monday, 29 December 2025

Serikali yaipeleka NIDA Kidigitali,Lengo kurahisisha Utolewaji wa Vitambulisho

12/29/2025 09:10:00 pm

Na Mwandishi Wetu,

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene, amezindua namba maalumu, itakayotumiwa na wananchi kufuatilia kitambulisho cha taifa baada ya kuwasilisha maombi ya kitambulisho hicho, hali itakayopelekea wananchi kupata na kujua taarifa za maombi ya kitambulisho kwa kutumia namba maalumu hiyo.

Amezindua namba hiyo maalumu, leo jijini Dar es Salaam,  ambapo   amesema vitambulisho vingi vimezalishwa na tayari vimepelekwa sehemu husika, ikiwemo wilayani  ambapo muombaji wa kitambulisho alijiandikishia na bado wahusika awajafuata kadi zao hali inayopelekea baadhi ya wananchi kukosa huduma mbalimbali huku akizitaja huduma za afya, mafao ya ustawi, usajili wa wanafunzi katika vyuo mbalimbali samabamba na  maombi ya mikopo kutoka Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu(HESLB).

“Hivi leo tunavyozungumza katika wilaya zetu zote nchini, viko vitambulisho vingi sana ambavyo havijachukuliwa na sababu kubwa inakua kwamba muombaji hajui kitambulisho chake kipo katika hatua gani, kupitia mfumo huu ambao ninauzindua utajibiwa na utaambiwa kama namba yako umepata ndani ya siku tano na kama ujapata ndani ya siku tano tangu ulipoomba ukitumia mfumo huu(15274) utajibiwa kwanini ujapata.”Amesema Waziri Simbachawene

Ameongeza pia serikali inafikiria kusitisha matumizi ya namba ya utambulisho (NIN) kwani watu wengi wameacha kwenda kuchukua vitambulisho vyao, ambavyo vimezalishwa kwa fedha nyingi ya kodi ya watanzania, hivyo wanapaswa kwenda kuchukua vitambulisho vyao na sio kutumia namba ya utambulisho kama kitambulisho.

Akizungumza katika uzinduzi huo,Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa(NIDA),James Kaji amesema mamlaka imeendelea kushusha vitambulisho hadi ngazi ya kata lakini bado wananchi hawajavifuata vitambulisho  na wameamua kuvipeleka  wilayani na anaamini sasa kupitia mfumo huo mpya wa namba 15274 vitambulisho vitaendelea kufuatwa kwani mfumo huo umerahisisha zaidi taarifa za muombaji kupatikana mkononi kiganjani kwa kupitia simu ya mkononi.

DKT. MWIGULU AKAGUA HALI YA UZALISHAJI NA USAMBAZAJI WA MAJI RUVU CHINI*

12/29/2025 01:36:00 pm

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Desemba 29, 2025 amekagua hali za uzalishaji na usambazaji wa maji eneo la Ruvu Chini, mkoani Pwani.

Akizungumza baada ya ukaguzi huo, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amesema kuwa ili kukabiliana na changamoto ya upungufu wa maji unaotokana na mabadiliko ya tabia nchi, Serikali ilianza utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maji katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita.

“Mipango hii ya ujenzi wa miradi inayolenga kukabiliana na changamoto ya upungufu wa maji ilianza muda mrefu, Serikali iliona na ilianza kutafuta majawabu ya hali hii miaka mitatu iliyopita kwa kujenga miradi mikubwa itakayotoa matokeo chanya” Amesema Dkt. Mwigulu

FAMILIA NI MSINGI WA HAKI NA USTAWI, TUZILINDE- MHE. MTAMBULE

12/29/2025 01:35:00 pm

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mkoani Dar Es Salaam Mhe. Saad Ahmed Mtambule amesisitiza Waislamu na Watanzania wote kwa Ujumla kurejea katika misingi na maadili ya Kitanzania kwa kuimarisha familia na kulea Vijana katika maadili na utamaduni wa Kitanzania.

Mhe. Mrambule amebainisha hayo leo Jumamosi Disemba 27, 2025 wakati wa kongamano la dini Jijini Dar Es Salaam, akisisitiza kuwa familia  ndiyo msingi wa haki na ustawi wa watu na Taifa kwa ujumla, hivyo ni muhimu kuwekeza katika familia na maadili ya Mtanzania katika kukuza jamii.

"Chakula kikuu cha amani ni sisi binadamu na sisi chimbuko letu si chama cha siasa ama ofisi fulani. Chimbuko letu sisi ni Familia kama Taasisi ya kwanza ya binadamu. Familia ni msingi wa amani, msingi wa haki na msingi wa ustawi wa Taifa lolote lile."Amesema Mhe. Mtambule.

Katika hatua nyingine, Mhe. Mtambule amebainisha kuwa ikiwa ataonekana mtu asiyefuata maadili, mwenye kuendekeza vitendo vya rushwa, ubadhirifu na kutowajibika vyema ni kushindwa kwa Taasisi familia, akisema kabla ya shule, vyama vya siasa na Taasisi za kidini ni muhimu kutambua umuhimu na nafasi ya familia katika malezi na kumtengeza raia.

AMANI NA UTULIVU VYATAWALA SIKUKUU YA KRIMASI DAR ES SALAAM

12/29/2025 01:35:00 pm

Maelfu ya Wananchi wa Mkoa wa Dar Es Salaam wameendelea kujitokeza katika maeneo mbalimbali Jijini hapa kwaajili ya kusherehekea Sikukuu ya Krismasi, iliyo maarufu zaidi kwa waumini wa dini ya Kiikristo kote ulimwenguni ikiwa leo ni siku ya pili maarufu kama Boxing day, siku maalum kwaajili ya kupeana zawadi za Krismasi.

