DOREEN BLOG

HABARI, MICHEZO NA BURUDANI

Adbox

Monday, 22 December 2025

POLISI YAJIIMARISHA KULINDA RAIA MSIMU HUU WA KRISMASI NA MWAKA MPYA

12/22/2025 07:43:00 pm

Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, (DCP) David Misime, amesema Jeshi hilo kwa kushirikiana na Vyombo vingine vya ulinzi na usalama vitaendelea kuimarisha ulinzi na usalama wakati na baada ya sikukuu za Krismasi na Mwaka mpya, wito ukitolewa kwa kila mwananchi kutambua na kuheshimu thamani na umuhimu wa amani na usalama kwa kila mmoja.

Taarifa iliyotolewa leo Jumatatu Disemba 22, 2025 na Jeshi la polisi imewataka pia wale wote watakaokuwa wakisafiri kutoka eneo moja kwenda jingine kuzingatia sheria za usalama barabarani kama sehemu ya kuepuka ajali za barabarani, wakikumbusha kuhusu kaulimbiu ya wiki ya nenda kwa usalama isemayo "endesha salama, familia inakusubiri."

"Maisha yetu na shughuli zetu wakati wa hizi sikukuu yanahitaji mazingira ya amani ili kila mmoha aweze kushiriki kwenye ibada za kumshukuru Mungu, kukaa na familia na marafiki bila ya bugudha yeyote ile hivyo tuilinde amani kwa ushirikiano na kwa nguvu zetu zote." Imesema taarifa hiyo.

"Aidha wito unatolewa kwa wananchi wote na kwa wote watakaokuwa nchini kuwa kinachohitajika ni kila mmoja wetu kutambua thamani na umuhimu wa amani na usalama, ni wakati muafaka pia kuendelea kuyakataa yale ambayo yana malengo ya kuvuruga amani kipindi hiki cha sikukuu na baada." Imeongeza kusema taarifa hiyo ya polisi.

Polisi pia imeeleza kuwa hali ya usalama nchini ni shwari licha ya matukio machache ya uvunjifu wa amani yaliyojitokeza, likisema hali hiyo imetokana na Watanzania kufahamu umuhimu wa kila mmoja kulinda na kuimarisha amani, utulivu na usalama kama nyenzo kuu ya kuwawezesha kushiriki katika shughuli za kijamii na kiuchumi.

Friday, 19 December 2025

KIKAO CHA KAMATI YA WATAALAM YA KITAIFA YA USIMAMIZI WA MAAFA CHAPITISHA MIONGOZO YA KUKABILIANA NA MAAFA NCHINI*

12/19/2025 09:49:00 pm

Na mwandishi wetu, Dodoma.

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Dkt. Jim Yonazi ameongoza Kikao cha Kamati ya Wataalam ya Kitaifa ya Usimamizi wa Maafa leo 19 Desemba,2025 kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano uliopo Ofisi ya Waziri Mkuu Ngome, Jijini Dodoma.

Katika kikao hicho, Mpango wa Taifa wa dharura wa  kukabiliana na Ukame, Mafuriko na Majanga mengine yanayohusiana kwa kipindi cha Novemba 2025 hadi Juni 2026 umejadiliwa na kupokelewa na wajumbe wa kikao.

Aidha, Miongozo ya uanzishwaji na Uendeshaji wa kituo cha operesheni na Mawasiliano ya dharura na Timu ya kukabiliana na Dharura ngazi ya Taifa na Mkoa imejadiliwa na kupitishwa na wajumbe wa kikao.

Miongozo iliyojadiliwa na kupitishwa ni pamoja na, Mwongozo wa Uanzishaji wa kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura, Mwongozo wa Uendeshaji wa kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura Ngazi za Mikoa, Mwongozo wa Uanzishaji na Uendeshaji wa Timu ya Mkoa ya kukabiliana na Dharura.

Pia, Muongozo wa Uanzishaji na Uendeshaji wa Timu ya Taifa ya kukabiliana na Dharura, Muongozo wa Uendeshaji wa Kituo cha Taifa cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura, Muongozo wa kuandaa Mpango wa Mkoa wa kujiandaa na kukabiliana na Maafa.

Pamoja na hayo, Wajumbe wa kikao hicho walipokea na kuridhia Mkakati wa Utekelezaji wa Mpango wa Utoaji wa Huduma za Tahadhari ya mapema kwa wote kwa kipindi cha miaka Mitano (2026-2030).

Awali, Dkt Yonaz ametoa Pongezi kwa Taasisi na Sekta mbalimbali zinazokabiliana na Maafa kwa kuendelea kufanya vizuri na kutoa Elimu ya maafa Nchini na Nchi Jirani.

=MWISHO=

Dkt,MWIGULU AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MADARAJA LINDI.*

12/19/2025 07:25:00 pm

_Asisitiza Rais Dkt. Samia amedhamiria kushughulika kwa vitendo na umasikini wa watanzania_

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Desemba 19, 2025 amekagua maendeleo ya ujenzi wa Madaraja na Ukarabati wa barabara kuu ya Marendego-Nangurukuru-Lindi-Mingoyo

Akizungumza baada ya ukaguzi huo, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amewaambia wakazi wa Somanga mkoani Lindi kuwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anatekeleza miradi ya kimkakati ili kushughulika kwa vitendo na umasikini wa Watanzania

Amesema kuwa Rais Dkt. Samia alisimamia ukamilishaji wa Bwawa la Kuzalisha Umeme la Julius Nyerere ili kuhakikisha kila mtanzania ananufaika na huduma ya nishati ya umeme. 

“Tumeshuhudia Rais Dkt. Samia namna anavyotekeleza miradi kwenye sekta mbalimbali ikiwemo uvuvi, maji, kilimo, afya, elimu na hata uwezeshaji wananchi kiuchumi”

TARURA YAPEWA TUZO KUTAMBUA MCHANGO WAKE KATIKA SEKTA YA UCHUKUZI

12/19/2025 06:46:00 pm

Arusha

Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) imepewa tuzo ya  kutambua mchango wake katika maendeleo ya sekta ya uchukuzi nchini. 

Tuzo hiyo imekabidhiwa na Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mhe. Joseph Mkude akimwakilisha Waziri wa Uchukuzi na kupokelewa na Mkurugenzi wa Mipango ya Miundombinu, Mhandisi Edward Amboka.

Tuzo hiyo imetolewa katika Mkutano wa 18 wa Tathmini ya Utendaji wa Sekta ya Uchukuzi uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa (AICC) jijini Arusha.

TARURA imeshiriki Mkutano huo ikiwa ni mdau wa sekta ya uchukuzi, ambapo ilitumia Mkutano huo kwa kuwasilisha utekelezaji wa shughuli za Wakala kwa mwaka wa fedha 2024/2025 na kutoa elimu kwa wadau kuhusu majukumu na kazi mbalimbali zinazofanywa na Wakala.

Mpango wa Elimu kwa Umma Kuhusu Muungano utakuwa endelevu

12/19/2025 02:06:00 pm
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni amesema Mpango wa Elimu kwa Umma Kuhusu Muungano utakuwa endelevu ili kuhakikisha elimu hiyo inamfikia kila mmoja. 

Ameyasema hayo Desemba 19, 2025 wakati akizungumza katika kipindi cha Asubuhi Njema kinachorushwa na ZBC ambapo amesema Waandishi wa Habari wanayo nafasi kubwa katika utoaji wa elimu kwa umma ndio maana Ofisi ya Makamu wa Rais imewapa nafasi na itakuwa ikishirikiana nao kwa asilimia kubwa.

“Katika kuhakikisha hilo leo tumeandaa Semina ya Wahariri wa Vyombo vya Habari Zanzibar kisha tutaifanya kwa Wahariri Bara na baadaye tutaandaa makongamano mbalimbali.”
 
Amesema Mpango wa Elimu kwa Umma kuhusu Muungano,  wanufaika wakubwa watakuwa vijana ambao ndio walengwa kutokana na wengi wao kuwa wamezaliwa baada ya Muungano(1964).

Tuesday, 16 December 2025

Watanzania naomba tulinde Amani kwa maendeleo yetu Binafsi

12/16/2025 07:27:00 pm

Watanzania wamehfgimizwa kulinda na kuitunza miundombinu inayojengwa katika maeneo mbalimbali nchini ili iweze kudumu na kutumika kwa muda mrefu zaidi na kuwanufaisha zaidi, wakihimizwa pia kulinda amani kwa maslahi ya ustawi na maendeleo binafsi na ya Taifa kwa ujumla.

Wito huo umetolewa na Bi. Fatuma Ramadhan Mchekwa, Mkazi wa Temeke Jijini Dar Es Salaam wakati akizungumza na chombo chetu cha habari leo Jumanne Disemba 16, 2025, akisisitiza kuwa uharibifu wa Miundombinu umekuwa ukiligharimu taifa fedha nyingi.

"Tunachoomba sisi ni amani, amani iendelee na tusifanye fujo kwasababu tunapoharibu miundombinu ikiwemo ya mwendokasi hizi ni kodi zetu wenyewe kwahiyo tunajikomoa wenyewe. Tunafanya biashara  tunalipa ushuru na kodi zetu ndizo zinazoleta maendeleo ila leo badala ya kusema tuendelee kuleta maendeleo tunarudi kukarabati miundombinu iliyoharibiwa." Amesema Bi. Fatuma.

Katika hatua nyingine Bi. Fatuma amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa ujenzi wa miundombinu mbalimbali ikiwemo ujenzi wa barabara ya Mbagala- Kariakoo, ujenzi wa shule ya msingi Kidugulo pamoja na kufikisha umeme kwenye maeneo yote ya Chanika, suala ambalo limeboresha maisha ya wananchi kupitia sekta mbalimbali za kiuchumi na kijamii.L

Wafugaji Chanika waishukuru Serikali ujio wa miradi mikubwa ya ufugaji.

