DOREEN BLOG

HABARI, MICHEZO NA BURUDANI

Adbox

Wednesday, 3 September 2025

KATIBU MKUU CHAMA CHA MADEREVA WA SERIKALI (CMST)NYABANGE ATUMA PONGEZI KWA RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN

9/03/2025 11:35:00 am
Doreen Aloyce ,Dodoma
 
 Katibu Mkuu wa Chama Cha. madereva wa Serikali (CMST,) Castro Nyabange amesema kuwa chama chicho kinampongeza kwa dhati Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa hatua mbalimbali za kuboresha maslahi ya watumishi wa umma wakiwemo madereva.

Ameyasema hayo jijini Dodoma wakati wa  Mkutano wa Chama cha Madereva wa Serikali Tanzania (CMST), uliofunguliwa na Waziri mkuu Kassim Majaliwa .

Nyambage amesema kuwa chama kinatambua mchango wa Serikali 
 Amesema chama hicho kimekuwa nguzo muhimu katika kuboresha huduma za udereva Serikalini na kuchangia maendeleo ya Taifa kwa ujumla.

“Upandishaji wa mishahara kwa watumishi umetugusa pia sisi madereva, awali sisi madereva wa Serikali tulikuwa na mishahara ya viwango vya chini sana, tunaahidi kufanya kazi bega kwa bega na Serikali kwa kuzingatia weledi katika utendaji.”
 


Aidha amesema chama kinajivunia kuanzishwa ofsi mbili Dodoma na Zanzibar licha ya changamoto zinazo wakabili ikiwemo ukosefu wa fedha za kuendesha shughuli zao pamoja na waajiri kutowa ruhusu madereva kuhudhuria vikao mbalimbali.

Kwa upande wake, Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega amesema madereva ni mhimili muhimu katika utekelezaji wa majukumu ya kila siku ya Serikali na nidhamu na uadilifu ndio msingi wa heshima wa kada hiyo.



“Sisi Serikali tutahakikisha ustawi wa madereva unakuwa kipaumbele chetu, wao wakiishi vizuri maana yake ni kwamba watafanya kazi zao kwa ufanisi mkubwa.”
 
Waziri Ulega amesema lengo la mkutano huo ni kujadili changamoto na kubadilisha uzoefu na kuimarisha mshikamano.

Awali akifungua mkutano huo Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema kuwa madereva wa Serikali wanawajibu wa kufanya kazi kwa weledi na nidhamu ya hali ya juu ikiwemo ukaguzi wa gari kabla na baada ya safari, kujaza na kutunza kikamilifu taarifa za safari na matengenezo.

Amewataka madereva na wasimamizi wahakikishe usalama wa vyombo vya usafiri, abiria, mizigo na nyaraka za Serikali pamoja na kutumia vifaa vya kisasa vya usalama, na kujiepusha na tabia zinazoweza kuhatarisha maisha, mali na siri za Serikali.

Pia, Waziri Mkuu amewahakikishia madereva hao kuwa Serikali inaendelea kufanyia kazi changamoto mbalimbali zinazowakabili madereva ili kuendelea kuimarisha mazingira ya kazi na ustawi wa madereva wa Serikali kote nchini.
 


“Changamoto mlizowasilisha ni mwendelezo wa kazi kubwa iliyopo mbele yetu, na kwa ushirikiano kati ya Serikali, Waajiri na Chama cha Madereva, tutaendelea kusonga mbele kwa hatua madhubuti ili kuboresha kada hii muhimu kwa manufaa ya Taifa letu.”
 
Pia, Waziri Mkuu amewataka waajiri wahakikishe stahiki za madereva zinalipwa kwa wakati, mafunzo ya mara kwa mara yanafanyika, miundo ya ajira inatekelezwa ipasavyo na wanapewa kipaumbele katika motisha mbalimbali.



Mkutanao huo wenye kaulimbiu isemayo “Dereva wa Serikali, Epuka Ajali, Linda Gari Lako na Watumiaji Wengine wa Barabara na Oktoba Shiriki Uchaguzi Mkuu”.
 umehudhuriwa na madereva wa Serikali zaidi ya 2,500 kutoka Tanzania Bara na Zanzibar.

Mwisho.