Suala la amani, utulivu na usalama limeshuhudiwa pia katika maeneo yenye misururu ya watu ikiwemo kwenye Fukwe za Coco (Coco Beach), Wilayani Kinondoni pamoja na eneo maarufu la Mlimani city.

Katika fukwe hizo, Polisi wameonekana wakfanya doria za mguu, farasi pamoja na magari ili kuhakikisha kila mmoja anasherehekea sikukuu hiyo kwa amani na utulivu, wananchi wakiipongeza serikali na polisi kwa kuhakikisha amani inaendelea kuwepo.

Kwa nyakati tofauti mara baada ya kushindwa kwa upangaji, uratibu na ufanyikaji wa maandamano yaliyokuwa haramu hapo Disemba 09, 2025, baadhi ya wanaharakati walikuwa wakihamasisha maandamano hayo kufanyika katika sikukuu hii, kabla ya kupingwa na kukataliwa kwake kulikofanywa na Watanzania wenye kutambua na kuhamasisha zaidi umuhimu wa amani na utulivu kwa mustakabali wa maendeleo na ustawi wa Taifa na Mtanzania mmoja mmoja.

Friday, 26 December 2025

JESHI LA POLISI LAWASHUKURU WATANZANIA KWA KUDUMISHA AMANI SIKU YA KRISMASI

12/26/2025 01:12:00 pm

Na Mwandishi wetu,Dodoma

Jeshi la Polisi Tanzania limetoa shukrani kwa wananchi wote nchini kwa ushirikiano waliouonyesha katika kulinda na kudumisha amani kipindi chote cha Sikukuu ya Krismasi, iliyoadhimishwa  25 Desemba 2025. 

Kwa mujibu wa Taarifa  iliyotolewa na Msemaji wa Jeshi la Polisi Makao Makuu, Dodoma DCP David Misime
,amesema hatua hiyo imewezesha sherehe za mwaka huu kufanyika kwa utulivu na bila changamoto  za kiusalama. 

Amesema hali ya usalama imeendelea kuwa shwari katika maeneo yote ya nchi, huku wananchi wakiendelea kusherehekea sikukuu kwa kufuata sheria, taratibu na kanuni za nchi bila wasiwasi wala hofu. 

" Jeshi la Polisi limeeleza kuwa ushirikiano baina ya wananchi na vyombo vya ulinzi umekuwa nguzo muhimu katika kufanikisha dhamira ya kulinda amani na kutengeneza mazingira mazuri ya kusherehekea, "amesema

Akitoa wito kwa umma, Msemaji wa Jeshi hilo amewataka Watanzania kuendelea kuilinda amani kama msingi wa maendeleo ya taifa. 

“Tunaendelea kuwasihi wananchi kudumisha amani kwani ndiyo inatupa fursa ya kusherehekea bila hofu tukiwa na marafiki na jamaa,” amesema.

 Ameongeza kuwa bila amani hakuna shughuli za kijamii na kiuchumi zinazoendelea kwa ufanisi.

Kupitia taarifa hiyo amebainisha kuwa shughuli za kiuchumi, ikiwemo biashara, usafirishaji, huduma za kijamii na kazi za utumishi wa umma zinaendelea kama kawaida bila wasiwasi wowote.

Aidha  Jeshi hilo linasisitiza wananchi kuendelea ushirikiano na utulivu huku likiahidi  kuendelea kuimarisha ulinzi katika maeneo yo te na , kuhakikisha kila raia anabaki salama wakati wote.

 Pia limewataka wananchi kuendelea kutoa taarifa mapema pale wanapotilia shaka viashiria vya uvunjifu wa amani, ili kuchukua hatua za haraka na kuzuia madhara yanayoweza kujitokeza.

Mwishoo

Thursday, 25 December 2025

Waziri Simbachawene atahadharisha watanzania kujiepusha na msukumo wa dhulma,uongo na ubinafsi

12/25/2025 06:16:00 pm
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene ameitahadharisha jamii ya watanzania kujiepusha na msukumo wa dhulma,uongo na ubinafsi unaoenezwa kupitia  mitandao ya kijamii…. …

Ametoa rai hiyo leo, wakati wa Ibada ya Krismasi iliyosaliwa katika Kanisa la Parokia ya Pwaga, wilayani Mpwapwa, mkoani Dodoma  huku Paroko wa Parokia hiyo,Padri Daniel Kijaji akimuombea hekima na busara katika jukumu alilokabidhiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt.Samia Suluhu Hassan la kuiongoza wizara hiyo ambapo pia alimshukuru kwa kuchangia kiasi cha Shilingi Milioni Kumi kwa ajili ya ujenzi wa Kanisa hilo.

Monday, 22 December 2025

POLISI YAJIIMARISHA KULINDA RAIA MSIMU HUU WA KRISMASI NA MWAKA MPYA

12/22/2025 07:43:00 pm

Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, (DCP) David Misime, amesema Jeshi hilo kwa kushirikiana na Vyombo vingine vya ulinzi na usalama vitaendelea kuimarisha ulinzi na usalama wakati na baada ya sikukuu za Krismasi na Mwaka mpya, wito ukitolewa kwa kila mwananchi kutambua na kuheshimu thamani na umuhimu wa amani na usalama kwa kila mmoja.