12/16/2025 04:31:00 pm

Wafugaji wa Kata ya Chanika, Wilayani Ilala Mkoani Dar Es Salaam wameishukuru serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan kwa mapinduzi na ujio wa miradi mikubwa ya ufugaji iliyowasaidia kujikwamua na umaskini na kuongeza kipato.

Kwaniaba ya wafugaji hao, Bw. Hamim Idrisa, Katibu wa Wafugaji Kata ya Chanika, ameeleza kuwa ipo miradi mitatu iliyozinduliwa katika Kata ya Chanika katika kipindi cha miaka minne ya awamu ya kwanza ya Rais Samia, ambayo imewaneemesha wafugaji ikiwemo mradi wa kuku wa Mayai na mradi wa kukabiliana na usugu wa madawa ya mifugo.

"Mradi wa kwanza ni ufugaji wa kuku bila dawa ambao umekuwa msaada mkubwa sana kwetu, upo pia mradi wa kukabiliana na usugu wa madawa dhidi ya vimelea vya magonjwa na mradi wa mwisho ni huu wa kuku wa mayai ambapo serikali inatupa nyenzo, madawa na elimu kupitia Maafisa tulionao kwenye Kata yetu." Amesema Bw. Idrisa.

Katika upande wa maendeleo ya Jamii na ustawi, Bw. Idrisa amezungumzia sekta ya afya, akiishukuru serikali kwa ujenzi wa Chumba cha kuhifadhia maiti kwenye Hospitali ya Nguvu Kazi pamoja na kuanza kwa mradi wa Zahanati ya Kidugilo, ambapo fedha na eneo la utekelezaji wa mradi huo imeshapatikana.

Monday, 15 December 2025

Chanika yapaa kimaendeleo miaka minne ya Rais Samia

12/15/2025 10:44:00 pm
CHANIKA WAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA UJENZI WA SHULE NA MOCHWARI

CHANIKA YAPAA KIMAENDELEO, MIAKA MINNE YA RAIS SAMIA

Wananchi wa Kata ya Chanika, Ilala Mkoani Dar Es Salaam wamemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa maboresho makubwa ya huduma za afya na elimu Wilayani humo, wakisisitiza umuhimu wa wazazi kuwaandikisha watoto wao katika msimu ujao wa masomo 2026, ili waweze kunufaika na uwekezaji mkubwa uliofanywa ndani ya Wilaya ya Temeke na Tanzania kwa ujumla.

Wananchi hao wameeleza namna ambavyo walilazimika kusafirisha miili ya wapendwa wao wanaofariki kwenda kuhifadhiwa Wilayani Kisarawe kutokana na kukosekana kwa Vyumba vya kuhifadhia maiti katika Kata yao ya Chanika kwenye Hospitali ya Nguvukazi.

Akizungumza na mwandishi wetu wa habari Bi. Jaliah Kabeya, Mkazi wa Chanika Jijini Dar Es Salaam amesema kwasasa katika sekta ya elimu na afya hakuna changamoto yoyote, akishukuru pia kwa ujenzi wa barabara za ndani ya Wilaya yao ikiwemo changamoto ya mafuriko Tazara suala ambalo lilikuwa likikwamisha shughuli za usafiri na usafirishaji ndani ya eneo hilo.

"Tunamshukuru Mungu na Mama Samia kwa hili, tumuombee dua ili aendeleze pale alipobakiza kwasababu yeye si malaika na hawezi kufanya yote kwa wakati mmoja na kwa haya aliyoyafanya pia ni muhimu kuwa na roho shukrani." Amesema Bi. Jaliah.

Mwananchi huyo pia ameshukuru kwa usimamizi wa mikopo ya Asilimia kumi ya Halmashauri inayotolewa kwa wanawake, Vijana na wenye ulemavu, akisema suala hilo limesaidia pakubwa kuwakwamua wananchi na umaskini, akisifu pia michakato yake na mikopo kuwa rahisi.

WAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUBORESHA HUDUMA ZA KIJAMII NCHINI

12/15/2025 10:37:00 pm


RAIS SAMIA AMETUONDOLEA UKATILI WA KIJINSIA NCHINI- BI. MAPUNDA0

WANAWAKE WAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUWAENZI NA KUWAPATIA MAHITAJI

Bi. Sikitiko Casian Mapunda, Mkazi wa Nguvu Mpya Jijini Dar Es Salaam amemtaja Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kama Kiongozi na Mama jasiri na shujaa, akimshukuru kwa kuwekeza katika masuala ya Kijamii ikiwemo yanayowahusu wanawake pamoja na watoto.

Bi. Mapunda amebainisha hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatatu Disemba 15, 2025, akisema huko nyuma baadhi ya Makundi yalisahaulika ikiwemo wanawake na Vijana, akisema ni mara ya kwanza kuona Rais akiwaita Vijana na kuwasikiliza kero na changamoto walizonazo.

"Nimshukuru pia sana Mama kwa namna alivyoifanya miundombinu ya GongolaMboto kupitika tofauti kabisa na zamani ilivyokuwa. Sasa hivi barabara ya Gongolamboto ni tofauti kabisa na ilivyokuwa miaka mitano iliyopita, ni kama barabara za Ulaya, tuna Mahospitali na mpaka barabara za ndani nazo zinapitika wakati wote." Amesema Bi. Mapunda.

Amemshukuru Rais Samia pia kuhusu usimamizi wake wa mikopo ya asilimia kumi inayotolewa na Halmashauri kwaajili ya wanawake, Vijana na wenye ulemavu, akimuomba pia kushughulikia masharti magumu ya upatikanaji wa mikopo hiyo.

Katika hatua nyingine Bi Mapunda pia akizungumza na mwandishi wetu wa habari, ameeleza na kushukuru kupungua kwa matukio ya ukatili wa kijinsia nchini ikiwemo matukio ya ubakaji kwa wasichana na wanawake, akisema huko nyuma kabla ya ujio wa Rais Samia udhalilishaji ulikuwa mkubwa na wanawake wengi wa Mijini na Vijijini walikuwa na hofu kubwa ya kupita katika baadhi ya maeneo kwa kuhofia matukio ya ubakaji yaliyokuwepo.

KIKUNDI CHA WAMANDA WAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA MAONO YAKE

12/15/2025 12:33:00 pm

Kikundi cha Akinamama wanaonufaika na Mikopo ya asilimia kumi ya Halmashauri cha Wamanda kilichopo Nzega Mkoani Tabora wamemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa usimamizi na maboresho makubwa ya mfumo wa Mikopo hiyo, wakisema imewasaidia kiuchumi na kuwaongezea kipato kwa asilimia kubwa.

Bi. Stellah William, Kwa niaba ya wanakikundi wenzake amesema kupitia kipato wanachokipata sasa kupitia kikundi hicho, ameweza kusomesha watoto, kuendesha maisha pamoja na kumpa ujasiri mkubwa wa kuweza kutafuta fedha na kujiendeleza kiuchumi.

"Kwakweli kikundi hiki kimeninufaisha kwenye kusomesha watoto na wajukuu wangu, naendelea pia kunufaika na mambo mengi sana na zaidi kimenifanya niwe jasiri wa kutafuta fedha nikiwa peke yangu."

Nimpongeze pia Mama Samia kwa kuwa na maono yake ya kuona kuwa hata Kijijini kuna watu wanahitaji msaada wake na nimuombe Mama Samia asituchoke, tunamuhitaji sana na atuangalie kwa macho yake yote sisi akinamama wa Vijijini." Amesisitiza Bi. Stellah William.

Saturday, 13 December 2025

E- MREJESHO KUKUZA UWAJIBIKAJI KWA WATUMISHI WA UMMA

12/13/2025 12:21:00 pm

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema Wizara hiyo imefanya maboresho mbalimbali ya mifumo yake ikiwemo mfumo wa e- mrejesho, ili kutoa fursa zaidi kwa wananchi wa pembezoni kutoa maoni, malalamiko na pongezi kuhusu huduma zinazotolewa na serikali na Taasisi zake.
Mhe. Ridhiwani amebainisha hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar Es Salaam, akisema mfumo huo unapatikana kwenye simu za mkononi kupitia nambari *152*00#, ukiwa na module ya sema na Kiongozi, sehemu inayomruhusu mwananchi kutoa maoni kwa Waziri, Mkuu wa Mkoa ama Kiongozi mwingine, akisema mfumo huo utakusanya maoni na kisha kuchakatwa na kufanyiwa kazi.

"Mfumo huu wa e- mrejesho ni kiunganishi cha moja kwa moja cha mwananchi na Kiongozi na hii itatusaidia pale tunapojadili namna ya kuboresha mifumo ya utumishi wa umma na ni mfumo wa kweli huu, hata kama kuna Kiongozi hatojibu sisi tutasimamia kuhakikisha majibu yanapatikana." Amesema Mhe. Ridhiwani.

Aidha Mhe. Ridhiwani amehimiza wananchi kuutumia mfumo huo katika kutoa maoni yao, akisisitiza kuwa maboresho hayo yanaenda sambamba na utengenezaji wa Aplikesheni itakayowezesha wananchi kutoa mrejesho wa haraka na wa uwazi ili kuimarisha uwajibikaji wa watumishi wa serikali.

POLISI YASISITIZA KILA MMOJA KUWAJIBIKA KULINDA AMANI NCHINI

12/13/2025 07:01:00 am

Jeshi la Polisi nchini Tanzania limetoa wito kwa Kila Mwananchi kuendelea kutii sheria sambamba na kushirikiana na kila mmoja kwa nafasi yake katika kulinda na kuimarisha amani, hasa kwa kuzingatia umuhimu wa amani katika maisha na shughuli za kila siku za kijamii na kiuchumi.