Thursday, 28 August 2025

MKURUGENZI WA ( INEC ) AONDOA FOMU ZA UTEUZI ZA WAGOMBEA KITI CHA RAIS KWENYE UBAO WA MATANGAZO AGOST 28, 2025

8/28/2025 07:23:00 pm
MWANDISHI WETU, DODOMA

 Tume Huru ya Taifa ya chaguzi(INEC)Imeondoa fomu za uteuzi wa wagombea wa kiti cha Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania katika ubao wa matangazo wa Tume ikiwa zimepita saa 24 za kubandikwa fomu hizo ikiwa ni utekelezaji wa masharti ya sheria.

MKURUGENZI wa (INEC) 
Ramadhani Kailima ameondoa fomu hizo jijini Dodoma  Agosti 28 mwaka huu 2025 .

Kailima akiongozana na watumishi wa Tume ,ambapo Fomu hizo za wagombea wa kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zilibandikwa ili kutoa fursa ya kuweka pingamizi dhidi ya uteuzi wa mgombea wa kiti cha Rais na Makamu wa Rais ambapo pingamizi hilo linaweza kuwekwa na mgombea mwingine, Msajili wa Vyama vya Siasa au Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Fomu hizo zilibandikwa na Tume Saa 10:00 jioni ya Agosti 27, 2025 ambayo ilikuwa ni siku ya uteuzi na kuondolewa leo Agosti 28, 2025 Saa 10: 00 jioni.



Wednesday, 27 August 2025

BALOZI DKT, ASHA ROSE MIGIRO APOKELEWA RASMI MAKAO MAKUU CCM,AAHIDI USHINDI KUTEKELEZA ILANI YA CHAMA

8/27/2025 01:25:00 pm

Na Sebastian Mavyeo, Dodoma

 ‎Katibu mkuu wa chama cha mapinduzi CCM Dkt.Asha Rose Migiro ameishukuru kamati kuu ya CCM Taifa kwa kumteua kuwa mrithi wa Dkt.Emanuel Nchimbi katika nafasi hiyo huku akiahidi  kutekeleza ilani ya chama hicho.

Dkt.Migiro ameyasema hayo leo Agosti 26,2025 wakati alipopokelewa katika ofisi za makao makuu ya chama hicho jijini hapa Dodoma na aliyekuwa katibu mkuu CCM Taifa Dkt.Emanuel Nchimbi ambaye kwa sasa atakuwa mgombea mwenza wa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29.2025.‎‎

Amesema kuteuliwa kwake kumetokana na ushirikiano mkubwa aliyopewa na wanachama wa CCM kipindi alipokuwa  kiongozi wa chama hicho katika   nyadhifa mbalimbali.


‎‎"Nishukuru kamati ya Halmashauri kuu ya CCM kwa kukubali mimi niwe mrithi wa Dkt.Nchimbi,Dkt.Nchimbi ana uzoefu mkubwa ndani ya CCM ameingia akiwa mdogo hadi sasa, hivyo naamini uwezo wake ni mkubwa ndani ya chama.‎‎

"Wanachama wa CCM ndio mtaji na raslimali zetu,kwa upande wangu kuwa katibu mkuu wa CCM ni kutokana na nyie kunipa ushirikiano katika kazi mbalimbali nilizozifanya ndani ya chama hiki hivyo tutahakikisha wagombea wetu wote wanapata ushindi mnono katika uchaguzi mkuu,"amesema Dkt.Migiro.

‎‎Awali aliyekuwa katibu mkuu wa CCM Taifa Dkt.Emanuel Nchimbi amemshukuru mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kumteua kuwa katibu mkuu wa chama hicho kwa kipindi chote alichoongoza . 

huku akiwashukuru wanachama wa CCM kwa ushirikiano waliyompatia kipindi cha uongozi wake.‎‎"kwanza wana CCM  wa Dodoma ni wakarimu sana na watakuonesha ushirikiano,tunaipongeza halmashauri kuu ya CCM kwa kukuteua wewe ,tunavishukuru vikao vya CCM kwa kuona uzito wa nafasi hii na kumteua mtu anayesitahili pia nimshukuru mwenyekiti wa CCM  kwa nafasi aliyonipa kipindi chote pamoja na wana ccm kwa ushirikiano mlionionesha,"amesema Dkt.Nchimbi.‎

Mwish

Saturday, 23 August 2025

RC. MKOA WA ARUSHA KENAN KIHONGOS ACHUKUA KITI CHA AMOS MAKALLA .