Taarifa iliyotolewa leo Jumatatu Disemba 22, 2025 na Jeshi la polisi imewataka pia wale wote watakaokuwa wakisafiri kutoka eneo moja kwenda jingine kuzingatia sheria za usalama barabarani kama sehemu ya kuepuka ajali za barabarani, wakikumbusha kuhusu kaulimbiu ya wiki ya nenda kwa usalama isemayo "endesha salama, familia inakusubiri."

"Maisha yetu na shughuli zetu wakati wa hizi sikukuu yanahitaji mazingira ya amani ili kila mmoha aweze kushiriki kwenye ibada za kumshukuru Mungu, kukaa na familia na marafiki bila ya bugudha yeyote ile hivyo tuilinde amani kwa ushirikiano na kwa nguvu zetu zote." Imesema taarifa hiyo.

"Aidha wito unatolewa kwa wananchi wote na kwa wote watakaokuwa nchini kuwa kinachohitajika ni kila mmoja wetu kutambua thamani na umuhimu wa amani na usalama, ni wakati muafaka pia kuendelea kuyakataa yale ambayo yana malengo ya kuvuruga amani kipindi hiki cha sikukuu na baada." Imeongeza kusema taarifa hiyo ya polisi.

Polisi pia imeeleza kuwa hali ya usalama nchini ni shwari licha ya matukio machache ya uvunjifu wa amani yaliyojitokeza, likisema hali hiyo imetokana na Watanzania kufahamu umuhimu wa kila mmoja kulinda na kuimarisha amani, utulivu na usalama kama nyenzo kuu ya kuwawezesha kushiriki katika shughuli za kijamii na kiuchumi.

Friday, 19 December 2025

KIKAO CHA KAMATI YA WATAALAM YA KITAIFA YA USIMAMIZI WA MAAFA CHAPITISHA MIONGOZO YA KUKABILIANA NA MAAFA NCHINI*

12/19/2025 09:49:00 pm

Na mwandishi wetu, Dodoma.

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Dkt. Jim Yonazi ameongoza Kikao cha Kamati ya Wataalam ya Kitaifa ya Usimamizi wa Maafa leo 19 Desemba,2025 kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano uliopo Ofisi ya Waziri Mkuu Ngome, Jijini Dodoma.

Katika kikao hicho, Mpango wa Taifa wa dharura wa  kukabiliana na Ukame, Mafuriko na Majanga mengine yanayohusiana kwa kipindi cha Novemba 2025 hadi Juni 2026 umejadiliwa na kupokelewa na wajumbe wa kikao.

Aidha, Miongozo ya uanzishwaji na Uendeshaji wa kituo cha operesheni na Mawasiliano ya dharura na Timu ya kukabiliana na Dharura ngazi ya Taifa na Mkoa imejadiliwa na kupitishwa na wajumbe wa kikao.

Miongozo iliyojadiliwa na kupitishwa ni pamoja na, Mwongozo wa Uanzishaji wa kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura, Mwongozo wa Uendeshaji wa kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura Ngazi za Mikoa, Mwongozo wa Uanzishaji na Uendeshaji wa Timu ya Mkoa ya kukabiliana na Dharura.

Pia, Muongozo wa Uanzishaji na Uendeshaji wa Timu ya Taifa ya kukabiliana na Dharura, Muongozo wa Uendeshaji wa Kituo cha Taifa cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura, Muongozo wa kuandaa Mpango wa Mkoa wa kujiandaa na kukabiliana na Maafa.

Pamoja na hayo, Wajumbe wa kikao hicho walipokea na kuridhia Mkakati wa Utekelezaji wa Mpango wa Utoaji wa Huduma za Tahadhari ya mapema kwa wote kwa kipindi cha miaka Mitano (2026-2030).

Awali, Dkt Yonaz ametoa Pongezi kwa Taasisi na Sekta mbalimbali zinazokabiliana na Maafa kwa kuendelea kufanya vizuri na kutoa Elimu ya maafa Nchini na Nchi Jirani.

=MWISHO=

Dkt,MWIGULU AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MADARAJA LINDI.*

12/19/2025 07:25:00 pm

_Asisitiza Rais Dkt. Samia amedhamiria kushughulika kwa vitendo na umasikini wa watanzania_

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Desemba 19, 2025 amekagua maendeleo ya ujenzi wa Madaraja na Ukarabati wa barabara kuu ya Marendego-Nangurukuru-Lindi-Mingoyo

Akizungumza baada ya ukaguzi huo, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amewaambia wakazi wa Somanga mkoani Lindi kuwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anatekeleza miradi ya kimkakati ili kushughulika kwa vitendo na umasikini wa Watanzania

Amesema kuwa Rais Dkt. Samia alisimamia ukamilishaji wa Bwawa la Kuzalisha Umeme la Julius Nyerere ili kuhakikisha kila mtanzania ananufaika na huduma ya nishati ya umeme. 

“Tumeshuhudia Rais Dkt. Samia namna anavyotekeleza miradi kwenye sekta mbalimbali ikiwemo uvuvi, maji, kilimo, afya, elimu na hata uwezeshaji wananchi kiuchumi”

TARURA YAPEWA TUZO KUTAMBUA MCHANGO WAKE KATIKA SEKTA YA UCHUKUZI

12/19/2025 06:46:00 pm

Arusha

Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) imepewa tuzo ya  kutambua mchango wake katika maendeleo ya sekta ya uchukuzi nchini. 