Polisi pia kupitia kwa Msemaji wake David Misime, limesisitiza kuendelea kuelimishana na kuhimizana katika kuyakataa yale yote yanayohamasishwa kwa njia mbalimbali ili kuwachonganisha na kuwajengea chuki Watanzania, lengo likiwa ni kuwaingiza Watanzania katika vurugu ambazo mara zote zimekuwa si nzuri kulingana na kile kinachoshuhudiwa kwenye Mataifa mengine duniani.

"Jeshi la Polisi pia kwa kushirikiana na Vyombo vingine vya ulinzi na usalama vinaendelea kuwaahidi kuwa tutaendelea kulinda usalama wa nchi yetu sote, maisha na mali za kila mmoja ndani ya Taifa letu la Tanzania." Amesema Msemaji huyo wa Jeshi la Polisi Tanzania Naibu Kamishna wa Polisi DCP David Misime.

Katika hatua nyingine, Polisi imeeleza kuwa nchi bado ni salama na shughuli za kiuchumi na za kijamii zinaendelea vyema katika kipindi cha saa 24 zilizopita, likishukuru pia kwa ushirikiano wanaoendelea kuupata kutoka kwa wananchi wa Tanzania.

Thursday, 11 December 2025

MARIDHIANO YATATUPA AMANI YA KUDUMU- WANANCHI

12/11/2025 11:03:00 pm

Watanzania wamehimiza utayari wa Jamii na makundi mbalimbali kushiriki katika mchakato wa maridhiano, wakisisitiza kuwa maridhiano ni silaha muhimu ya utatuzi wa migogoro mbalimbali inayotokea katika jamii kwani maridhiano ndiyo kitovu cha upatanishi kwa Taifa.

Wito huo umetolewa kufuatia kauli zilizotolewa mara kadhaa na Rais Samia Suluhu Hassan, aliyesisitiza kuongoza mchakato wa maridhiano ya Kitaifa ili kuwa na mwelekeo wa pamoja kama Taifa na zaidi katika mchakato wa upatikanaji wa Katiba mpya ya Tanzania.

Baadhi ya wananchi hao akiwemo Bw. Ridhiwan Hamidu Muhimu na Mansour Bakari, wakazi wa Ilala Jijini Dar Es Salaam wamezungumza nasi na kusisitiza kuwa chuki na magomvi si utamaduni wa Watanzania na maridhiano yatamfanya kila mmoja kupata kile anachostahili.

"Maridhiano yatapelekea kila mmoja kupata kile anachokistahili. Bila ya mazungumzo hatutoweza kufikia kwenye hali nzuri, bila ya maridhiano hatutakuwa na amani ya kudumu nchini." Amesisitiza Bw. Ridhiwan.

Bw. Bakari pia amezungumzia kuhusu ghasia za Oktoba 29, 2025 akisema maandamano haramu hayawezi kusaidia katika utatuzi wa changamoto na badala yake huzaa athari nyingi zaidi ambazo zimekuwa zikiwaathiri wananchi wa kawaida badala ya kuleta jawabu kwenye changamoto.

POLISI YAWATAKA WATANZANIA KUJIEPUSHA CHUKI NA UCHONGANISHI

12/11/2025 03:17:00 pm

Jeshi la Polisi nchini Tanzania limewataka Wananchi kuendelea kuwakataa na kuyakataa yale yote yenye mwelekeo wa kichonganishi, uzushi, uongo, yenye kujenga chuki pamoja na yenye kuhamasisha kufanya vurugu na matukio yote yenye viashiria vya kuvunja sheria za nchi.

Taarifa kwa Vyombo vya habari iliyotolewa mapema leo Alhamisi Disemba 11, 2025 na Msemaji wa Jeshi la Polisi, Naibu Kamishna wa Polisi David Misime imesisitiza pia kutosambaza ujumbe wenye kuleta chuki na uchochezi kwa jamii na badala yake kufuta ujumbe wa namna hiyo kwenye Mitandao ya kijamii ikiwemo WhatsApp.

"Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na   usalama vina wahakikishia kuwa vitaendelea kulinda amani na usalama wa nchi pamoja na maisha na mali zenu na tuendelee kutoa wito wa kuzingatia kanuni za kiusalama zinazotakiwa zianze na kila mmoja wetu kwanza sambamba na sisi sote kutii sheria." Imesema taarifa hiyo.

Katika hatua nyingine Polisi imeeleza kuwa kila mmoja aendelee kufanya shughuli zake halali bila hofu kutokana na usalama kuendelea kuimarika kote nchini Tanzania kutokana na ushirikiano mkubwa unaoendelea kutolewa kwa Vyombo vya ulinzi na usalama katika kulinda  na kuimarisha amani, utulivu na usalama nchini Tanzania.

Wednesday, 10 December 2025

RC MAKALLA AWAPONGEZA WANANCHI KWA KUYAKATAA MAANDAMANO YA DISEMBA 09

12/10/2025 04:55:00 pm

 *_Awahamasisha wananchi kujikita kwenye shughuli za kiuchumi_* 

 *_Awataka kujenga utamaduni wa kudumu wa kulinda amani na kuyakataa maandamano_* 

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla leo Jumatano Disemba 10, 2025, amewapongeza wananchi kwa kuyakataa maandamano ya Disemba 09, 2025, akiwataka kujenga utamaduni wa kudumu wa kukataa maandamano na matukio yote yenye viashiria vya uvunjifu wa amani Mkoani Arusha.

Mhe. Makalla amebainisha hayo wakati wa ziara yake ya kukagua shughuli za kibiashara  kwenye soko la Kilombero Jijini Arusha, akiahidi kuwa serikali na Vyombo vya ulinzi na usalama Mkoani Arusha vitaendelea kuhakikisha usalama na amani inakuwepo.

"Dunia imeona na watanzania wameithibitishia dunia ya kwamba wakiamua kulinda amani wanailinda, wasiotutakia mema jana wameaibika. Watanzania wanapenda amani na hawajazoea mambo ya maandamano na uvunjifu wa amani na wale wote waliokuwa wanataka vurugu leo wamejifungua- wana maumivu kwani hawakufanikiwa." Amesema Mhe. Makalla.

Mhe. Makalla kadhalika kando ya kuwahakikishia wananchi ulinzi na usalama muda wote, amehimiza pia umuhimu wa wananchi kujikita katika shughuli zao za kiuchumi na kijamii, akionya na kutangaza utimamu wa Vyombo vya ulinzi na usalama katika kukabiliana na wote wanaopanga kufanya vitendo vya uhalifu na uvunjifu wa amani katika Mkoa wa Arusha.

POLISI YAONYA WANAOENDELEA KUHAMASISHA MAANDAMANO

12/10/2025 09:22:00 am
POLISI YAONYA WANAOENDELEA KUHAMASISHA MAANDAMANO

Jeshi la Polisi nchini Tanzania kwa kushirikiana na Vyombo vingine vya ulinzi na usalama nchini wamewahakikishia wananchi kuwa wataendelea kulinda usalama wa Tanzania sambamba na maisha na mali za wananchi ili waweze kuendelea na shughuli zao kwa amani, utulivu na usalama.

Taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Jeshi la Polisi Makao Makuu, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) David Misime leo Disemba 10, 2025, limeonya pia kuhusu wanaopanga kujitokeza leo kwenye Mitaa mbalimbali ili kufanya kile kinachoitwa maandamano ya amani kutokana na kushindwa kuyafanya jana Oktoba 29, 2025.

"Jeshi la Polisi linaendelea kuwakumbusha, kuwasisitiza na kuwaonya wasifanye hivyo kwani wanachokiita maandamano ya amani yasiyo na kikomo yalipigwa marufuku kutokana na kukosa sifa kulingana na matakwa ya Katiba na sheria ya Polisi na Polisi wasaidizi sura 322." Amesema Misime.

Polisi pia imeeleza kuwa kwa ambaye atakaidi kutii sheria za nchi kwa lengo la kuhatarisha usalama wa nchi ili kusimamisha shughuli za kiuchumi na kijamii zisiendelee,  watadhibitiwa ili nchi ibaki salama na watanzania wema na wapenda amani wabaki salama.

Aidha Taarifa ya Polisi imetoa wito pia kwa wananchi kuendelea kufanya shughuli zao na kufuata maelekezo watakayokuwa wanapewa na Vyombo vya ulinzi na usalama katika maeneo yote nchini sambamba na kutii sheria za nchi ili taifa liendelee kuwa salama na kila mmoja kuweza kuendelea na shughuli zake.

Tuesday, 9 December 2025

TUNAIMARISHA ZAIDI ULINZI NA USALAMA USIKU HUU- POLISI

12/09/2025 10:42:00 pm
TUNAIMARISHA ZAIDI ULINZI NA USALAMA USIKU HUU- POLISI

Jeshi la Polisi nchini Tanzania limetoa taarifa yake kwa Vyombo vya habari kuhusu hali ya usalama nchini kwa kipindi cha saa sita tangu ilipotoka taarifa ya awali majira ya saa 6 mchana leo Jumanne Disemba 09, 2025.

Kulingana na Msemaji wa Polisi, Makao Makuu Dodoma, David Misime amesema hali ya usalama nchini imeendelea kuwa shwari na Vyombo vya Ulinzi na Usalama vimeendelea kuimarisha usalama nchini, pamoja na kulinda raia na mali zao hadi muda huu wa jioni.

"Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Vyombo vingine vya ulinzi na usalama vingependa kuwahakikishia kuwa kuanzia majira haya vitaimarisha zaidi ulinzi na usalama tunapoelekea usiku ili kuzuia na kudhibiti vitendo vyovyote vinavyoweza kuwa ni tishio la kiusalama." Amesema Kamanda Misime.

Katika hatua nyingine, Jeshi la Polisi limetoa wito kwa kila mwananchi kuendelea kuzingatia kanuni za kiusalama na kuendelea kutii sheria za nchi kwani kila mmoja anahitaji kuwa salama wakati wote.