8/23/2025 10:20:00 pm

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mh. Kenan Kihongos ametangazwa rasmi kuwa Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo chama cha mapinduzi (CCM).

Akizungumza na vyombo vya Habari makao makuu ya chama cha mapinduzi CCM mara baada ya kutangaza majina ya wagombea ubunge kupitia chama cha mapinduzi CCM, Aliyekuwa katibu wa Itikadi,uenezi na mafunzo Ccm Amos Makala amesema kuwa kuanzia sasa Mh.Kenan Kihongos anachukua nafasi hiyo.



MH.AESHI HILALY ATANGAZWA RASMI KUGOMBEA UBUNGE JIMBO LA SUMBAWANGA MJINI

8/23/2025 09:32:00 pm




Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Sumbawanga Mjini Aeshi Hilaly ametangwa rasmi kugombea Ubunge akitetea nafasi yake . 

Mh.Aeshi amekuwa kiongozi bora katika kutetea maslah ya wananchi na Taifa kwa ujumla. 

Aeshi amekiwa hodari kuchangia  hoja mbalimbali Bungeni za kuleta maendeleo ndani ya Jimbo lake. 


Friday, 22 August 2025

TBN Yajumuika na Viongozi wa Habari Kuelekea Uchaguzi 2025

8/22/2025 12:12:00 pm


IMG-20250821-WA0061
Dar es Salaam, Agosti 21, 2025: 

WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Profesa Paramagamba Kabudi, ametaja majukumu makuu matano ambayo sekta ya habari nchini inapaswa kuyatekeleza kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025, akisisitiza umuhimu wa taaluma, weledi na maadili katika kuripoti.

Akizungumza kwenye Mkutano wa Wadau wa Sekta ya Habari na Utangazaji Kanda ya Mashariki uliofanyika jijini Dar es Salaam, Profesa Kabudi alisema vyombo vya habari ni mhimili muhimu katika kukuza demokrasia na kulinda amani wakati wa uchaguzi.

“Vyombo vya habari vinapaswa kuhakikisha wananchi wanajua haki na wajibu wao, kutoa elimu juu ya sera za wagombea, kufuatilia ukiukwaji wa sheria za uchaguzi, kuhamasisha ushiriki wa makundi maalum kama vijana na wanawake, na kupambana na taarifa potofu badala ya kuzisambaza,” alisema Profesa Kabudi.

IMG-20250821-WA0057
IMG-20250821-WA0059

Aidha, alisisitiza kuwa utekelezaji wa majukumu hayo lazima uongozwe na misingi ya taaluma na maadili ya uandishi wa habari ili kulinda heshima ya tasnia na kuepusha vurugu au uvunjifu wa amani.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari, Wakili Patrick Kipangula, alikumbusha waandishi wa habari kuhakikisha wanakuwa na ithibati kabla ya kufanya kazi za kihabari, hususan katika kuripoti uchaguzi.
IMG-20250821-WA0028
IMG-20250821-WA0031
IMG-20250821-WA0030

“Kifungu cha 19 cha Sheria ya Huduma za Habari kinasema bayana kuwa mtu yoyote anayetaka kufanya kazi ya uandishi ni lazima awe amepewa ithibati na Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari. Hivyo ni kosa la jinai kwa mwandishi wa habari kufanya kazi bila ithibati,” alisema Kipangula.

Aliongeza kuwa uhalali wa waandishi wa habari katika kipindi hiki ni jambo lisiloweza kupuuzia, kwani tasnia hiyo inahusisha majukumu makubwa yanayoathiri utulivu wa taifa.
IMG-20250821-WA0046(1)
Mkutano huo uliwahusisha wadau mbalimbali wa sekta ya habari na utangazaji, ambao walijadili nafasi ya vyombo vya habari katika kulinda maadili ya kitaifa na kuhakikisha wananchi wanapata taarifa sahihi kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025.
IMG-20250821-WA0058
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Profesa Palamagamba Mwaluko Kabudi (wa nne kutoka kushoto waliokaa), akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi na wadau wa sekta ya habari na utangazaji baada ya kufungua Mkutano wa Wadau wa Habari na Utangazaji Kanda ya Mashariki uliofanyika jijini Dar es Salaam. Waliokaa kutoka kulia ni Meneja wa Huduma za Utangazaji wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Mhandisi Andrew Kisaka, Kaimu Mkurugenzi wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari Patrick Kipangula, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Rodney Mbuya, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Gerson Msigwa, pamoja na Kamishna na Msemaji wa Jeshi la Polisi, DCP David Misime pamoja na Mjumbe wa Kamati ya Amani ya Mkoa wa Dar es Salaam. 