Tuzo hiyo imekabidhiwa na Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mhe. Joseph Mkude akimwakilisha Waziri wa Uchukuzi na kupokelewa na Mkurugenzi wa Mipango ya Miundombinu, Mhandisi Edward Amboka.

Tuzo hiyo imetolewa katika Mkutano wa 18 wa Tathmini ya Utendaji wa Sekta ya Uchukuzi uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa (AICC) jijini Arusha.

TARURA imeshiriki Mkutano huo ikiwa ni mdau wa sekta ya uchukuzi, ambapo ilitumia Mkutano huo kwa kuwasilisha utekelezaji wa shughuli za Wakala kwa mwaka wa fedha 2024/2025 na kutoa elimu kwa wadau kuhusu majukumu na kazi mbalimbali zinazofanywa na Wakala.

Mpango wa Elimu kwa Umma Kuhusu Muungano utakuwa endelevu

12/19/2025 02:06:00 pm
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni amesema Mpango wa Elimu kwa Umma Kuhusu Muungano utakuwa endelevu ili kuhakikisha elimu hiyo inamfikia kila mmoja. 

Ameyasema hayo Desemba 19, 2025 wakati akizungumza katika kipindi cha Asubuhi Njema kinachorushwa na ZBC ambapo amesema Waandishi wa Habari wanayo nafasi kubwa katika utoaji wa elimu kwa umma ndio maana Ofisi ya Makamu wa Rais imewapa nafasi na itakuwa ikishirikiana nao kwa asilimia kubwa.

“Katika kuhakikisha hilo leo tumeandaa Semina ya Wahariri wa Vyombo vya Habari Zanzibar kisha tutaifanya kwa Wahariri Bara na baadaye tutaandaa makongamano mbalimbali.”
 
Amesema Mpango wa Elimu kwa Umma kuhusu Muungano,  wanufaika wakubwa watakuwa vijana ambao ndio walengwa kutokana na wengi wao kuwa wamezaliwa baada ya Muungano(1964).

Tuesday, 16 December 2025

Watanzania naomba tulinde Amani kwa maendeleo yetu Binafsi

12/16/2025 07:27:00 pm

Watanzania wamehfgimizwa kulinda na kuitunza miundombinu inayojengwa katika maeneo mbalimbali nchini ili iweze kudumu na kutumika kwa muda mrefu zaidi na kuwanufaisha zaidi, wakihimizwa pia kulinda amani kwa maslahi ya ustawi na maendeleo binafsi na ya Taifa kwa ujumla.

Wito huo umetolewa na Bi. Fatuma Ramadhan Mchekwa, Mkazi wa Temeke Jijini Dar Es Salaam wakati akizungumza na chombo chetu cha habari leo Jumanne Disemba 16, 2025, akisisitiza kuwa uharibifu wa Miundombinu umekuwa ukiligharimu taifa fedha nyingi.

"Tunachoomba sisi ni amani, amani iendelee na tusifanye fujo kwasababu tunapoharibu miundombinu ikiwemo ya mwendokasi hizi ni kodi zetu wenyewe kwahiyo tunajikomoa wenyewe. Tunafanya biashara  tunalipa ushuru na kodi zetu ndizo zinazoleta maendeleo ila leo badala ya kusema tuendelee kuleta maendeleo tunarudi kukarabati miundombinu iliyoharibiwa." Amesema Bi. Fatuma.

Katika hatua nyingine Bi. Fatuma amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa ujenzi wa miundombinu mbalimbali ikiwemo ujenzi wa barabara ya Mbagala- Kariakoo, ujenzi wa shule ya msingi Kidugulo pamoja na kufikisha umeme kwenye maeneo yote ya Chanika, suala ambalo limeboresha maisha ya wananchi kupitia sekta mbalimbali za kiuchumi na kijamii.L

Wafugaji Chanika waishukuru Serikali ujio wa miradi mikubwa ya ufugaji.

12/16/2025 04:31:00 pm

Wafugaji wa Kata ya Chanika, Wilayani Ilala Mkoani Dar Es Salaam wameishukuru serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan kwa mapinduzi na ujio wa miradi mikubwa ya ufugaji iliyowasaidia kujikwamua na umaskini na kuongeza kipato.

Kwaniaba ya wafugaji hao, Bw. Hamim Idrisa, Katibu wa Wafugaji Kata ya Chanika, ameeleza kuwa ipo miradi mitatu iliyozinduliwa katika Kata ya Chanika katika kipindi cha miaka minne ya awamu ya kwanza ya Rais Samia, ambayo imewaneemesha wafugaji ikiwemo mradi wa kuku wa Mayai na mradi wa kukabiliana na usugu wa madawa ya mifugo.

"Mradi wa kwanza ni ufugaji wa kuku bila dawa ambao umekuwa msaada mkubwa sana kwetu, upo pia mradi wa kukabiliana na usugu wa madawa dhidi ya vimelea vya magonjwa na mradi wa mwisho ni huu wa kuku wa mayai ambapo serikali inatupa nyenzo, madawa na elimu kupitia Maafisa tulionao kwenye Kata yetu." Amesema Bw. Idrisa.

Katika upande wa maendeleo ya Jamii na ustawi, Bw. Idrisa amezungumzia sekta ya afya, akiishukuru serikali kwa ujenzi wa Chumba cha kuhifadhia maiti kwenye Hospitali ya Nguvu Kazi pamoja na kuanza kwa mradi wa Zahanati ya Kidugilo, ambapo fedha na eneo la utekelezaji wa mradi huo imeshapatikana.