JESHI LA POLISI LAKANUSHA TAARIFA ZA UPOTOSHAJI MTANDAONI, LATHIBITISHA USALAMA NCHINI KUWA SHWARI

12/09/2025 02:29:00 pm


Na Mwandishi wetu, Dodoma

Jeshi la Polisi nchini limekanusha taarifa zinazoenezwa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu kuwepo kwa maandamano leo Desemba 9, 2025, na kusisitiza kuwa hadi majira ya mchana hali ya usalama nchini kote ni shwari.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Jeshi la Polisi, Makao Makuu ya Polisi Dodoma,David Misime vyombo vya ulinzi na usalama vinaendelea kuimarisha ulinzi na kulinda maisha ya wananchi pamoja na mali zao kama ilivyo jukumu lao la msingi.

Polisi imeeleza kuwa picha na video zinazosambazwa mitandaoni zikidaiwa kuonyesha maandamano yanayoendelea leo si sahihi, bali ni matukio ya zamani na kwamba baadhi ya picha hizo zinatoka katika matukio ya Oktoba 29, 30 na 31 mwaka 2025, huku zingine zikitoka miaka ya nyuma ikiwemo tukio la Juni mwaka huu ambalo lilihusisha sherehe za jando za jamii ya Wamaasai zilizofanyika katika msitu wa TANAPA jijini Arusha.

Jeshi hilo limekumbusha kuwa maandamano yaliyokuwa yanatajwa kama “maandamano ya amani” yalipigwa marufuku tangu Desemba 5, 2025, baada ya kubainika hayakukidhi matakwa ya kisheria ikiwemo Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 na Sheria ya Polisi na Polisi Wasaidizi, Sura ya 322.

Aidha, Polisi imetoa wito kwa wananchi kuendelea kufuata sheria za nchi na kupuuza taarifa za upotoshaji, kwa manufaa ya amani na usalama wa Taifa.

WAFUNGWA 1,036 WAPATA MSAMAHA WA RAIS SAMIA

12/09/2025 11:44:00 am

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan leo Disemba 09, 2025, Tanzania ikiadhimisha miaka 64 ya uhuru wa Tanzania bara, ametangaza kuwasamehe wafungwa 1,036, wafungwa 22 kati yao wakiachiliwa huru na wengine 1,014 wakipunguziwa adhabu zao.

Kulingana na taarifa iliyosainiwa na Waziri wa mambo ya ndani ya nchi Mhe. George Simbachawene, Ikulu imeeleza kuwa ni matarajio ya serikali kuwa wafungwa walioachiwa huru watarejea tena katika jamii kushirikiana na wananchi katika ujenzi wa Taifa na kujiepusha kutenda makosa ili wasirejee tena gerezani.

Miongoni mwa waliosamehewa  ni wafungwa wagonjwa wenye magonjwa ya kudumu au sugu ambao wapo katika hatua za mwisho pamoja na wafungwa wazee wenye umri wa miaka 70 au zaidi- Vyote vikitakiwa kuthibitishwa na jopo la waganga wa Wilaya na Mikoa.

Aidha wengine walionufaika na msamaha huo ni wafungwa wa kike walioingia na ujauzito gerezani au wenye watoto wanaonyonya au wasionyonya waliohukumiwa kifungo cha mwaka mmoja na kuendelea pamoja na wafungwa wenye ulemavu wa mwili na akili wasio na uwezo wa kufanya kazi.

Aidha wamesamehewa pia wafungwa waliohukumiwa adhabu ya kuwekwa kizuizini (under president's pleasure) ambao wamekaa gerezani kuanzia miaka kumi au zaidi

Prf. Kitila :Serikali imepanga kufanya mageuzi makubwa katika uongozi wa mashirika ya umma

12/09/2025 11:43:00 am

Serikali imepanga kufanya mageuzi makubwa katika uongozi wa mashirika ya umma, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kuwa watendaji wakuu na wajumbe wa bodi za wakurugenzi wanapatikana kwa njia ya ushindani ili kuongeza uwazi, uadilifu na ushiriki mpana wa Watanzania wenye sifa.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo, amesema mfumo huo mpya utaanza kutumika kuanzia Julai 1, 2026 mara baada ya kupitishwa kwa sheria mpya inayoandaliwa na serikali.

Amesema uamuzi huo ni sehemu ya mpango mpana wa kuboresha utendaji wa mashirika ya umma, kuweka uwazi katika uteuzi wa viongozi, na kuondoa utaratibu wa uteuzi wa moja kwa moja uliokuwa ukilalamikiwa na wadau kwa kukosa ushindani wa wazi. 

“Kama ni Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO utaomba, uta-apply, na utashindanishwa. Kama unataka kuwa mjumbe wa bodi ya TPA au TISEZA utapitia mchakato wa ushindani. Watanzania wote wenye sifa wataomba, na uchaguzi utafanywa kwa ‘competitive recruitment,” amesema.
Katika maelezo yake kwa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Prof. Mkumbo amesema mageuzi hayo yanakwenda sambamba na hatua kadhaa zinazolenga kuongeza tija ya mashirika ya umma na kuimarisha mchango wake katika uchumi wa taifa na utoaji wa huduma kwa wananchi.

Prof. Mkumbo amesema serikali inaunda mfumo mpya na imara wa kupima maendeleo ya mashirika ya umma kwa kuzingatia tija ya kiuchumi na ubora wa huduma. Mashirika hayo yatapewa vigezo vipya vya kupimwa na kila moja litahesabiwa kwa kiwango kinachochangia kwenye uchumi na ustawi wa wananchi.

Amesema sheria mpya itayataka baadhi ya mashirika ya umma ya kibiashara kujisajili katika Soko la Hisa  ili Watanzania waweze kununua hisa na kumiliki mashirika yao, kupanua uwazi katika uendeshaji, na kuongeza uwajibikaji kwa menejimenti na bodi.

Serikali yaweka kipaumbele katika kuhuisha majengo na kupanga upya miji mikubwa

12/09/2025 11:43:00 am

Serikali imeweka kipaumbele katika kuhuisha majengo na kupanga upya miji mikubwa, hatua inayolenga kuongeza thamani ya makazi, kuboresha matumizi ya ardhi na kuvutia uwekezaji katika kipindi cha pili cha miaka mitano ya Serikali ya Awamu ya Sita.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo amesema mpango huo utahusisha ubia kati ya wananchi na sekta binafsi ili kubomoa nyumba chakavu, kujenga majengo mapya ya ghorofa na kuwapa wakazi sehemu za makazi na biashara ndani ya miradi hiyo.

Akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam siku ya Jumatatu, Prof. Mkumbo amesema Serikali tayari imeainisha maeneo matatu ya kuanzia Vingunguti, Buguruni na Manzese kwa mkoa wa Dar es Salaam ambapo michakato ya kuwavutia wawekezaji itatangazwa rasmi, huku wakazi waliopo wakihakikishiwa kunufaika moja kwa moja kupitia mfumo wa kupata ‘floor’ zao za makazi na biashara katika majengo mapya.

Waziri huyo amesema mageuzi ya miji ni sehemu ya mkakati mpana wa kufungua fursa za uchumi, kuongeza ajira na kuboresha ubora wa maisha katika maeneo ya mijini. Ameeleza kuwa matumaini ya Serikali ni kuona miji ya Dar es Salaam na baadaye mingine nchini ikiwa na makazi yaliyopangwa vizuri na miundombinu ya kisasa.

Amesema sambamba na kuhuisha miji, Serikali inaelekeza nguvu katika kufungua maeneo mapya ya utalii tofauti na yale yanayofahamika sana kama Ukanda wa Kaskazini, huku akitaja Hifadhi ya Taifa ya Ruaha kama moja ya maeneo makubwa yenye uzuri wa kipekee lakini ambayo hayajafunguliwa kikamilifu. Pia ameeleza kuwa utalii wa fukwe haujatumiwa ipasavyo licha ya Tanzania kuwa na mwambao mrefu uliojaa vivutio.

Prof. Mkumbo amesema Serikali itaendelea kushirikiana na sekta binafsi ya ndani na nje ya nchi ili kuongeza uwekezaji katika utalii, ujenzi na miundombinu, hatua anayosema itachochea ukuaji wa mapato ya taifa na kupanua ajira kwa vijana.

WAZIRI MKUU AWAKINGIA KIFUA WAFANYABIASHARA WADOGO ATOA ONYO KALI KWA HALMASHAURI ZOTE NCHINI

12/09/2025 11:43:00 am

Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu  Nchemba ameagiza Halmashauri zote Nchini  Majiji  kutochukuwa bidhaa halali za Wananchi  ambao ni wafanyabiashara wadogo wanaojitafutia riziki zao Barabarani kulingana na mitaji yao hata kama wakikutwa na makosa  ushughulikiwe utaratibu tu!  na sio kuua mitaji yao midogo 

"Huu utaratibu wa kuchukua bidhaa haukubaliki wafautilieni waliochukuwa bidhaa na kama hazipo hao ni wezi kama wezi wengine tusicheze na mitaji ya watu hatutapiga vita umasikini kama hatutaheshimu mitaji ya watu "  Waziri Mkuu 

Aidha ametumia jukwaa hilo kuwaambia kutangaza Ziara ya majiji yote Nchini kuangazia changamoto za wafanyabiashara hao na kuendelea kuacha utaratibu huo hapo hapo amesisitiza kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan ni mtu wa haki hivyo watendaji wasimuangushe

Monday, 8 December 2025

Waziri amewaomba Watanzania kutojihusisha na maandamano yasiyokuwa rasmi kisheria Disemba 9 ,2025.