Waliosimama nyuma ni viongozi wa Mtandao wa Wanablogu Tanzania (TBN) akiwemo Muhidin Issa Michuzi (Mdhamini), Mwenyekiti wa TBN Beda Msimbe, Mjumbe Joachim Mushi na Mweka Hazina ambaye pia ni Mtaalamu wa Habari, Cathbert Kajuna.

Thursday, 21 August 2025

MWENYEKITI WA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AONGOZA KIKAO CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUUYA CCM DODOMA

8/21/2025 01:46:00 pm

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiongoza Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa,kilichoketi leo Agosti 21,2025 Jijini Dodoma kwa ajili ya kufanya uteuzi  wa Wagombea  Ubunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Wabunge wa Viti Maalum,Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Viti Maalum.



Monday, 4 August 2025

MWENGE WA UHURU WAKAGUA MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 4.3 WILAYA YA NZEGA

8/04/2025 09:19:00 pm

Na Lucas Raphael,Tabora

MWENGE wa Uhuru umezindua miradi 6 ya maendeleo yenye thamani ya zaidi ya Shilingi bilioni 4.3 katika Halmashauri ya mbili ya wilaya ya nzega ambazo ni nzega vijijini na nzega mjini zote zipo mkoani i Tabora.

Akizungumza kwa nyakati tofauti akiwa katika eneo la miradi hiyo jana Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka huu Ismail Al Usi alionesha kuridhishwa na kazi nzuri iliyofanyika ikiwemo ubora wa miradi hiyo.


Alibainisha kuwa miradi hiyo iliyopo katika sekta ya elimu, afya, huduma za utawala, uwezeshaji wananchi kiuchumi na miundombinu ya barabara imeakisi dhamira ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ya kuboresha maisha ya wananchi.

Awali akipikea mwenge huo mkuu wa wilaya ya nzega , ndani ya Halmashauri ya Mji wa Nzega,  Naitapwaki  Tukai alisema kuwa  dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutumia Mwenge wa Uhuru kama chombo muhimu cha kuhamasisha maendeleo, mshikamano wa kitaifa na ushiriki wa wananchi katika miradi ya kijamii na kiuchumi.

Katika halmashauri ya wilaya ya Nzega Mwenge wa Uhuru utakimbizwa katika Halmashauri mbili za Nzega Mji na Nzega kwa umbali wa kilomita 117.2 ukianza na Halmashauri ya Mji wa Nzega kwa kupitia jumla ya miradi sita ya maendeleo inayogharimu shilingi bilioni 2.3, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa ajenda ya kuwaletea wananchi maendeleo endelevu.

Miradi hiyo ilijumuisha ujenzi wa kituo cha mafuta cha Nyarubanda Oil kilichogharimu shilingi bilioni 1.092, ujenzi wa zahanati ya Ipilili uliogharimu shilingi milioni 103, pamoja na ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa, ofisi ya walimu na matundu sita ya vyoo kwa gharama ya shilingi milioni 92.
Aidha alisema kwamba  miradi mingine ni wa kikundi cha vijana wajasiriamali cha Constrafrica waliopatiwa fedha asilimia 10 kiasi cha  shilingi milioni 19.
Pia mwenge huo uliweka jiwe la msingi  mradi wa upanuzi wa mfuko wa kusafisha na kutibu maji Nzega unaotekelezwa kwa shilingi milioni 620 na mradi wa ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kutoka Lumambo–Kitongo hadi FDC unaogharimu shilingi milioni 462.1.


Aidha, Mwenge wa Uhuru mwaka huu unabeba kaulimbiu isemayo: “Jitokeze Kushiriki Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 kwa Amani na Utulivu”, ikiwa ni wito kwa Watanzania wote kushiriki kikamilifu katika mchakato wa uchaguzi huku wakidumisha amani, mshikamano na utulivu wa kitaifa.

 mwisho

WANANCHI YATUMIENI MAONYESHO YA NANENANE KUJIFUNZA MBINU BORA ZA KILIMO - RC CHACHA

8/04/2025 09:14:00 pm
Na Lucas Raphael,Tabora

Mkuu wa mkoa wa Tabora ,Paulo Chacha amewataka wananchi Kuyatumia maonyesho ya nane nane kujifunza mbinu Bora za uzalishaji wa mazao ya Kilimo,Mifugo na uvuvi kupata maarifa sahihi zitakazowasaidia kufanya uzalishaji wenye tija ili waweze kujikwamua kiuchumi .