Monday, 15 December 2025

Chanika yapaa kimaendeleo miaka minne ya Rais Samia

12/15/2025 10:44:00 pm
CHANIKA WAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA UJENZI WA SHULE NA MOCHWARI

CHANIKA YAPAA KIMAENDELEO, MIAKA MINNE YA RAIS SAMIA

Wananchi wa Kata ya Chanika, Ilala Mkoani Dar Es Salaam wamemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa maboresho makubwa ya huduma za afya na elimu Wilayani humo, wakisisitiza umuhimu wa wazazi kuwaandikisha watoto wao katika msimu ujao wa masomo 2026, ili waweze kunufaika na uwekezaji mkubwa uliofanywa ndani ya Wilaya ya Temeke na Tanzania kwa ujumla.

Wananchi hao wameeleza namna ambavyo walilazimika kusafirisha miili ya wapendwa wao wanaofariki kwenda kuhifadhiwa Wilayani Kisarawe kutokana na kukosekana kwa Vyumba vya kuhifadhia maiti katika Kata yao ya Chanika kwenye Hospitali ya Nguvukazi.

Akizungumza na mwandishi wetu wa habari Bi. Jaliah Kabeya, Mkazi wa Chanika Jijini Dar Es Salaam amesema kwasasa katika sekta ya elimu na afya hakuna changamoto yoyote, akishukuru pia kwa ujenzi wa barabara za ndani ya Wilaya yao ikiwemo changamoto ya mafuriko Tazara suala ambalo lilikuwa likikwamisha shughuli za usafiri na usafirishaji ndani ya eneo hilo.

"Tunamshukuru Mungu na Mama Samia kwa hili, tumuombee dua ili aendeleze pale alipobakiza kwasababu yeye si malaika na hawezi kufanya yote kwa wakati mmoja na kwa haya aliyoyafanya pia ni muhimu kuwa na roho shukrani." Amesema Bi. Jaliah.

Mwananchi huyo pia ameshukuru kwa usimamizi wa mikopo ya Asilimia kumi ya Halmashauri inayotolewa kwa wanawake, Vijana na wenye ulemavu, akisema suala hilo limesaidia pakubwa kuwakwamua wananchi na umaskini, akisifu pia michakato yake na mikopo kuwa rahisi.

WAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUBORESHA HUDUMA ZA KIJAMII NCHINI

12/15/2025 10:37:00 pm


RAIS SAMIA AMETUONDOLEA UKATILI WA KIJINSIA NCHINI- BI. MAPUNDA0

WANAWAKE WAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUWAENZI NA KUWAPATIA MAHITAJI

Bi. Sikitiko Casian Mapunda, Mkazi wa Nguvu Mpya Jijini Dar Es Salaam amemtaja Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kama Kiongozi na Mama jasiri na shujaa, akimshukuru kwa kuwekeza katika masuala ya Kijamii ikiwemo yanayowahusu wanawake pamoja na watoto.

Bi. Mapunda amebainisha hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatatu Disemba 15, 2025, akisema huko nyuma baadhi ya Makundi yalisahaulika ikiwemo wanawake na Vijana, akisema ni mara ya kwanza kuona Rais akiwaita Vijana na kuwasikiliza kero na changamoto walizonazo.

"Nimshukuru pia sana Mama kwa namna alivyoifanya miundombinu ya GongolaMboto kupitika tofauti kabisa na zamani ilivyokuwa. Sasa hivi barabara ya Gongolamboto ni tofauti kabisa na ilivyokuwa miaka mitano iliyopita, ni kama barabara za Ulaya, tuna Mahospitali na mpaka barabara za ndani nazo zinapitika wakati wote." Amesema Bi. Mapunda.

Amemshukuru Rais Samia pia kuhusu usimamizi wake wa mikopo ya asilimia kumi inayotolewa na Halmashauri kwaajili ya wanawake, Vijana na wenye ulemavu, akimuomba pia kushughulikia masharti magumu ya upatikanaji wa mikopo hiyo.

Katika hatua nyingine Bi Mapunda pia akizungumza na mwandishi wetu wa habari, ameeleza na kushukuru kupungua kwa matukio ya ukatili wa kijinsia nchini ikiwemo matukio ya ubakaji kwa wasichana na wanawake, akisema huko nyuma kabla ya ujio wa Rais Samia udhalilishaji ulikuwa mkubwa na wanawake wengi wa Mijini na Vijijini walikuwa na hofu kubwa ya kupita katika baadhi ya maeneo kwa kuhofia matukio ya ubakaji yaliyokuwepo.

KIKUNDI CHA WAMANDA WAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA MAONO YAKE

12/15/2025 12:33:00 pm

Kikundi cha Akinamama wanaonufaika na Mikopo ya asilimia kumi ya Halmashauri cha Wamanda kilichopo Nzega Mkoani Tabora wamemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa usimamizi na maboresho makubwa ya mfumo wa Mikopo hiyo, wakisema imewasaidia kiuchumi na kuwaongezea kipato kwa asilimia kubwa.

Bi. Stellah William, Kwa niaba ya wanakikundi wenzake amesema kupitia kipato wanachokipata sasa kupitia kikundi hicho, ameweza kusomesha watoto, kuendesha maisha pamoja na kumpa ujasiri mkubwa wa kuweza kutafuta fedha na kujiendeleza kiuchumi.