12/08/2025 02:38:00 pm

Waziri wa Mambo ya ndani Mhe. George Boniface Simbachawene amesisitiza kuwa maandamano yanayohamasishwa kufanyika kesho Jumanne Disemba 09, 2025 ni haramu na yatadhibitiwa na Vyombo vya ulinzi na usalama ikiwa yatafanyika, akitaka wote wanaotaka kuandamana kufuata sheria na miongozo iliyopo.

Kulingana na Waziri Simbachawene mbele ya  waandishi wa habari leo Jumatatu Disemba 08, 2025, amewaomba pia Watanzania kutojihusisha na maandamano hayo yasiyokuwa rasmi kisheria   kutokana pia na kushamiri kwa matukio na viashiria vya uvunjifu wa amani na uhalifu.

"Maandamano hayo yanayoitwa ya amani hayaonekani yanaombwa na nani, kwa utaratibu gani na yatafanyika wapi. Haya yanayoelezwa ni kwamba wanaeleza tu kuwa yatakuwa hayana ukomo na yatakuwa makubwa kuliko yale ya tarehe 29."

"Ndugu zangu kama yakiwa hayo ni maandamano yasiyo na ukomo, maandamano ambayo ni makubwa kuliko yale ambayo watu walichoma mali za watu, watu, walichoma vituo vya mafuta, majengo ya serikali, Vituo vya polisi na hata watu wakafa, sasa haya tunayoambiwa ni makubwa kuliko yale si maandamano kwasababu kwanza hayana kibali kwa mujibu wa sheria lakini pia hayaeleweki yanafanywa na nani." Amesema Mhe. Waziri

Kulingana na Waziri Simbachawene, maandamano rasmi kulingana na sheria, maandamano ni lazima yawe na ukomo, lazima yaombwe na mtu mahususi, yawe na ujumbe, yaseme shabaha pamoja na kueleza muelekeo wake ili Jeshi la Polisi liweze kutoa huduma yake ya ulinzi kwa waandamanaji wa tukio husika.

Mhe. Simbachawene amethibitisha kuwa maandamano ya Disemba 09 ni haramu na yasiyokubalika, akitoa rai kwa wote walioichoka amani ya Tanzania kuheshimu sheria za nchi na ikiwa vinginevyo, Vyombo vya ulinzi na usalama vitawathibiti kulingana na sheria.

Sunday, 7 December 2025

KAULI YA MSIGWA "VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA VIPO TIMAMU MUDA WOTE KULINDA RAIA"

12/07/2025 02:53:00 pm

Msemaji Mkuu wa Serikali ya Tanzania Bw. Gerson Msigwa amesisitiza kuwa Vyombo vya Ulinzi na usalama, wakati wote vipo tayari muda wote kuhakikisha kuwa Mipaka ya nchi, Watanzania na mali zao wanabakia salama muda wote.

"Sisi kama Nchi, Vyombo vyetu vya ulinzi na usalama kama vilivyokuwa jana, kama vilivyo leo ndivyo vitakavyokuwa tarehe tisa Disemba na tarehe zitakazofuata. Wakati wote Vyombo vyetu vipo tayari kuhakikisha watu na mali zao wapo salama na mipaka yetu inabakia salama. Vipo tayari si tarehe tisa tu ni wakati wote kuhakikisha nchi inakuwa salama." Amesema Msigwa.

Akizungumza na chombo kimoja cha Habari Mkoani Dar Es Salaam, Msemaji huyo wa serikali ametoa wito pia kwa Watanzania kushiriki katika kuilinda nchi yao kwa wivu mkubwa, akiwataka kutohakikisha hakuna anayeweza kuwapangia la kufanya na badala yake wafanye mambo kwa namna ya mahitaji yao wenyewe.

Msigwa kadhalika amesisitiza kuwa serikali ya awamu ya sita ipo tayari muda wote kuwasikiliza Watanzania na kuyafanya yale yote watakayoona yanafaa kulingana na rasilimali zilizopo nchini.

355 MIKONONI MWA POLISI MKOANI MWANZA KWA WIZI NA UPORAJI WA OKTOBA 29.

12/07/2025 12:01:00 pm

Jeshi la Polisi Mkoani Mwanza limefanya msako na kufanikiwa kuwakamata jumla ya wahalifu wapatao 355 ambao wamekamatwa na kufikishwa Mahakamani kwa makosa mbalimbali ikiwemo wizi na uporaji walioufanya wakati na baada ya uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025.

Kulingana na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Naibu Kamishna wa Polisi Wilbroad Mutafungwa, Polisi kwa kushirikiana na Vyombo vingine vya ulinzi na usalama vimewakamata Jumla ya watu wengine 116  kwa tuhuma za uchochezi na kuhamasisha maandamano haramu wanayopanga kuyafanya Jumanne ya Disemba 09, 2025.

Kulingana na Kamanda Mutafungwa watuhumiwa 355 waliokamatwa walikutwa na Mitungi 118 ya gesi ya Kampuni ya Lake Oil Oryx na Mihan, Magodoro 40 aina ya Super Banco na Tanform pamoja na jora 18 za Vitambaa vya kushonea magodoro.

"Watuhumiwa wengine wamekamatwa na  difu 1 ya gari, Injini 3 za magari, Gear boksi, Mashine 2 za ATM, Matenki 4 ya maji, Fire Extinguisher 3, Compresser 01, Pipa 4 za Kemikali za kutengenezea magodoro, Friji 1 aina ya Voni, Kasiki 2, ndoo za rangi pamoja na mabati 14." Amesema Kamanda Mutafungwa.

Jeshi la Polisi Mkoani Mwanza kando ya kueleza kuendelea na doria katika Mkoa mzima wa Mwanza, katika taarifa yake kwa umma limetoa rai kwa wananchi kutokubali kushirikishwa kwenye maandamano haramu yaliyopigwa marufuku hapo Disemba 09, 2025, Wazazi na walezi wakitakiwa kuwazuia watoto wao kutojiingiza kwenye maandamano na badala yake washirikiane na serikali kuimarisha amani na utulivu kwenye siku hiyo muhimu ya kumbukizi ya Tanzania kupata uhuru wake.

RC MTAKA ALIA NA VIJANA WA GEN_Z NCHINI, AWATAKA KULINDA AMANI YA NCHI YAO.

12/07/2025 11:06:00 am

Na Mwandishi wetu,Njombe

Mkuu wa Mkoa wa Njombe Antony Mtaka amekisihi  kikundi cha vijana wanaojiita Gen_Z kutambua kuwa wao ni kizazi  kinachobeba matumaini na sura ya taifa,hivyo wanapaswa kulinda Amani badala ya kujiingiza kwenye makundi ya kutaka kuangamiza Taifa.

Mkuu huyo wa Mkoa ametoa kauli hiyo kwenye Ibada katika Kanisa la wa Adventist Wasabato lililopo Mkoa wa Njombe ambapo ametumia Fursa hiyo kuisihi jamii hususani Vijana kutambua kuwa Amani ni Tunda la Haki ambapo ni wajibu wa kuilinda Amani ya nchi yetu kwa Wivu Mkubwa,

 “Mkoa wetu bado upo salama,hauna matishio ya kihalifu,tunaendelea kujenga mazingira thabiti ya ulinzi wa watu na mali,ili kutoa fursa kwa wananchi wetu kuendelea kufanya shughuli zao za uzalishaji mali na mahangaiko yao ya kujipatia kipato cha siku, 

"Na kuongeza " Usalama wa mkoa wetu, utatuongezea imani kwa wawekezaji wetu mbalimbali kuendelea kuamini kwamba Njombe ni mahala sahihi pa wao kuweka mitaji yao,wana Njombe tushikamane kuhakikisha tunaziepuka aina yoyote ya chokochoko zitakazoashiria uhalibifu wa mali, uwekezaji,miradi ya umma na binafsi,au uharibifu wa uhai wa wananchi wenzetu." Amesema  Rc  Mtaka.

Hata hivyo amewataka Wananchi kutoa taarifa kwenye vyombo husika pale watakapoona na  kuhisi dalili yoyote inayoashiria uvunjifu wa amani , kuhatarisha usalama wa eneo lao ,kwani ulinzi shirikishi huanza na wanajamii mmoja mmoja kwa kutoa taarifa kwa wakati.

Ikumbukwe kuwa kupitia mitandao ya kijamii kumekuwepo na baadhi ya wanaharakati walioanzisha kikundi kinacho jiita wana Gen _Z cha kuhamasisha maandamano na uvunjifu wa Amani Nchini jambo ambalo halikubaliki kwa Taifa na jamii kwa ujumla.

Mwisho.

Saturday, 6 December 2025

MKASA WA SALAH WA SUDAN NA HARAKATI MFU ZA MANGE KIMAMBI

12/06/2025 04:30:00 pm

Mwaka 2019 Alaah Salah alikuwa na umri wa miaka 22 huku akiwa mwanafunzi wa mwaka wa pili kwenye Chuo Kikuu cha Sudan. Aliongoza na kuhamasisha maandamano yaliyomtoa Omar Bashir madarakani. Mpaka sasa Omar Bashir yuko kifungoni akitumikia adhabu ya makosa ya jinai aliyotenda madarakani.

Wakati huo wengi waliingizwa barabarani bila ya kujua kuwa walikuwa wakifanikisha mradi wa aliyeitwa mwanamke shujaa na mzalendo, Salah akapata umaarufu mkubwa, akitukuzwa na Mataifa na Vyombo vya habari vya Kimagharibi, akitwikwa majina kadhaa na kumpa sifa za ujasiri na ushujaa kama mpigania haki, demokrasia na Mwanamapinduzi wa kweli.

Baada ya Mapinduzi ya mwaka 2019 upepo ukabadilika, lengo la mabeberu likatimia, Omar akapinduliwa watu wakidhani kuwa matumaini yao yanaenda kutimia, bahati mbaya ndio ukawa mwanzo wa kuiharibu nchi yao wenyewe, Jinamizi la mauaji likatanda, unyanyasaji ukatapaaa Sudan na Mwanamke Salah akapotea na haonekani tena akikemea ama kupaza sauti kuhusu unyanyasaji na ukatili unaoendelea nchini mwake.