Kauli hiyo ilitolewa jana   wakati wa uzinduzi wa maonyesho ya nane nane kwa Kanda ya Magharibi yaliyofanyika katika viwanja vya Ipuli  mkoani Tabora.

Chacha alisema kwamba maonyesho hayo yalitumika vizuri yanaweza keta Tija kwa wakulima na kuweza kuongeza uzalishaji mkubwa.

"Wengi wetu tupo kwa lengo la kuona kujifunnza mbinu Bora , uzalishaji mazao ya Kilimo ,mifumgo na uvuvi ili kupata maarifa yatakayotusaidia kupiga hatua kwenye Mapinduzi ya kijani na hivyo kuinua Pato na uchumi kwa Kaya zetu na taifa kwa ujumla " alisema Chacha.

Kwa upande wake , Msajili wa Mamlaka ya Wanunuzi wa Mbegu kutoka Wizara ya Kilimo Twalib Njohole alibainisha lengo la maonyesho ya nane nane ni kutoa elimu na teknolojia bora ya kilimo ili kuongeza uhakika wa uzalishaji wa mazao.

Afisa Masoko wa Wakala wa Mbegu za kilimo (ASA) Okia John, aliwataka Wakulima kutumia Mbegu ambazo zimethibitishwa na mdhibiti ubora ili waweze kupata mavuno bora .

"Tuna mhakikishia Mkulima Mbegu ambayo tunampa hapa kwenye hili banda atakapofika ni Mbegu bora kwa sababu imethibitisha na mdhibiti ubora wa Mbegu" Okia alisisitiza

Maonyesho ya nane nane kwa Kanda ya magharibi yanafanyika kwenye viwanja vya Ipuli ambapo tamati yake itakuwa Agosti 8,2025 ambapo yatafungwa na Mkuu wa mkoa wa Kigoma Saimon Silo.

"maonyesho haya yamebebwa na kauli mbiu ya " _Chagua Viongozi Bora kwa Maendeleo Endelevu ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi"._

Mwisho

WAKAZI 8000 KUNUFAIKA NA MRADI WA MAJI KUTOA ZIWA VICTORIA

8/04/2025 09:10:00 pm
Na Lucas Raphael,Tabora

Mradi wa upanuzi wa majisafi ya Ziwa Victoria toka Makomero hadi Mgongoro utawanufaisha Zaidi ya wakazi 8000 wa vitongoji viwili na kijiji kimoja Wilayani Igunga mkoani Tabora.  
 
Akizungumza kabla ya kuzinduliwa mradi huo uliogharimu Shilingi 840 milioni ambao uliwekewa jiwe la msingi na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,mkurugenzi mtendaji wa Mamlaka ya majisafi na usafi wa mazingira mjini Igunga,Iguwasa,Alex Ntonge  alisema unawanufaisha wakazi ambao walikuwa wakihangaika kutafuta maji.
 


Alieleza kuwa wakazi wa maeneo hayo wamekuwa wakipata changamoto kubwa ya maji na kuwafanya watumie muda mqingi kuhangaikia maji.
 
Kwa sasa alisema adha waliyokuqa nayo wakazi hao imeisha kwani wanapata huduma ya majisafi na salama kupitia mradi huo.
 


Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2025,Ismail Ali Ussi,aliipongeza Iguwasa kwa kuhakikisha wakazi wake wanapata maji na kusema kuwa sekta ya maji inafanya kazi nzuri.
 
Alisema Rais Samia Suluhu Hassan amefanya kazi nzuri ya kuhakikisha fedha nyingi zaidi zinaenda sekta ya maji ambayo nayo haijamuangusha kwa kuwa na miradi yenye ubora.
 
Alieleza kuwa watumishi wa sekta hiyo wanafanyankazi nzuri sana na hawana budi kupongezwa kutokana na utendaji aao mzuri wa kazi.
 