"Kwakweli kikundi hiki kimeninufaisha kwenye kusomesha watoto na wajukuu wangu, naendelea pia kunufaika na mambo mengi sana na zaidi kimenifanya niwe jasiri wa kutafuta fedha nikiwa peke yangu."

Nimpongeze pia Mama Samia kwa kuwa na maono yake ya kuona kuwa hata Kijijini kuna watu wanahitaji msaada wake na nimuombe Mama Samia asituchoke, tunamuhitaji sana na atuangalie kwa macho yake yote sisi akinamama wa Vijijini." Amesisitiza Bi. Stellah William.

Saturday, 13 December 2025

E- MREJESHO KUKUZA UWAJIBIKAJI KWA WATUMISHI WA UMMA

12/13/2025 12:21:00 pm

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema Wizara hiyo imefanya maboresho mbalimbali ya mifumo yake ikiwemo mfumo wa e- mrejesho, ili kutoa fursa zaidi kwa wananchi wa pembezoni kutoa maoni, malalamiko na pongezi kuhusu huduma zinazotolewa na serikali na Taasisi zake.
Mhe. Ridhiwani amebainisha hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar Es Salaam, akisema mfumo huo unapatikana kwenye simu za mkononi kupitia nambari *152*00#, ukiwa na module ya sema na Kiongozi, sehemu inayomruhusu mwananchi kutoa maoni kwa Waziri, Mkuu wa Mkoa ama Kiongozi mwingine, akisema mfumo huo utakusanya maoni na kisha kuchakatwa na kufanyiwa kazi.

"Mfumo huu wa e- mrejesho ni kiunganishi cha moja kwa moja cha mwananchi na Kiongozi na hii itatusaidia pale tunapojadili namna ya kuboresha mifumo ya utumishi wa umma na ni mfumo wa kweli huu, hata kama kuna Kiongozi hatojibu sisi tutasimamia kuhakikisha majibu yanapatikana." Amesema Mhe. Ridhiwani.

Aidha Mhe. Ridhiwani amehimiza wananchi kuutumia mfumo huo katika kutoa maoni yao, akisisitiza kuwa maboresho hayo yanaenda sambamba na utengenezaji wa Aplikesheni itakayowezesha wananchi kutoa mrejesho wa haraka na wa uwazi ili kuimarisha uwajibikaji wa watumishi wa serikali.

POLISI YASISITIZA KILA MMOJA KUWAJIBIKA KULINDA AMANI NCHINI

12/13/2025 07:01:00 am

Jeshi la Polisi nchini Tanzania limetoa wito kwa Kila Mwananchi kuendelea kutii sheria sambamba na kushirikiana na kila mmoja kwa nafasi yake katika kulinda na kuimarisha amani, hasa kwa kuzingatia umuhimu wa amani katika maisha na shughuli za kila siku za kijamii na kiuchumi.

Polisi pia kupitia kwa Msemaji wake David Misime, limesisitiza kuendelea kuelimishana na kuhimizana katika kuyakataa yale yote yanayohamasishwa kwa njia mbalimbali ili kuwachonganisha na kuwajengea chuki Watanzania, lengo likiwa ni kuwaingiza Watanzania katika vurugu ambazo mara zote zimekuwa si nzuri kulingana na kile kinachoshuhudiwa kwenye Mataifa mengine duniani.

"Jeshi la Polisi pia kwa kushirikiana na Vyombo vingine vya ulinzi na usalama vinaendelea kuwaahidi kuwa tutaendelea kulinda usalama wa nchi yetu sote, maisha na mali za kila mmoja ndani ya Taifa letu la Tanzania." Amesema Msemaji huyo wa Jeshi la Polisi Tanzania Naibu Kamishna wa Polisi DCP David Misime.

Katika hatua nyingine, Polisi imeeleza kuwa nchi bado ni salama na shughuli za kiuchumi na za kijamii zinaendelea vyema katika kipindi cha saa 24 zilizopita, likishukuru pia kwa ushirikiano wanaoendelea kuupata kutoka kwa wananchi wa Tanzania.

Thursday, 11 December 2025

MARIDHIANO YATATUPA AMANI YA KUDUMU- WANANCHI

12/11/2025 11:03:00 pm

Watanzania wamehimiza utayari wa Jamii na makundi mbalimbali kushiriki katika mchakato wa maridhiano, wakisisitiza kuwa maridhiano ni silaha muhimu ya utatuzi wa migogoro mbalimbali inayotokea katika jamii kwani maridhiano ndiyo kitovu cha upatanishi kwa Taifa.

Wito huo umetolewa kufuatia kauli zilizotolewa mara kadhaa na Rais Samia Suluhu Hassan, aliyesisitiza kuongoza mchakato wa maridhiano ya Kitaifa ili kuwa na mwelekeo wa pamoja kama Taifa na zaidi katika mchakato wa upatikanaji wa Katiba mpya ya Tanzania.

Baadhi ya wananchi hao akiwemo Bw. Ridhiwan Hamidu Muhimu na Mansour Bakari, wakazi wa Ilala Jijini Dar Es Salaam wamezungumza nasi na kusisitiza kuwa chuki na magomvi si utamaduni wa Watanzania na maridhiano yatamfanya kila mmoja kupata kile anachostahili.

"Maridhiano yatapelekea kila mmoja kupata kile anachokistahili. Bila ya mazungumzo hatutoweza kufikia kwenye hali nzuri, bila ya maridhiano hatutakuwa na amani ya kudumu nchini." Amesisitiza Bw. Ridhiwan.