Taifa hilo limekumbwa na moja ya migogoro ya kibinadamu mibaya zaidi duniani, zaidi ya watu milioni 15 wamelazimika kukimbia makazi yao na zaidi ya watu milioni 30 wanahitaji msaada wa kibinadamu, wakiwemo milioni 24.6 wanaokabiliwa na njaa kali, kwa mujibu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa. Makadirio yanaonesha kuwa watu wapatao 150,000 wameuawa ndani ya mwaka wa kwanza wa mapigano pekee.

Alaah ni mfano halisi wa kile Mange Kimambi anachokifanya kwa sasa nchini Tanzania, haishi Tanzania na mara zote amedai kuwa hana la kupoteza nchini. Si ndugu wala mali zake na ndicho kinachomfanya kuwa kinara wa kuhamasisha vurugu nchini- aiweke nchi kwenye janga, apokee malipo yake na atuache Watanzania tukitaabika katikati ya machungu ya kuiharibu nchi yetu wenyewe.

Watanzania tuamke, tujifunze kwenye tone dogo la maumivu tulilolipata Oktoba 29, 2025. Tujiepushe na akina Alaah wa Tanzania wanaobebwa na kusifiwa na Vyombo vya habari vya magharibi ili kutupofusha akili na kuamini kuwa wanatutakia mema ilihali wanasimamia maslahi yao binafsi.

TAASISI ZA KIMATAIFA ZATAKIWA KUIACHA MIFUMO YA KITAIFA KUFANYA KAZI YAKE

12/06/2025 11:09:00 am

Serikali ya Tanzania katika taarifa yake kwa Vyombo vya habari leo Ijumaa Disemba 05, 2025 imetangaza kuzipokea na kuzifanyia kazi taarifa na matamko mbalimbali yaliyotolewa na nchi rafiki, mashirika ya kimataifa na Taasisi za maendeleo kuhusu Tanzania na matukio ya uvunjifu wa amani wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Jumatano Oktoba 29, 2025.

Kulingana na Taarifa ya Wizara ya mambo ya nje, miongoni mwa waliotoa matamko hayo ni pamoja na Ubelgiji, Canada, Denmark, Ujumbe wa Umoja wa Ulaya (EU), Finland, Ufaransa, Ghana, Ujerumani, Ireland, Italia, Uholanzi, Norway, Poland, Slovakia, Hispania, Sweden, Uswisi, Uingereza, Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa, Marekani pamoja na Taasisi ya Thabo Mbeki ya Afrika kusini.

Katika taarifa hiyo, Tanzania imeonesha kushangazwa na baadhi ya maudhui ya matamko hayo, hasa ikizingatiwa kuwa kulifanyika mazungumzo ya wazi kati ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mabalozi wanaowakilisha nchi hizo nchini, tarehe 28 Novemba 2025.

Serikali imesisitiza kuwa, pamoja na kutambua nafasi ya jumuiya ya kimataifa katika kuimarisha demokrasia na maendeleo ya kijamii na kisiasa, ni muhimu pia kuheshimu uamuzi wa kuundwa kwa Tume ya Uchunguzi itakayochunguza kwa kina matukio ya vurugu zilizotokea baada ya uchaguzi, na kuandaa ripoti kamili.

Ripoti hiyo, kwa mujibu wa Serikali ndiyo itakayoleta uelewa mpana kuhusu kilichotokea na kuwa msingi wa mashauriano na ushirikiano wa baadaye katika kujenga taifa lenye amani na umoja.

"Serikali ya Tanzania inaendelea kuwa mstari wa mbele katika ushirikiano wa kimataifa kwaajili ya amani na maendeleo na inatoa wito kwa wadau wote kuruhusu mifumo ya kitaifa kufanya kazi yake kwa mujibu wa taratibu zilizowekwa," imeeleza taarifa hiyo.

Aidha, Serikali ya Tanzania imewahakikishia wadau wa maendeleo na jumuiya ya kimataifa kuwa itaendelea kujadiliana na kushirikiana nao katika masuala yote ya maslahi ya pande zote, kwa misingi ya usawa na kuheshimiana.

Friday, 5 December 2025

Dkt .Asha-Rose Migiro, awasisitiza wanawake nchinii jukumu la uongozi katika kulinda na kuimarisha amani.

12/05/2025 02:27:00 pm
Na Doreen Aloyce,Dodoma

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Asha-Rose Migiro, ametaka kuanzishwa kwa mazungumzo ya kitaifa ya maridhiano huku akiwasisitiza wanawake nchini kuchukua jukumu la uongozi katika kulinda na kuimarisha amani. Wito huo umetolewa wakati wa ufunguzi wa Jukwaa la Wanawake 2025 lililofanyika jijini Dodoma chini ya kaulimbiu “Mama ni Amani”.

Katika hafla hiyo, washiriki walioneshwa makala ya video iliyodokeza matukio ya vurugu za Oktoba 29, 2025, ikionesha kiwango cha uharibifu wa mali na taarifa za vifo, ingawa idadi kamili ya waliofariki haikutajwa. Dk. Migiro alisema matukio hayo hayalingani na utamaduni wa Tanzania wa mshikamano na utulivu, hivyo kuhitaji hatua za makusudi kurejesha hadhi ya taifa.

Amefafanua kuwa zaidi ya asilimia 50 ya Watanzania ni vijana na ndiyo maana wanawake wanapaswa kuwa mstari wa mbele katika malezi, uongozi wa majadiliano ya maridhiano na kuzuia kurudiwa kwa matukio ya vurugu.

Washiriki wa jukwaa hilo walitoa maoni mbalimbali kuhusu nafasi ya mwanamke katika kudumisha amani.
Kate Kamba alisisitiza kuwa wanawake ni walimu wa kwanza wa familia na wanabeba jukumu muhimu la kujenga misingi inayoweza kuzuia machafuko ya baadaye. Alionya kuwa bila kuwekeza katika malezi bora, taifa linaweza kupoteza mwelekeo wake.

Sifa Swai, kwa upande wake, alisema changamoto za usalama wa amani zimehamia zaidi kwenye mitandao ya kijamii ambako taarifa potofu husambaa kwa kasi, hivyo kuwaathiri hasa vijana. Aliongeza kuwa misukosuko katika biashara zinazomilikiwa na wanawake huathiri moja kwa moja ustawi wa familia na inaweza kuchochea migogoro ya kijamii.

Kwa pamoja, washiriki walikazia umuhimu wa sauti ya mwanamke katika kuponya makovu ya kijamii, kudumisha umoja na kuongoza juhudi za maridhiano nchini.

WATANZANIA WAFURAHISHWA NA META KUZIFUNGIA AKAUNTI ZA MANGE NA MARIA

12/05/2025 11:12:00 am

Wanaharakati Mange Kimambi na Maria Sarungu Tsehai wenye msururu kadhaa wa lawama, malalamiko na kutajwa kuwa sababu ya uvunjifu wa maadili, amani na umoja wa Watanzania wamefungiwa akaunti zao za Meta, kampuni mama ya Teknolojia yenye kumiliki mitandao ya (Instagram, Facebook na WhatsApp).

Mange na Maria wanashutumiwa pia kwa kuchochea matukio ya uvunjifu wa amani, mabaya zaidi kuwahi kutokea kwa siku za hivi karibuni nchini Tanzania, Yakifanyika wakati na baada ya uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 na kusababisha uharibifu mkubwa wa mali za umma na za binafsi, Wizi, uchomaji moto na vifo vya watu kadhaa kulikotokana na udhibiti wa tukio hilo na umiliki wa silaha kutoka kwa Vituo vya Polisi vilivyovamiwa na Makundi hayo ya kihalifu.

Meta imethibitisha taarifa hizo kwa kuandika " Akaunti hizo zimeondolewa kwa kukiuka sera yetu. Haturuhusu watu kuunda akaunti mpya zinazofanana na zile tulizoziondoa awali kwa kukiuka viwango vya juu vya Taasisi ya Meta."

Mange na Maria wanatajwa kupokea mabilioni ya fedha kutoka kwa Taasisi na watu binafsi ili kuchochea vurugu, chuki na machafuko ndani ya Tanzania, wakitumia mitandao yao ya Kijamii kuratibu na kuhamasisha machafuko na mauaji ya raia nchini Tanzania kwa kipindi kirefu hivi sasa suala ambalo limesababisha wananchi wa Tanzania kufurahishwa na uamuzi wa @meta kuzifungia akaunti zao kwa mustakabali wa amani na ulinzi wa haki za binadamu. 

Watu hawa wamepigiwa mfano kama watu halisi wanaotumia Mitandao ya Kijamii kwa namna hasi yenye kuleta hasara, ghasia na vurugu kwenye jamii kwa maslahi yao binafsi bila kujali haki za wengine.

Hii si mara ya kwanza kwa Kampuni ya Meta kuzifungia akaunti zinazokiuka miongozo ya kampuni hiyo ya teknolojia kwani Januari 2021, Meta waliifunga akaunti ya X ya Rais wa Marekani Donald Trump kwa kile walichokieleza kama hatari ya kuchochea vurugu baada ya kutoa wito kwa wafuasi wake kuvamia bunge wakijaribu kuvuruga kikao cha kuidhinisha ushindi wa Rais Mstaafu Joe Biden. Vurugu hizo zilifanyika na zilisababisha uharibifu na vifo kadhaa vya wananchi.

Aidha mwaka 2022 Mtandao wa X pia ulizifungia akaunti za gazeti maarufu nchini humo la Caravan na akaunti ya muigizaji Sushant Singh na ya Mwanaharakati Hansraj Meena kwa madai ya kukiuka masharti ya mtandao huo kutokana na kujihusisha na maandamano ya kutaka mabadiliko katika kilimo nchini humo.