Mkuu wa Wilaya ya Igunga,Sauda Mtondoo alisema kukamilika kwa mradi huo kunafanya wakazi wanaopata majisafi na salama mjini Igunga kufikia asilimia mia moja.
 
Mwisho.
 

WAZIRI Mkuu Mh. Kassim Majaliwa Asisitiza kuendelea kusimamiwa kwa Itifaki ya SADC dhidi ya Rushwa._*

8/04/2025 09:04:00 pm
Na Mwandishi wetu

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ametoa wito kwa Wakuu wa Taasisi za Kupambana na Rushwa  wa Jumuiya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) kuendelea kusimamia kikamilifu na kwa ufanisi utekelezaji wa Itifaki ya Jumuiya hiyo dhidi ya Rushwa ili kujenga ukanda usio na Rushwa.

Amesema kuwa Itifaki ya SADC Dhidi ya Rushwa bado ni nyenzo muhimu katika kufanikisha utawala bora, amani na muungano endelevu wa kikanda hivyo viongozi hao wanapaswa kuhakikisha kuwa juhudi za kupambana na rushwa zinaendelezwa.

Ametoa wito huo leo (Agosti 04, 2025) alipomuwakilisha Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye Ufunguzi wa Maadhimisho ya miaka 20 ya Utekelezaji wa Itifaki ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika Dhidi ya Rushwa, yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Gran Melia, jijini Arusha.

“Lazima tukiri kwamba rushwa ni tishio kwa usalama. Inachochea uhalifu uliopangwa, usafirishaji haramu wa binadamu, ugaidi, na kudhoofika kwa utawala wa sheria.”


Aidha, Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa katika kipindi cha hivi karibuni, nchi Wanachama wa SADC ikiwemo Tanzania zimeendelea kuimarisha sheria za mapambano dhidi ya rushwa, kuziwezesha Taasisi zinazosimamia udhibiti na mapambano dhidi ya rushwa pamoja na kutoa elimu kwa wananchi juu ya athari za rushwa kwa ustawi wa Taifa.

“Hata ushirikiano wa kikanda katika mapambano dhidi ya rushwa umeimarika kwa kubadilishana taarifa, mashirikiano katika masuala ya sheria pamoja na uchunguzi wa pamoja katika kushughulikia masuala ya rushwa ya kikanda”

Kadhalika Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa Tanzania kwa upande wake, inachukulia mapambano dhidi ya rushwa kama kipaumbele cha kitaifa na jambo la msingi kwa maendeleo Taifa na usalama wa Taifa.

“Njia iliyo mbele huenda ikawa ndefu, lakini tusiwaze kushindwa. Kwa ushirikiano endelevu, maono ya kimkakati, na utashi wa kisiasa, tunaweza na tunapaswa kujenga ukanda wa SADC usio na rushwa”

Mheshimiwa Majaliwa amewapongeza viongozi hao kwa kuendelea kusimamia mikakati mbalimbali ya kupiga vita rushwa ikiwemo kuanzishwa kwa mfumo imara ya ufuatiliaji, tathmini na utoaji wa taarifa SADC. Pamoja na Kielelezo cha Jitihada za Kikanda za Kupambana na Rushwa.

Kwa upande wake, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Stegomena Tax amesema kuwa Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, inaendelea  kusimama imara katika kuendeleza utawala bora na kuheshimu utawala wa sheria, ambayo ni nguzo kuu katika mapambano yao ya pamoja dhidi ya rushwa.

“Warsha hii, imekuja wakati muafaka, ikiwa ni jukwaa la kubadilishana uzoefu bora, kuimarisha ushirikiano, na kuoanisha juhudi zetu katika kupambana na rushwa kwa ufanisi zaidi katika ukanda huu.”

Naye, Mwenyekiti wa Kamati ya Kupambana na Rushwa ya SADC, ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Crispin Francis Chalamila amesema kuwa kupitia mikakati Miwili ya Kupambana na Rushwa ya (2018-2022) na (2023-2027), wamefanikiwa kuandaa mtaala wa Kikanda uliowekwa viwango vya uchunguzi na kinga dhidi ya rushwa, kuandaa Mfumo wa Ufuatiliaji na Tathmini wa Kikanda wa Kupambana na Rushwa pamoja na Kuandaliwa kwa Tathmini ya Kikanda ya Mapambano Dhidi ya Rushwa.
Mwisho. 
Adbox