Bw. Bakari pia amezungumzia kuhusu ghasia za Oktoba 29, 2025 akisema maandamano haramu hayawezi kusaidia katika utatuzi wa changamoto na badala yake huzaa athari nyingi zaidi ambazo zimekuwa zikiwaathiri wananchi wa kawaida badala ya kuleta jawabu kwenye changamoto.

POLISI YAWATAKA WATANZANIA KUJIEPUSHA CHUKI NA UCHONGANISHI

12/11/2025 03:17:00 pm

Jeshi la Polisi nchini Tanzania limewataka Wananchi kuendelea kuwakataa na kuyakataa yale yote yenye mwelekeo wa kichonganishi, uzushi, uongo, yenye kujenga chuki pamoja na yenye kuhamasisha kufanya vurugu na matukio yote yenye viashiria vya kuvunja sheria za nchi.

Taarifa kwa Vyombo vya habari iliyotolewa mapema leo Alhamisi Disemba 11, 2025 na Msemaji wa Jeshi la Polisi, Naibu Kamishna wa Polisi David Misime imesisitiza pia kutosambaza ujumbe wenye kuleta chuki na uchochezi kwa jamii na badala yake kufuta ujumbe wa namna hiyo kwenye Mitandao ya kijamii ikiwemo WhatsApp.

"Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na   usalama vina wahakikishia kuwa vitaendelea kulinda amani na usalama wa nchi pamoja na maisha na mali zenu na tuendelee kutoa wito wa kuzingatia kanuni za kiusalama zinazotakiwa zianze na kila mmoja wetu kwanza sambamba na sisi sote kutii sheria." Imesema taarifa hiyo.

Katika hatua nyingine Polisi imeeleza kuwa kila mmoja aendelee kufanya shughuli zake halali bila hofu kutokana na usalama kuendelea kuimarika kote nchini Tanzania kutokana na ushirikiano mkubwa unaoendelea kutolewa kwa Vyombo vya ulinzi na usalama katika kulinda  na kuimarisha amani, utulivu na usalama nchini Tanzania.

Wednesday, 10 December 2025

RC MAKALLA AWAPONGEZA WANANCHI KWA KUYAKATAA MAANDAMANO YA DISEMBA 09

12/10/2025 04:55:00 pm

 *_Awahamasisha wananchi kujikita kwenye shughuli za kiuchumi_* 

 *_Awataka kujenga utamaduni wa kudumu wa kulinda amani na kuyakataa maandamano_* 

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla leo Jumatano Disemba 10, 2025, amewapongeza wananchi kwa kuyakataa maandamano ya Disemba 09, 2025, akiwataka kujenga utamaduni wa kudumu wa kukataa maandamano na matukio yote yenye viashiria vya uvunjifu wa amani Mkoani Arusha.

Mhe. Makalla amebainisha hayo wakati wa ziara yake ya kukagua shughuli za kibiashara  kwenye soko la Kilombero Jijini Arusha, akiahidi kuwa serikali na Vyombo vya ulinzi na usalama Mkoani Arusha vitaendelea kuhakikisha usalama na amani inakuwepo.

"Dunia imeona na watanzania wameithibitishia dunia ya kwamba wakiamua kulinda amani wanailinda, wasiotutakia mema jana wameaibika. Watanzania wanapenda amani na hawajazoea mambo ya maandamano na uvunjifu wa amani na wale wote waliokuwa wanataka vurugu leo wamejifungua- wana maumivu kwani hawakufanikiwa." Amesema Mhe. Makalla.

Mhe. Makalla kadhalika kando ya kuwahakikishia wananchi ulinzi na usalama muda wote, amehimiza pia umuhimu wa wananchi kujikita katika shughuli zao za kiuchumi na kijamii, akionya na kutangaza utimamu wa Vyombo vya ulinzi na usalama katika kukabiliana na wote wanaopanga kufanya vitendo vya uhalifu na uvunjifu wa amani katika Mkoa wa Arusha.

POLISI YAONYA WANAOENDELEA KUHAMASISHA MAANDAMANO

12/10/2025 09:22:00 am
POLISI YAONYA WANAOENDELEA KUHAMASISHA MAANDAMANO

Jeshi la Polisi nchini Tanzania kwa kushirikiana na Vyombo vingine vya ulinzi na usalama nchini wamewahakikishia wananchi kuwa wataendelea kulinda usalama wa Tanzania sambamba na maisha na mali za wananchi ili waweze kuendelea na shughuli zao kwa amani, utulivu na usalama.

Taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Jeshi la Polisi Makao Makuu, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) David Misime leo Disemba 10, 2025, limeonya pia kuhusu wanaopanga kujitokeza leo kwenye Mitaa mbalimbali ili kufanya kile kinachoitwa maandamano ya amani kutokana na kushindwa kuyafanya jana Oktoba 29, 2025.

"Jeshi la Polisi linaendelea kuwakumbusha, kuwasisitiza na kuwaonya wasifanye hivyo kwani wanachokiita maandamano ya amani yasiyo na kikomo yalipigwa marufuku kutokana na kukosa sifa kulingana na matakwa ya Katiba na sheria ya Polisi na Polisi wasaidizi sura 322." Amesema Misime.

Polisi pia imeeleza kuwa kwa ambaye atakaidi kutii sheria za nchi kwa lengo la kuhatarisha usalama wa nchi ili kusimamisha shughuli za kiuchumi na kijamii zisiendelee,  watadhibitiwa ili nchi ibaki salama na watanzania wema na wapenda amani wabaki salama.