Thursday, 4 December 2025

Simbachawene awataka Vijana na Wanaharakati kutafuta njia sahihi ya kudai haki ikiwemo mazungumzo mezani

12/04/2025 06:14:00 pm
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,George Simbachawene amewataka Vijana na Wanaharakati kutafuta njia sahihi ya kudai haki ikiwemo mazungumzo mezani akiwaasa kuwa vita na vurugu avijawahi kusaidia bali upelekea kupotea kwa amani huku akitolea mfano wa nchi ya Kidemokrasia ya Kongo ambayo takribani ni zaidi ya miaka thelathini wanaitafuta amani ambayo imepotea.

Ametoa kauli hiyo wakati wa Mkutano wa Pili unaohusisha Pande Tatu ikiwemo Serikali ya Tanzania, Jamhuri ya Demokrasia ya Congo na Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani UNHCR ambapo pia walitumia mkutano huo kusaini nyaraka zinazoelezea Mpango wa Urejeshwaji wa Wakimbizi Elfu Themanini na Sita na Mia Mbili Hamsini na Sita waliopo hapa nchini ambapo pia Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Ndani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo,Shabani Bihango na Mwakilishi wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani nchini Tanzania,Barbara Dotse waliishukuru Tanzania kwa kuhifadhi wakimbizi hao kwa muda unaozidi miaka thelathini.

Tuesday, 2 December 2025

matukio ya uvunjifu wa amani yaliyotokea wakati na baada ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025 yalikuwa ni matukio ya kupangwa yakiwa na lengo la kuiangusha dola ya Tanzania.

12/02/2025 06:34:00 pm
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema serikali na Vyombo vya ulinzi na usalama vimejipanga wakati wote kukabiliana na wanaoratibu, kupanga na kufadhili matukio ya uvunjifu wa amani yaliyopangwa kufanyika aidha Disemba 09 ama Disemba 25, 2025.

Rais Samia amebainisha hayo leo Jumanne Disemba 02, 2025 wakati akizungumza na wazee wa Mkoa wa Dar Es Salaam, akikaririwa awali akisema kwamba matukio ya uvunjifu wa amani yaliyotokea wakati na baada ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025 yalikuwa ni matukio ya kupangwa yakiwa na lengo la kuiangusha dola ya Tanzania.

"Ndugu zangu nilisema yaliyopita si ndwele tugange yajayo, lililopita limepita, kwa maneno tunasikia lipo jingine linapangwa lakini inshaallag Mola hatosimama nao, litapeperuka.

Lakini nataka niseme, nilimsikia mmoja kati ya waandaaji wa nje anasema ebu tarehe tisa lihairisheni subirini Krismasi kwasababu sasa hivi wamejipanga, nataka niwaambie wakati wowote wakija tumejipanga." Amesema Rais Samia.

Katika hatua nyingine Rais Samia amesema kama binadamu kukosana kupo, akikiri kuwa si kila wakati serikali inakuwa haina mapungufu, akisisitiza umuhimu wa kukaa, kuzungumza na kuondoa mapungufu 

Monday, 1 December 2025

WATANZANIA WANATAKA UWAZI NA UCHUNGUZI KAMILI- JAJI OTHMAN CHANDE

12/01/2025 05:58:00 pm

Mwenyekiti wa Tume ya Uchunguzi wa matukio ya uvunjifu wa amani wakati na baada ya uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 Jaji Mkuu mstaafu Mohammed Chande Othman amesema Watanzania wanataka uchunguzi kamilifu wa Matukio ya Oktoba 29 pamoja na kutaka uwazi kwenye kutekeleza wajibu wao.

Jaji mstaafu Othman amebainisha hayo leo Jumatatu Disemba Mosi, 2025 wakati akizungumza na waandishi wa habari, akisisitiza kuwa baadhi ya Mikutano yao wataifanya hadharani na mingine faragha ili kulinda haki za watu wengine.

"Mikutano yetu mingine itafanyika kwenye hadhara na mingine itabidi tuende kwenye faragha kwenye mazingira maalumu ili kulinda haki za mtu na Tanzania sasahivi tuna sheria ya kulinda faragha za watu." Amesema Jaji Othman.

Mwenyekiti huyo wa tume ameeleza kuwa matakwa hayo ya watanzania wameyapokea na ndiyo watakayoyatumia katika kujibu hadidu za rejea katika utekelezaji wa majukumu yao ya uchunguzi wa matukio hayo ya Oktoba 29, 2025.

TUSIKUBALI KUCHONGANISHWA NA WACHACHE WENYE MASLAHI BINAFSI- MWIGULU

12/01/2025 05:12:00 pm

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba akiwa kwenye Ziara yake ya Kikazi Mkoani Arusha, amesisitiza umuhimu wa kulinda amani kwa maendeleo na ustawi wa Watanzania, akiwataka wananchi kuamka na kuwakataa wale wote wanaowachonganisha kwa maslahi yao binafsi.

Akieleza kuwafahamu baadhi ya Watanzania wanaolipwa fedha ili kuwagombanisha na kuwataka kuingia barabarani kufanya vurugu, Mhe. Nchemba ameeleza kuwa wanaohamasisha vurugu nchini wamekuwa na visingizio kadhaa vya kuwahadaa wananchi huku lengo lao likiwa ni kuwagombanisha watanzania ili kutaka kuzifaidi rasilimali za nchi.

"Zimetokea vurugu, kwa aina  ya vurugu zilivyotokea, kwanini hatushtuki? Wanatumia visingizio vingine lakini hapa kuna mchezo. Zimetolewa fedha wakapewa vijana na wale Vijana wakaandaa Vijana wenzao na kuwataka kufanya vurugu. Leo tujiulize wale wanaotoa hizo fedha watazirudishaje? Na kama ni maandamano, Kiongozi wake alikuwa nani? Waliandamana kutoka wapi kwenda wapi? Ajenda yao ilikuwa ipi? Tunachonganishwa mno, kuna jambo watu wanatafuta. Amkeni Watanzania." Amesema Waziri Mkuu.

Mhe. Mwigulu akizungumza katika Mkutano wake wa hadhara kwenye Viwanja vya Magufuli, Leganga, Usa River, Wilayani Arumeru, amesisitiza kuwa ikiwa Tanzania itapoteza amani na utulivu wake, jamii na serikali itashindwa kukabiliana na umaskini, gharama kubwa za maisha na kukabiliana na tatizo la ajira kwa Vijana, akiwataka Watanzania kutorubuniwa na kuingia kwenye Vitendo vya Uvunjifu wa amani.

Sunday, 30 November 2025

MZEE WA UPAKO AWATAKA WATANZANIA KUJIFUNZA KUTOKANA NA TUKIO LA OKTOBA 29, "HALIPASWI KURUDIWA TENA"

11/30/2025 09:28:00 pm

Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC), Anthony Lusekelo ‘Mzee wa Upako’, ametoa wito kwa Watanzania kujifunza kutokana na tukio la Oktoba 29, akisema limeleta maumivu makubwa kwa taifa na halipaswi kurudiwa tena. Amesema tukio hilo limekuwa uzoefu mpya ambao Watanzania hawakuwahi kuupitia, akiwapa pole wakazi wa Dar es Salaam, Arusha, Songwe na Mwanza ambao amesema wameguswa sana na kilichotokea.

Amesema hali hiyo imemkumbusha mazingira ya mwaka 1977/1978 wakati wa vita dhidi ya Idd Amin, akieleza kuwa tukio la Oktoba 29 lilikuwa kama “vita ya wenyewe kwa wenyewe.” Pamoja na kueleza kuwa wapo waumini wake waliopigwa risasi maeneo ya Kimara, amesema hakuna Mtanzania ambaye hajaguswa, hivyo si wakati wa kulaumiana bali kila mtu ajihoji kwa nini nchi imefika hatua hiyo huku akionya kuwa kutokujifunza kutokana na kilichotokea kunaweza kusababisha tukio jingine kubwa zaidi baada ya miaka michache ijayo.

Mzee wa Upako amesema ni lazima Watanzania, wakiwemo viongozi wa dini, wazazi, viongozi wa serikali na kisiasa, kutafakari namna ambavyo heshima ya nchi imeharibika na kwamba  ni muhimu kurejea kwenye misingi hiyo ili matukio kama ya Oktoba 29 yasijirudie tena.

MISA YAWANOA WAANDISHI WA HABARI, NAIBU WAZIRI LONDO ASEMA SERIKALI ITAENDELEA KULINDA UHURU WAO

11/30/2025 11:32:00 am

Na Doreen Aloyce, Dodoma

NAIBU Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Dennis Lazaro Londo, amewahakikishia waandishi wa habari nchini kuwa Serikali itaendelea kulinda uhuru wao wa kujieleza pamoja na kuhakikisha wanatimiza majukumu yao kwa usalama na weledi.

Mhe. Londo amezungumza hayo ljijini Dodoma katika mafunzo ya waandishi wa habari  yaliyoandaliwa na Misa Tanzania yaliyowaleta pamoja Wanahabari 100 kutoka maeneo mbalimbali nchini, ambapo Londo amesema Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi itaendelea kushirikiana na wadau wa habari katika maeneo yote yanayohusu usalama kwa waandishi wa habari.

Aidha, amebainisha kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imeweka msukumo mkubwa katika kuhakikisha wananchi wanapata taarifa sahihi, sambamba na kulinda uhuru wa vyombo vya habari. 

" Falsafa ya Mhe. Rais kupitia “4R” zinaipa tasnia ya habari nafasi muhimu katika kulinda amani, kuimarisha umoja wa kitaifa na kuendeleza mijadala yenye tija kwa jamii." Amesema Londo.

Edwin Soko ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika – Tawi la Tanzania (MISA Tanzania),   ametahadharisha kuwa uandishi unaolenga kugawa jamii unadhoofisha misingi ya amani ambayo nchi imeijenga kwa miaka mingi,huku akisisitiza kuwa vyombo vya habari vinapaswa kujikita kuandika habari ambazo zitaleta umoja na mshikamo sio kuchochea mgawanyiko na uhasama kwa taifa.


“Hii ndiyo Tanzania, sisi ndiyo Watanzania,tukiruhusu nchi yetu ikawaka moto hatuna pa kwenda.Wapo wanaolaumu na kuona kama vyombo vya habari havijatimiza wajibu wake Oktoba 29,2025 wakati wa uchaguzi, na kusahau kuwa vyombo vya habari havilengi kwenye kuiboa jamii bali kuijenga ,”amesema Soko.

Pia Soko ametumia fursa hiyo,kusisitiza umuhimu wa waandishi na vyombo vya habari kuwa uhuru na kufanya kazi zao kwa kufuata maadili ya uandishi bila msukumo au shinikizo kutoka kwa watu binafsi.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha SAUT Mwanza, Dkt. Dotto Bulendu, akizungumza wakati akiwasilisha mada kuhusu umuhimu wa uandishi wa habari jengefu,amesema jamii inahitaji taarifa zenye mizania sahihi pia sauti za vijana zishirikishwe na zisikike katika mambo ya kitaifa.


“Nadhani uandishi huu utatusaidia kuondoka hapa tulipo,wananchi wanataka kuona serikali ikiwajibika na ikija na majibu pia wanahitaji kusikilizwa. Kwa maana hiyo waandishi tunatakiwa kuwa kiunganishi cha makundi yote na kuepuka habari zinazoibua taharuki,”amesema Bulendu 

Kwa upande wake Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini,DCP David Misime,akiwasilisha mada ya wajibu wa vyombo vya habari katika kukuza amani amesema ni pamoja na kuandaa na kutangaza taarifa nyingi zenye maudhui ya kuhımıza na kuimarisha umoja, mshikamano, amanı,utulivu na upendo utakaowezesha maridhiano.


“Yaliyotokea Oktoba 29,2025 hakuna ambaye hakuonja machungu yake.Tumejifunza,binafsi nimejifunza namna ya umuhimu wa amani,”amesema Misime.

DCP.Misime amesema, waandishi wanapaswa kubuni na kukuza majadiliano yanayojenga badala ya kugawa wananchi na taifa,kuzingatia ukosoaji wa kihabari unaojenga na wenye lengo la kuboresha,kuripoti mapungufu bila kuchochea migogoro,kuchambua masuala kwa uadilifu pamoja na kutoa majibu mbadala

Amesema,waandishi wa habari ni watu muhimu na wana mchango mkubwa katika kukuza na kuimarisha usalama, utulivu na amani.


Mwisho.


Saturday, 29 November 2025

HATUTORUHUSU KUTOKEA TENA KWA VURUGU NCHINI- SIMBACHAWENE

11/29/2025 01:28:00 pm

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. George Boniface Simbachawene ametoa wito kwa wananchi na hususani Vijana wa Tanzania kudumisha amani na kuepuka kupanga, kuratibu ama kushiriki kwenye maandamano, akisema kwamba Tanzania bado inakabiliwa na athari kubwa zilizosababishwa na matukio ya Uvunjifu wa amani ya siku ya uchaguzi Mkuu na baada ya uchaguzi huo wa Oktoba 29, 2025.

Waziri Simbachawene amesema hayo usiku wa Ijumaa Novemba 28, 2025 katika burudani ya amani iliyofanyika kwenye Soko la Nyama Choma la Kumbilamoto, Kata ya Vingunguti wilayani Ilala mkoani Dar es Salaam akibainisha kuwa maandamano hayo yalisababisha vifo, uharibifu wa mali za serikali na mali binafsi pamoja na kusimama kwa shughuli za kiuchumi katika maeneo mbalimbali ya nchi.

Simbachawene ameonya kuwa zipo taarifa za mipango ya maandamano mapya yanayotarajiwa kufanyika Desemba 9, 2025, akisisitiza kuwa Serikali haitaruhusu kutokea kwa vurugu nyingine na kuwaomba wananchi kutotumika na kuchochewa kurudia makosa yaliyopita.

Akirejea athari za maandamano ya Oktoba 29, Waziri Simbachawene amewataka vijana kufahamu gharama kubwa za uharibifu wa miundombinu, ikiwemo kuchoma vituo vya mabasi ya mwendokasi- mradi alioutaja kuwa umejengwa kwa ajili ya wananchi wasio na uwezo wa kumiliki magari. Amefafanua kuwa miradi hiyo inagharimiwa na kodi pamoja na mikopo ambayo vizazi vijavyo vitapaswa kuilipa.

Akizungumzia umuhimu wa amani, Waziri Simbachawene amesema Tanzania inaonekana kuonewa wivu kutokana na mafanikio yake, hivyo wananchi wanapaswa kuepuka kuvuruga misingi ambayo imeijengea nchi heshima na utulivu wa miaka mingi. Ameongeza kuwa baadhi ya majirani wa Tanzania wamekumbwa na migogoro kwa muda mrefu, akisisitiza kuwa wananchi wanapaswa kujifunza kutokana na changamoto za mataifa hayo.

“Na leo hii nilikuwa na mkutano mkubwa sana wa utatu kati ya Tanzania, Burundi na UNHCR (Shirika la kuhudumia wakimbizi duniani), tunafikiria namna ya kuwarudisha wakimbizi wale wa Burundi kurudi kwao maana wamekaa hapa karibu miaka 40…sasa tunafikiria warudi kwao kwa sababu masharti ya ukimbizi yameisha hawataki kuondoka, tunafikiria kutumia ushawishi wa nguvu ili waweze kuondoka. Kama wakimbizi hawataki kuondoka kwetu halafu sisi hatuienzi na kuiheshimu amani ya nchi yetu tutakuwa sisi ni wajinga wa mwisho kwa sababu tunaona na kusikia kwa wenzetu kinachotokea”, ameeleza.

Katika hatua nyingine, Waziri pia amewasisitiza wananchi kushirikiana na Jeshi la Polisi, akisema polisi ni sehemu ya jamii na wana jukumu la kulinda usalama wa raia na mali zao.

“Shirikianeni na jeshi la polisi, Jeshi la polisi na wananchi ni familia moja kwasababu kazi ya jeshi la polisi ni kulinda usalama wa raia na mali zake, polisi wawe marafiki zetu…ni marafiki zetu sio marafiki zetu? polisi ni watoto wetu, ni ndugu zetu. Tusigombanishwe na polisi, Polisi ni marafiki zetu na nimewaambia polisi, sasa tunataka tuoneshe aina ya jeshi la polisi ambalo linajenga urafiki na wananchi”, amesisitiza Mhe. Simbachawene.

Friday, 28 November 2025

KILA MMOJA YUPO HURU, HATUINGILIWI NA MAAMUZI YA BUNGE LA ULAYA- SERIKALI

11/28/2025 07:47:00 pm

Serikali ya Tanzania imetoa ufafanuzi kuhusu azimio lililopitishwa na Bunge la Umoja wa Ulaya (EU) Novemba 26, 2025, ambalo lilizungumzia madai ya ukiukwaji wa haki za binadamu nchini na kusababisha Kamisheni ya EU kusubirisha kwa muda utiaji saini wa Programu ya Ushirikiano ya Mwaka 2025 (AAP 2025) yenye thamani ya Euro milioni 156.


Serikali imesisitiza kuwa madai hayo hayana uthibitisho wa kuaminika na yametokana na taarifa za upande mmoja ambazo hazikupata fursa ya kupingwa au kupewa ufafanuzi.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo, Novemba 27, 2025, na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, imeeleza kuwa Serikali ya Tanzania inaheshimu uhusiano baina yake na EU, ambao ni wa kihistoria, wenye zaidi ya nusu karne, na umejengwa juu ya misingi ya mazungumzo, kuheshimiana na kutokuingiliana katika masuala ya ndani ya kila upande.

Imeendelea kueleza kuwa imesikitishwa na hatua ya Bunge la EU kujadili na kupitisha azimio dhidi ya Tanzania bila kuipa Serikali fursa ya kusikilizwa, jambo ambalo linakwenda kinyume na kanuni ya haki ya kusikilizwa (Principal of Natural Justice) inayotambuliwa katika mifumo yote ya utawala bora duniani.

Aidha, Serikali imefafanua kuwa Tanzania ni Taifa huru linaloongozwa kwa misingi ya mamlaka kamili ya kitaifa, hivyo halifungwi na maamuzi ya Bunge la EU na kwamba  kwa mujibu wa taratibu za kidiplomasia, uhusiano rasmi kati ya Tanzania na EU unasimamiwa na Kamisheni ya Umoja wa Ulaya na si Bunge lake, hivyo maazimio ya chombo hicho hayawi maagizo ya moja kwa moja kwa Serikali.

Kuhusiana na mijadala iliyoibuka kuhusu hatima ya misaada ya EU kwa Tanzania, Serikali imeweka wazi kuwa hakuna misaada iliyositishwa; badala yake, Kamisheni ya EU imesubirisha kwa muda utiaji saini wa Programu ya AAP 2025 ili kutoa nafasi ya mashauriano ya ziada.

Serikali imebainisha kuwa programu nyingine zote zilizokwishaidhinishwa na zinazoendelea kutekelezwa hazijaathiriwa na uamuzi huu; hivyo, taarifa zinazoenezwa kuhusu kusitishwa kwa misaada kwa ujumla wake hazina ukweli wowote.

Aidha, Serikali imetoa wito kwa Watanzania kupuuza taarifa potofu zinazoenezwa mitandaoni kuhusu suala hilo.
Adbox