Aidha Taarifa ya Polisi imetoa wito pia kwa wananchi kuendelea kufanya shughuli zao na kufuata maelekezo watakayokuwa wanapewa na Vyombo vya ulinzi na usalama katika maeneo yote nchini sambamba na kutii sheria za nchi ili taifa liendelee kuwa salama na kila mmoja kuweza kuendelea na shughuli zake.

Tuesday, 9 December 2025

TUNAIMARISHA ZAIDI ULINZI NA USALAMA USIKU HUU- POLISI

12/09/2025 10:42:00 pm
TUNAIMARISHA ZAIDI ULINZI NA USALAMA USIKU HUU- POLISI

Jeshi la Polisi nchini Tanzania limetoa taarifa yake kwa Vyombo vya habari kuhusu hali ya usalama nchini kwa kipindi cha saa sita tangu ilipotoka taarifa ya awali majira ya saa 6 mchana leo Jumanne Disemba 09, 2025.

Kulingana na Msemaji wa Polisi, Makao Makuu Dodoma, David Misime amesema hali ya usalama nchini imeendelea kuwa shwari na Vyombo vya Ulinzi na Usalama vimeendelea kuimarisha usalama nchini, pamoja na kulinda raia na mali zao hadi muda huu wa jioni.

"Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Vyombo vingine vya ulinzi na usalama vingependa kuwahakikishia kuwa kuanzia majira haya vitaimarisha zaidi ulinzi na usalama tunapoelekea usiku ili kuzuia na kudhibiti vitendo vyovyote vinavyoweza kuwa ni tishio la kiusalama." Amesema Kamanda Misime.

Katika hatua nyingine, Jeshi la Polisi limetoa wito kwa kila mwananchi kuendelea kuzingatia kanuni za kiusalama na kuendelea kutii sheria za nchi kwani kila mmoja anahitaji kuwa salama wakati wote.

JESHI LA POLISI LAKANUSHA TAARIFA ZA UPOTOSHAJI MTANDAONI, LATHIBITISHA USALAMA NCHINI KUWA SHWARI

12/09/2025 02:29:00 pm


Na Mwandishi wetu, Dodoma

Jeshi la Polisi nchini limekanusha taarifa zinazoenezwa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu kuwepo kwa maandamano leo Desemba 9, 2025, na kusisitiza kuwa hadi majira ya mchana hali ya usalama nchini kote ni shwari.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Jeshi la Polisi, Makao Makuu ya Polisi Dodoma,David Misime vyombo vya ulinzi na usalama vinaendelea kuimarisha ulinzi na kulinda maisha ya wananchi pamoja na mali zao kama ilivyo jukumu lao la msingi.

Polisi imeeleza kuwa picha na video zinazosambazwa mitandaoni zikidaiwa kuonyesha maandamano yanayoendelea leo si sahihi, bali ni matukio ya zamani na kwamba baadhi ya picha hizo zinatoka katika matukio ya Oktoba 29, 30 na 31 mwaka 2025, huku zingine zikitoka miaka ya nyuma ikiwemo tukio la Juni mwaka huu ambalo lilihusisha sherehe za jando za jamii ya Wamaasai zilizofanyika katika msitu wa TANAPA jijini Arusha.

Jeshi hilo limekumbusha kuwa maandamano yaliyokuwa yanatajwa kama “maandamano ya amani” yalipigwa marufuku tangu Desemba 5, 2025, baada ya kubainika hayakukidhi matakwa ya kisheria ikiwemo Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 na Sheria ya Polisi na Polisi Wasaidizi, Sura ya 322.

Aidha, Polisi imetoa wito kwa wananchi kuendelea kufuata sheria za nchi na kupuuza taarifa za upotoshaji, kwa manufaa ya amani na usalama wa Taifa.

WAFUNGWA 1,036 WAPATA MSAMAHA WA RAIS SAMIA

12/09/2025 11:44:00 am

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan leo Disemba 09, 2025, Tanzania ikiadhimisha miaka 64 ya uhuru wa Tanzania bara, ametangaza kuwasamehe wafungwa 1,036, wafungwa 22 kati yao wakiachiliwa huru na wengine 1,014 wakipunguziwa adhabu zao.

Kulingana na taarifa iliyosainiwa na Waziri wa mambo ya ndani ya nchi Mhe. George Simbachawene, Ikulu imeeleza kuwa ni matarajio ya serikali kuwa wafungwa walioachiwa huru watarejea tena katika jamii kushirikiana na wananchi katika ujenzi wa Taifa na kujiepusha kutenda makosa ili wasirejee tena gerezani.

Miongoni mwa waliosamehewa  ni wafungwa wagonjwa wenye magonjwa ya kudumu au sugu ambao wapo katika hatua za mwisho pamoja na wafungwa wazee wenye umri wa miaka 70 au zaidi- Vyote vikitakiwa kuthibitishwa na jopo la waganga wa Wilaya na Mikoa.

Aidha wengine walionufaika na msamaha huo ni wafungwa wa kike walioingia na ujauzito gerezani au wenye watoto wanaonyonya au wasionyonya waliohukumiwa kifungo cha mwaka mmoja na kuendelea pamoja na wafungwa wenye ulemavu wa mwili na akili wasio na uwezo wa kufanya kazi.

Aidha wamesamehewa pia wafungwa waliohukumiwa adhabu ya kuwekwa kizuizini (under president's pleasure) ambao wamekaa gerezani kuanzia miaka kumi au zaidi
Adbox